Kuna siku mchana kulikua na jua Kali hatar, tukashangaa ghafla Kama mvua ya mawe, natoka nje kucheki mvua kubwa ya maharage inanyesha
Wakati bado hatujajua inakotokea ukatua mfuniko wa pressure cooker ktkt ya uwanja, na michuzi ya kutosha
Kabla hatujageukiana na Maza kwa mshangao mtu akagonga hodi, kijana mmoja akasema samahani nimekuja kuchukua mfuniko wangu,
Kaja na fagio, akafagia amebeba na mfuniko, alipoondoka jmn tulilupuka kwa kicheko tukiwa ndani,
Lilikua kundi la wakaka wa geto kwa jirani walikua wanachemsha maharage wakafungua mfuniko kucheki Kama yameiva bila kuepua, gesi yote na mvuke ukainyanyua sufuria ikapaa na maharage yakavuka fensi kuja kwetu