Turudi nyuma kidogo, ilikuwaje CHADEMA wakasusa katikati ya bunge la katiba?

Turudi nyuma kidogo, ilikuwaje CHADEMA wakasusa katikati ya bunge la katiba?

John Mloy

Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
39
Reaction score
157
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa CHADEMA chini ya mwamvuli wa UKAWA walisusia bunge la katiba likiwa katikati ya majadiliano na likiwa ktk hatua nzuri ya kupata katiba nzuri ya wananchi. Sababu kubwa ya kususa ilikuwa ni kutokubaliana na CCM juu ya muundo wa Mungano, wakati CHADEMA wakitaka muundo wa serikali tatu, CCM wao walitaka tubaki na serikali mbili kama ilivyo sasa.

Mimi kwa mtazamo wangu naona wapinzani walipoteza nafasi muhimu kabisa ya kupata katiba mpya kwani ktk mchakato kama ule huwezi kupata kila kitu, ni lazima ukubali kupoteza baadhi ya mambo ili mengine yaende. Kwa mfano kwenye ile rasimu kulikuwa na mambo mengi mazuri zaidi ya muundo wa muungano. Tungekubali kuliacha hilo lkn tungepata mengine kama tume huru, kuhoji uchaguzi wa rais mahakamani na mengine ambayo sio ya ksiasa kama haki za wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, walemavu na makundi mengine, hlf hilo la muundo wa muungano lingeweza kuja baadaye baada ya kupata hiyo katiba mpya. Lkn ksbb wanasiasa siku zote ni wabinafsi na wanavutia upande wao, hatma yake tumekosa yote.

Sasa miaka sita baadaye ndo tunataka tena katiba mpya ktk serikali ambayo ina vipaumbele tofauti na haina interest tena na mambo ya katiba mpya...

Je mchakato wa katiba mpya utafanikiwa ktk utawala huu wa awamu ya sita? Kwa maoni yangu inawezekana lkn itakuwa kwa mbinde sana, itatumika nguvu kubwa sana kufikia hatua tuliyokuwa tumefika kipindi kile. Na lazima tujifunze kutowaachia wanasiasa pekee ndo waamue hatma ya maisha yetu.

Mungu ibariki TANZANIA.
 
Usichanganye madesa bhana! Waliosusia lile Bunge la Katiba walikuwa ni UKAWA! na siyo Chadema kwa mwamvuli wa UKAWA.

Na sababu zao walishazitoa kitambo. Binafsi naamini JK hakuwa na dhamira ya 100% ya kutupatia Watanzania Katiba Mpya!

Na ndiyo maana alijaza Wanasiasa kwenye lile Bunge, badala ya Wataalam wengi Wazalendo na Wanasiasa wachache.
 
Ila jua kwamba baada ya CHADEMA(UKAWA) kujitoa mchakato wa katiba uliendelea hadi kufikia wajumbe waliobaki kupiga kura na pia wajumbe wengine wakiwa nje ya nchi wakaonekana wamepiga kura ili akidi itimie.

Wakakabidhi kwa mhe. rais halafu ndio ikawa kimya.
 
Mchakato ule!ulianzishwa Ili kupata rasimu AMBAYO itakuja kutumika kupata katiba hapo mbeleni!!Ukawa ikiongozwa na CHADEMA iligomea mchakato ule kwa kupewa maelekezo ya kufanya hivyo kutoka kwa wenye NCHI Baada kuona malengo ya rasimu ya warioba yatasiginwa na wenye chama chao wenye Uchu wa madaraka!!!CCM wanaichukia Sana CHADEMA Sio tu kwasababu ni chama pinzani bali kwa kuwa Mwenyekiti wake anafanya kazi na wenye NCHI kustabilize serikali ya CCM AMBAYO imetekwa na mafisadi kwa jina la wenye chama!!KWAMBA chama kina wenyewe!!!kama Baba wa Taifa alivyoanzisha TANU Baadae CCM hivyo hivyo na CHADEMA itazaa chama kingine kipya ambacho kitakuja kutwaa madaraka huko mbeleni!!!na Mwenyekiti ataanza kwa kuwa Waziri mkuu hapo Baadae kabla chama hicho kigeni hakijaa twaa madaraka!!!
 
Hakika CHADEMA walifanya mistake inayowafanya wajutie. Kwa sasa fedha zipelekwe ktk miradi ya maendeleo
 
John Mloy,

..ccm ambao waliendelea na mchakato walitakiwa watupatie katiba mpya yenye mambo mazuri uliyoyaorodhesha isipokuwa serikali 3.

..mchakato wa kupata katiba ulikuwa hautegemei uwepo wa vyama vya upinzani ktk bunge maalum.

..Ccm walihakikisha kwamba wanaingiza idadi ya makada ya kutosha ktk bunge maalum ili katiba mpya iandikwe vile wanavyotaka Ccm.

..Lawama zinatakiwa ziende kwa Ccm. Kwanza walikuwa na akidi ya kutosha kuandika ktk mpya. Pili waliendelea na mchakato mpaka mwisho.
 
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa CHADEMA chini ya mwamvuli wa UKAWA walisusia bunge la katiba likiwa katikati ya majadiliano na likiwa ktk hatua nzuri ya kupata katiba nzuri ya wananchi. Sababu kubwa ya kususa ilikuwa ni kutokubaliana na CCM juu ya muundo wa Mungano, wakati CHADEMA wakitaka muundo wa serikali tatu, CCM wao walitaka tubaki na serikali mbili kama ilivyo sasa.

Mimi kwa mtazamo wangu naona wapinzani walipoteza nafasi muhimu kabisa ya kupata katiba mpya kwani ktk mchakato kama ule huwezi kupata kila kitu, ni lazima ukubali kupoteza baadhi ya mambo ili mengine yaende. Kwa mfano kwenye ile rasimu kulikuwa na mambo mengi mazuri zaidi ya muundo wa muungano. Tungekubali kuliacha hilo lkn tungepata mengine kama tume huru, kuhoji uchaguzi wa rais mahakamani na mengine ambayo sio ya ksiasa kama haki za wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, walemavu na makundi mengine, hlf hilo la muundo wa muungano lingeweza kuja baadaye baada ya kupata hiyo katiba mpya. Lkn ksbb wanasiasa siku zote ni wabinafsi na wanavutia upande wao, hatma yake tumekosa yote.

Sasa miaka sita baadaye ndo tunataka tena katiba mpya ktk serikali ambayo ina vipaumbele tofauti na haina interest tena na mambo ya katiba mpya...

Je mchakato wa katiba mpya utafanikiwa ktk utawala huu wa awamu ya sita? Kwa maoni yangu inawezekana lkn itakuwa kwa mbinde sana, itatumika nguvu kubwa sana kufikia hatua tuliyokuwa tumefika kipindi kile. Na lazima tujifunze kutowaachia wanasiasa pekee ndo waamue hatma ya maisha yetu.

Mungu ibariki TANZANIA.
Well written John Mloy. Hekima ni kitu adimu sana ambacho viongozi wa CDM hawajajaaliwa. Ile Bunge Maalum la Katiba ilikuwa kama watu wanaandika mkataba. Kwenye mkataba wowote watu wanaangalia win win situation. Walipaswa kukubali some of things wasizozipendelea as long as zingine za kwao zimekubalika.

Pangekuwa mahali pazuri pa kuanzia, with amendments provision in the future.
 
Back
Top Bottom