Tupeane uzoefu kidogo katika biashara hii ya Ng'ombe

Tupeane uzoefu kidogo katika biashara hii ya Ng'ombe

Kama una eneo la kuwatunza naona kunenepesha ni nzuri.
Unakuwa tu na lishe ya kutosha na upatikanaji wa majani kwa urahisi.
 
Mfumo mmbovu kuliko wote ni wa kununua mnadani na kuuza,Na kununua ndama uje uwalee ndiyo uuze nao hovyo kabisa.
Hapo mpango mzima ni kununua ng'ombe wa Maziwa wenye Mimba na kuwauza.Rudi tena nikupe sababu ya hiyo mifumo mibovu.Nishapita kote huko.



Sent using Jamii Forums mobile app
Karibu mkuu unielimishe japo kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini umechagua ngombe na sio kuku, bata au njiwa ?
Nadhani lazima kuna kitu kimekuvutia hadi ukawaza kufanya hili jambo....

Options zote nina uhakika zina pro and cons.., tafuta hizo na jipime kulingana na uhalisia wako, utapata nini cha kufanya
 
Kwanini umechagua ngombe na sio kuku, bata au njiwa ?
Nadhani lazima kuna kitu kimekuvutia hadi ukawaza kufanya hili jambo....

Options zote nina uhakika zina pro and cons.., tafuta hizo na jipime kulingana na uhalisia wako, utapata nini cha kufanya
Asante Sana kwa mawazo yako
Ila mkuu niliomba kwa mtu mwenye mawazo au ushauri pia napokea kwa mikono miwili
Hivyo endapo una wazo zuri na lenye manufaa
Naomba unipe nitalipokea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini umechagua ngombe na sio kuku, bata au njiwa ?
Nadhani lazima kuna kitu kimekuvutia hadi ukawaza kufanya hili jambo....

Options zote nina uhakika zina pro and cons.., tafuta hizo na jipime kulingana na uhalisia wako, utapata nini cha kufanya

Labda kaona yule jamaa kadakwa na ARV kwa kunenepesha ng’ombe
Maana watu hupata mawazo kwa matukio, we never know [emoji2957]


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Hii biashara si nyepesi kama unavyofikiria na haina faida kama unavyohisi. Kunenepesha ng'ombe wa kienyeji ni gharama kubwa sana na haichukui hiyo miezi 3 unayohisi, mashudu ya pamba kg 1 inauzwa 1000-1500 kanda ya ziwa fikiria ng'ombe anakula kilo ngapi kwa siku na miezi 6-12 je?

Kununua ng'ombe kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine ni hatari sana wanaweza kukufia wote watapokula majani tofauti na waliyokulia, ndama hawafi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nunua ng'ombe,pakia kwenye fuso kauze,nunua mnada huu,uza mnada ule,nunua mnada huohuo ila nje ya mnada,ingiza mnadani kula Cha juu hata hamsini hamsini,
Hivyo ndo wanafanya wanaotaka kupandisha mtaji chap chap,kuliko ufuge usubiri faida miezi mitatu mbele
Huu ndio ukweli wa hii biashara kawaida faida halisi ikizidi sana ni laki moja, unatakiwa kuwa na mtaji wa ng'ombe walio tayari kuuzwa 100+ ukikusanya hizo 40,50 au 70 kwa 100 ndio utaona faida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom