Tupia jina la memba mmoja wa JF ambaye katoweka humu

Tupia jina la memba mmoja wa JF ambaye katoweka humu

Asante sana kwa heshima hii nisiyostahili uliyonipa.

Hata ningestahili heshima hiyo, bado naona changamoto nyingi.

Changamoto kubwa imekuwa ni kufuta nini kisichotakiwa kusemwa kutoka nini kinachotakiwa kusemwa (redaction). Kwa sisi tusiotegemea magazeti, unaweza kukaa na mzee wako yuko barazani (la mawaziri) akaongea nawe kama mazungumzo ya familia, wewe ukahamaki kesho ukayaelezea hapa isivyofaa, unaweza kuhatarisha usalama wa watu wasio na hatia.

Nyingine ni kusema kwa staha itakayohimiza na kutunza heshima katika ulimwengu ambao hauna heshima hata kwa wenye heshima. Ni vigumu kusemezana sana na watu wengi, hususan kama wengine hawajui kanuni za kusemezana kwa staha hata ndogo tu ya kujuana na kuheshimiana kama jamaa moja angalau kwa uraia.

Kijamii, kwa upande, hatujawa na utayari kwa habari zenye ukweli unaohitajika. Upande mdogo ambao tumepata huo utayari hatujawa na mipango ya kuendeleza hizo habari zikishapatikana.

Ndiyo maana nikiongea na ahali zangu fulani wanaojua yanayoendelea kwa undani, wanashauri kuendeleza biashara zetu na ustawi wa familia ughaibuni tu.

Maana nikiangalia email za balozi za Tanzania nje mpaka mazungumzo ya watu wa ndani ni shida.

Na hapo kuna wazee wangu nawaheshimu wanaendesha mambo.

Inaelekea ufahamu ni bidhaa adimu.

Na kulazimu adimu ni wazimu.
Mkuu Mdogo wako wamempiga ban!!
Msalimu sana
 
Mkuu Mdogo wako wamempiga ban!!
Msalimu sana
Yule kisirani chake anakijua mwenyewe.

Dakika moja anaongelea usomi na kuhubiri upole kama mtawa wa ki Buddha (alisoma sana temple, kisha akaipotezea akaenda kujichanganya Wall St), dakika nyingine, akishaona umemvunjia heshima tu, anakufurumushia matusi ya kichaa kumshinda 2Pac mpaka unashangaa kama huyu ni mtu yule yule au tofauti.

Anasema hapa wajinga wengi na bora hata hivyo anavyopigwa ban, maana akiwepo sana ataishia kutukanana nao tu, kitu ambacho kinaweza kuwa si kizuri kwa wasiostahili kuona uchafuzi wa jukwaa.

Yupo New Orleans sasa na bibie wake wameenda ku party Fat Tuesday ya Mardi Graas.
 
Nimemsahau yule aliyekukuwa anatupa mambo ya Mr 900 inapendeza manake yeye mpaka urusi alifika. Nani nisaidieni
 
Back
Top Bottom