Tusahau ya kampuni ya NICOL, hii ndio biashara itakayotutoa sisi watanzania

Tusahau ya kampuni ya NICOL, hii ndio biashara itakayotutoa sisi watanzania

Ndugu mnafuatatilia mada hii, napenda kuchukua fursa ya mjadala huu kuwaomba wale wanaomiliki hisa katika makampuni ambayo hisa zake zinauzwa kwenye soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) kama vile TWIGA, TBL, CRDB, n.k. kushiriki katika utafiti wangu.

Nimeandaa dodoso ambayo unaweza kujaza online, kwa kugonda kwenye link ifuatayo:

https://www.surveymonkey.com/s/58DLYW8

Ukimaliza kujaza, bofya kitufe cha "Done", nayo itanifikia mara moja.

Natanguliza shukrani za dhati, kwa wale watakaopenda kuchangia katika utafiti huu.
 
Bado wachanga tukikuwa tutafika.

Kwanini usianzishe?

Hapo wa kuogopwa ni huyo jamaa mwenye briefcase.
 
Napenda sana hizi mutual funds but lazima nikiri naziogopa nikichek ya nicol hata yaliyotokea kwenye financial crisis huko USA jinsi hao managers walivyocheza na investments za watu bei za hisa zikaporomoka watu wakala hasara while wao managers wakijilipa bonus na kusepa nakiri napata uoga kwakweli though kuunganisha mitaji its the best idea kwa watu na mataifa maskin kama yetu ili kustay competitive
 
Bado wachanga tukikuwa tutafika.

Kwanini usianzishe?

Hapo wa kuongopwa ni huyo jamaa mwenye briefcase.

DADA YANGU FAIZA FOXY vitu kama hivyo huwezi kuanzisha mwenyewe kuna vitu vingi vya kuangalia
kama

board of trustee n.k

Hapa sasa ndiko kuna msala kwani ni lazima uweke watu experienced na wenye hadhi fulani katika jamii hiyo na kwa nchi zetu hizi hizi Mutual Funds zinazokufa kila leo watu wengi wanaogopa viti hivi kwani wanaamini kibaya chochote kikitokea CV zao zitaharibika

na kama ujuavyo Investment Business ni business yenye ku contain risk sana
 
Napenda sana hizi mutual funds but lazima nikiri naziogopa nikichek ya nicol hata yaliyotokea kwenye financial crisis huko USA jinsi hao managers walivyocheza na investments za watu bei za hisa zikaporomoka watu wakala hasara while wao managers wakijilipa bonus na kusepa nakiri napata uoga kwakweli though kuunganisha mitaji its the best idea kwa watu na mataifa maskin kama yetu ili kustay competitive


But kwa wenzetu wana MF ambazo ziko strong sana pamoja na kitokea kwa ile inshu ya 2008 iliyopelekea Kupotea kwa ramani kwa
LEHMAN BROTHERS
 
Kwa miaka mingi sana nimefikilia swala la kuleta hizi financial vehicles kwenye Tanzania market, nadhani Umoja Fund is some kind of mutual fund lakini there is very few information kuhusu fund. Ukweli ni kwamba Watanzania hawana knowledge ya kutosha kuhusu MF, pili hakuna sheria ya kuongoza MF na tatu lack of liquid investment vehicles nayo inachangia. Kama utatengeneza MF Portfolio it is obvious kwamba utawekeza kwenye Kilimo na Private Equity (ambayo nayo ni mzozo kwa bongo).

Kama kuna mtu ambae yuko interesting na kuexplore this sector, am willing to share some information. Cha muhimu ni how to raise capital investment fund, kudetermine ROI, kujua jinsi ya kulobby TZ government to write a guideline laws.


Mkuu kwanza kabisa naomba nishukuru kwa kuchangia mada hii

mie binafsi niko interesting ku explore this sector lakini ni vyema kabisa kama ni information tu share hapa ili mimi, yule na wao waweze kujua na kufumbua upeo wao kuhusu hizi financial vehicles
 
DADA YANGU FAIZA FOXY vitu kama hivyo huwezi kuanzisha mwenyewe kuna vitu vingi vya kuangalia
kama

board of trustee n.k

Hapa sasa ndiko kuna msala kwani ni lazima uweke watu experienced na wenye hadhi fulani katika jamii hiyo na kwa nchi zetu hizi hizi Mutual Funds zinazokufa kila leo watu wengi wanaogopa viti hivi kwani wanaamini kibaya chochote kikitokea CV zao zitaharibika

na kama ujuavyo Investment Business ni business yenye ku contain risk sana

Usijifunge mwenyewe, weka proposal na feasibility yako vizuri, ikikaa sawa ntakusaidia kupata wadhamini na hata wawekezaji.
 
Usijifunge mwenyewe, weka proposal na feasibility yako vizuri, ikikaa sawa ntakusaidia kupata wadhamini na hata wawekezaji.


safi sana dada yangu natumaini hata watu ambao walikuwa hawajui waanzie wapi nahisi kwa post yako itatoa mwanga sana kwa vijana
 
Hizi nondo nimezipenda sana mkuu C.T.U Mi nikajua wewe unakaunta tera peke yake kumbe hata huku kwenye uchumi unakaunta tera pia.
 
Last edited by a moderator:
Hizi nondo nimezipenda sana mkuu C.T.U Mi nikajua wewe unakaunta tera peke yake kumbe hata huku kwenye uchumi unakaunta tera pia.

kawaida tu mkuu
kidogo kidogo tunajifunza kutoka kwa waungwana wengu tu hapa jf
 
Mutual fund ni very interesting financial investment tool, kuna mambo mengi sana yakuangalia before to put it pamoja. Lakini important zaidi ni diversification of risk, na hii unaweza kuipata tuu kama utakuwa una sector mbali mbali ambazo unaweza kuwekeza na kujua parformance ya hizo sector historical. Tatizo la Tanzania ni kwamba kwanza hakuna sector nyingi ambazo zipo public, nyingi ni private na Wanye sector hizo hawaitaji mitaji kutoka kwa watu private wanategemea sana Bank. Pili sheria za Tanzania zinabana kupeleka mitaji nje ya Tanzania, hivyo huwezi kutoa pesa Tanzania kuweka kwenye world largest index kama SP 500.

Hivyo option kubwa Tanzania ni kuwa na Private Equity, ambayo hii unaweza kuamua unawekeza kwenye sector mbili au tatu then kutokana na ROI za ile investment unaweza toa dividend kwa investors in quarterly base na kuonyesha Portfolio growth. Huwezi chukua western private equity model na kuimplement Tanzania, it will never work. Hivyo creativity ndio key kubwa sana. You need to be creative kwa kutengeneza mfumo unaondena na mfumo wa Tanzania.

Kikubwa sana ni first, how are you planning to raise capital? This is a focal point, sababu kunaitajika enough liquidity ya kufanya wewe uweze kujiendesha na wewe uweze kuwekeza. Pili, wapi utawekeza hizi fedha, what are the guidelines za kuwekeza na ni kwa vipi those guideline will be parallel to Tanzania law. Tatu, You will need your own money to win the trust of other people monies. Mimi nilipiga mahesabu ya at least million 100 kuanzia na hii ni portfolio capital not cash to run operational, you will need that too.

Mwisho you need investment salesman, na hawa ni wagumu sana kuwapata Tanzania. People who knows how to make a pitch on Investment vehicles.
 
kutumia ni muhimu kwa uchumi kukua. kuweka akiba kuna faida pale tu akiba hiyo inapowekezwa. Akiba kidogo zinapounganishwa huwa akiba kubwa ambayo huweza kuwekezwa katika mradi mkubwa wenye manufaa makubwa. Watanzania tuna matatizo matatu makubwa: kwanza hatujiamini, pili hatuaminiani na tatu ni umimi. NICOL ilikufa kwa vile wenye nguvu za kisiasa na kiushawishi hawakuwaamini wale wenye weledi na kuthubutu. badala ya kuweka nguvu za fikra na fedha kwenye kapu moja tukaingia kwenye malumbano ya kipuuzi na kupambana kama panzi huku kunguru akina rabo bank, Kempisk na wengine wakijitwalia mali zetu bure bwerere. Serikali ya Tanzania inaongozwa na ndugu zetu wasiojua tofauti kati ya wageni na wazawa. wao anafikiria ili mradi kampuni iko nchini na inalipa kodi basi inachangia sana kukuza uchumi. mutual funds tukizielewa vema tukazianzisha na kuziendesha kiadilifu zitaweka uchumi wetu mikononi mwetu. lakini ili tuumiliki uchumi utakaokuwa mikononi mwetu lazima tuachane na mawazo madogo ya kuwa na biashara yangu tufikirie kuwa na biashara za kutawala sekta nzima. Hivi viduka na vikampuni vya kujenga ghorofa mbli tatu havitaweza kuichangamsha vya kutosha mifuko hii. Tutumie kwa uangalifu, tuweke akiba kwa hekima na tuwekeze kwa kwa umahiri. PAMOJA TUTAWEZA. USHINDI WAHITAJI USHINDANI
 
Kwa miaka mingi sana nimefikilia swala la kuleta hizi financial vehicles kwenye Tanzania market, nadhani Umoja Fund is some kind of mutual fund lakini there is very few information kuhusu fund. Ukweli ni kwamba Watanzania hawana knowledge ya kutosha kuhusu MF, pili hakuna sheria ya kuongoza MF na tatu lack of liquid investment vehicles nayo inachangia. Kama utatengeneza MF Portfolio it is obvious kwamba utawekeza kwenye Kilimo na Private Equity (ambayo nayo ni mzozo kwa bongo).

Kama kuna mtu ambae yuko interesting na kuexplore this sector, am willing to share some information. Cha muhimu ni how to raise capital investment fund, kudetermine ROI, kujua jinsi ya kulobby TZ government to write a guideline laws.

Sheria zipo nenda CMSA watakuelimisha zaidi
 
Serikali ifungue milango waje wawekezaji wa nje wanaoaminika waaanzishe hapa ili tujifunze na sisi.
 
Mutual
Kikubwa sana ni first, how are you planning to raise capital? This is a focal point, sababu kunaitajika enough liquidity ya kufanya wewe uweze kujiendesha na wewe uweze kuwekeza. Pili, wapi utawekeza hizi fedha, what are the guidelines za kuwekeza na ni kwa vipi those guideline will be parallel to Tanzania law. Tatu, You will need your own money to win the trust of other people monies. Mimi nilipiga mahesabu ya at least million 100 kuanzia na hii ni portfolio capital not cash to run operational, you will need that too.

Mwisho you need investment salesman, na hawa ni wagumu sana kuwapata Tanzania. People who knows how to make a pitch on Investment vehicles.

Katika nchi ambayo Fixed Deposits zinzowekwa kwenye mabenki zinalipa hadi 14% inabidi ujipange sana maana RISK ipo juu mnoo. Unashangaa umesha commit funds mwaka mzima kwa 8% ghafla demand ya loanable funds inafikia 14% hapo lazima manager ukune kichwa.
 
Muundo wa wazo la NICOL lilikuwa na bado ni wazo hai. Kukosea njia ndiyo kujua njia. Kuna sababu mbalimbali zilizoikwamisha NICOL kutofikia malengo yake. Ninakumbuka tatizo lilianzia kwenye Initial Public Offer (IPO) kutopata subscribers wa kutosha. Kwa mtazamo wangu, siasa za uchaguzi wa mwaka huo zilikuwa na athari kubwa katika kutofikia malengo ya IPO. Dr. Salim Ahmed Salim na waadilifu wengine wanaoshiriki katika siasa za nchi hii walikuwa wanaiunga mkono NICOL kwa mtazamo wa kuwawezesha wazawa na kuhakikisha hatma ya ubinafsishaji haiishii kwenye kuuza mashirika ya umma kwa wageni na wenyeji wachache. Mtazamo huu ulitafsiriwa kinyume na watawala na waliokuwa wanaandaliwa kurithishwa utawala. Ziliibuka hisia za NICOL kuonekana kama chombo gheresha cha kukusanya fedha za kumfadhiri Dr. SAS. Kwa hiyo badala ya serikali kuwaunga mkono kwa dhati, kukawepo na uhusiano wa mashaka. Pia nia ya mmoja wa waasisi na Kiongozi wa NICOL wakati huo kujiandaa kugombea ubunge katika jimbo ambalo angepambana na shemeji wa Mtawala wetu yalikaribisha misuguano baridi na Serikali. Mwisho wa yote NICOL haikuweza kuandikisha hata nusu ya waraka wa matarajio (Prospectus). Wakapewa muda wa nyongeza lakini bado hawakufikia nusu. Na kutokana na tafsiri potofu ya Watawala wetu hata kile kidogo walichokusanya hawakuweza katika mashirikia waliyokuwa wamelenga. Lengo kubwa la NICOL wakati huo lilikuwa kuinunua Benki ya NMB iwapo ingeuzwa. Baadae ilikuja kuuzwa lakini ikaangukia mikononi mwa Benki ya Wanaushirika wa Netherland (Rabo Bank).

Kwa ufupi, unapokosea, kilicho sahihi si kuachana na jambo ulilokuwa unafanya bali kufanya tathmini kujua kwa nini ulikosea na ulikosea wapi ili ujipange upya kuliendeleza jambo lako kwa usahihi zaidi. Edson angeridhika na kukosea jaribu lake la kwanza, leo hii dunia ingekuwa bado inawasha vibatari.

Kwa uelewa wangu, Deci ilikuwa revolving fund aina ya Ponzi Scheme. Ni tofauti na Mutual Funds. Kwenye mutual funds hatutoi hela kuwagawia wanahisa kwa mgunzumko wa kutegemea mmoja alete na mwingine apewe. Bali tunatoa gawio katika muda maalumu kulingana na hisa za mwanahisa. Na hili linategemeana na matokeo (Profit or loss) ya uwekezaji katika vitega uchumi ambavyo hiyo fund imewekezwa.

Nawashukuru waasisi wake maana miaka hiyo ya 2005 walinipa kibarua kama karani wa uhamasishaji wa manunuzi ya hisa za NICOL pale mlimani. Fursa hii ilinipa nafasi ya kushuhudia uelewa wetu juu ya masuala ya hisa na masoko ya hisa. Kama ulivyosema C.T.U uelewa wetu juu ya masoko ya mitaji, amani na hisa uko chini sana. Nilipita kila corridor, kila idara na kila ofisi pale mlimani. Nami nikiwa ndo nimefunuliwa kujua mambo ya hisa, sikushangaa sana kubaini uelewa wa wanafunzi wa masomo ya Biashara katika maeneo haya bali niliuzunika kutumia muda mwingi kuwaelimisha watu waliokuwa kwenye idara ambazo watu wake wanahusika moja kwa moja na tasnia hii.


Kwa mtazamo wangu kuiachia serikali ianzishe Private Mutual Funds litakuwa kosa la kiufundi. Chombo cha Sekta Binafsi lazima kianzishwe na Sekta Binafsi, Kiendeshwe na Kumilikiwa na Sekta Binafsi. Serikali iwajibike tu kuweka frameworks. Maana chombo kikiisha kuwa Public Limited Company (PLC) lazima Serikali ichukue jukumu lake kulinda maslahi mapana ya umma.

Nimekupa like mkuu,unachoongea ni sahihi kabisa,uelewa wa wasomi tena wa hayo hayo masomo ya biashara juu ya hiz issues ni mdogo sana ,na ukija kwa general public ndo kabisaa patupu. Like nyingine ni kweli kuwa mutual funds inabid iwe kwa muundo wa PLC then mkono wa serikali utaingia kama tu unavyoingia ktk kuhakikisha mazingira bora kwa wawekezaji .kusema kwamba wanasiasa waingie hapa tena ni kurud kule kule tulikotoka
 
C.T.U
Nimekuwa nikiuliza na kujiuliza kama Tanzania tuna Private Sector Pension Scheme na kote nilikouliza sijapata majibu. Nimehoji pia kama Sheria zetu hasa ya Social Security Act na Capital Markets and Securities Act kama zinatoa fursa hii.

Hoja uliyoleta Mkuu C.T.U ni muhimu kuliko watu watakavyoichangia. Tunapohamasisha ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi, mambo makuu ambayo Sekta ya umma popote duniani inayoyatarajia kuyapata kutoka Sekta binafsi la kwanza kabisa ni pesa/mitaji ya kuendeshea miradi, mengine ni teknolojia, na ujuzi wa kusimamia na kuendesha utoaji wa huduma za umma.

Kwa uchanga wa Sekta binafsi ya Tanzania ni dhahiri kwamba bila jitihada ya maksudi tunaweza kujikuta huu ubia unageuka kuwa Public-Foreigners-Partnership na hivyo kuleta tofauti ndogo sana kati ya athari za Ubinafsishaji (Privatization) na Ubia (PPP). Na kwa mifano michache hili limeanza kujitokeza. Mfano nani ameona mbia kutoka Sekta binafsi ya Tanzania ameshiriki kwenye uwekezaji wa miradi michache ifuatayo:
  • Bandari ya Bagamoyo: Mkataba kati ya Serikali na Wachina?
  • GE & Symbion Power na Serikali ya Tanzania?
  • Makaa ya Mawe Mchuchuma-Liganga kati ya Sichuan Hongda Group na NDC (SPV Tanzania China International Mineral Resources Limited)?
  • Uzalishaji wa Umeme Mtwara kati ya China na Serikali ya Tanzania?
Lipo tatizo la ushirikishwaji lakini pia lipo tatizo la Uwezo wa sekta binafsi yetu kimitaji na kiujuzi. Bado sekta ya umma haijatambua kuwa imeruhusu zama za dola kuhodhi uchumi kuwa zilipendwa na wakati huohuo bado sekta binafsi Tanzania haijafahamu uwepo wa fursa ya kuchukua majukumu ya sekta ya umma katika kuendesha miundombinu na kutoa huduma za umma.

Ukijaribu kuliangaza kwa undani tatizo la mitaji ni kubwa zaidi ya mengine na lina athari mbaya sana kwa deni la Taifa katika siku zijazo. Katika mazingira ya PPP niliyozungumzia ni kama hakuna local financial instruments za kuweza kufadhili miradi mikubwa. Miradi ya PPP ni miradi inayohitaji mikopo/mitaji mikubwa inayotumia kipindi kirefu sana katika marejesho (>25 years). Window nyingi zilizopo kwenye taasisi za kifedha nchini ni zile zinazoiva ndani ya muda mfupi. Hakuna taasisi yenye Uwezo wa kukopesha mathalani TZS bilioni 200-300 kwa miradi kama kumi mfululizo ambazo zitalipwa kwa miaka 20. Je, nini athari ya uchumi wa nchi kuwa na mitaji/mikopo mingi iliyotolewa na taasisi za nje, kufadhili makampuni ya nje katika kuendesha miradi ya ndani?

Wazo uliloleta ni moja ya mawazo mazuri ambayo binafsi naafikiana nayo. Ni wakati sasa tuwe na mifuko ya makabwela itakayosaidia katika uwekezaji mkubwa. Tuboreshe sheria zetu za masoko ya mitaji na dhamana (Capital Market and Securities) ziwe kichocheo za Sekta binafsi kujifunza utamaduni wa kuweka hazina (Savings).

Hakuna kitu kimekuwa kikiniuma katika miaka ya hivi karibuni hapa JF kama mada za maana kama hii kukosa wachangiaji.
Mkuu, ulichokisema ni kweli ila umesahau kuwa tatizo kubwa ambalo linachangia kwa Tanzania ni kuwa na wataalamu wachache kwenye suala la uwekezaji na hili ndio linachangia matatizo yote na vitu vyote ulivyo vitaja hapo juu.
Kwa kipindi kirefu Watanzania wamekuwa wana dhana kuwa wahasibu ndio wataalamu wa mambo ya uwekezaji kwa Ulaya na USA pamoja na nchi nyingine zilizoendelea wala sivyo hivyo wataalamu wa uwekezaji ni kama Investment Analyst, Fund Manager ni wazuri kwenye speculating (Speculator) ambao wanahusika na future performance ya miradi sio waatalamu wa uhasibu wanaohusika na past records za kampuni na hapa ndio kunaleta utata kwa Tanzania.
Tunaitaji zaidi wataalamu wa miradindio watakao weza kupeleka miradi mbele. Mimi binafsi ni mtaalamu wa miradi ni Investment Analyst na background yangu ni engineering. Tukiweza kuwa na wataalamu wengi wa miradi tutaona mabadiliko makubwa lasivyo watu kutoka nje yaani wawekezaji watakuja Tanzania watavuna na kuondoka na faida yote na huku tukibakiwa na faida ndogo ambayo haiwezi kuleta mabadiliko makubwa kwenye uchumi wa nchi.
 
Mimi binafsi siwezi kuwekeza kwenye mutual funds hapa Tanzania katika haya mazingira ya sasa. NICOL imechangia woga wangu but kikubwa ni udhaifu wa regulatory authorities kusimamia haya mambo. Mfano kuna watu walifanya Insider Dealing NICOL ikanunua hisa kwenye kiwanda cha dawa cha mdogo wa Mengi, lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa. Hata serikali kuwahoji tu wahusika ili kujiridhisha kuwa hakukuwa na njama zozote za wizi bali ni matatizo ya kiufundi, hakuna, nchi za wenzetu NICOL wangeitwa hadi kwenye parliamentary committee kujieleza lakini hapa kwetu hawajawahi hata kuchunguzwa kama kuna wrong doing.

Mitaji ni tatizo sugu hapa nchini, umebahatisha kamtaji kako then ukapeleke kwenye MF ambako kama wasanii wakichakachua si serikali wala bunge litaingilia kati kujaribu kutetea vijisenti vya wananchi wake ni vigumu sana. Hakuna serious Fraud crackdown in the country, heri niendelee kudunduliza na kuja kutoka at 55 yrs kuliko kudhulumiwa at 35 yrs na nisitoke maishani mwangu mote .
 
..... Mfano kuna watu walifanya Insider Dealing NICOL ikanunua hisa kwenye kiwanda cha dawa cha mdogo wa Mengi....
Kwenye hii acquisition, insider (Dr. R. Mengi) acted in favor of NICOL and its shareholders. Kwanza kwa ku-declare interest kufuatia udugu wa damu na mwenye Kiwanda. Pili akaenda mbali zaidi kupinga huo uwekezaji na alipoona wenzake kwenye Kamati ya Uwekezaji hawamuelewi na badala yake wanamuona kama mtu mwenye wivu wa maendeleo ya mdogo wake, akaamua kujiuzuru ujumbe wa hiyo Kamati. Kwa hiyo hii kama ni kuwa insider dealing haikuwa mbaya. Ilikuwa njema ya kuokoa pesa za wanahisa.

Hata mie naona ni udhaifu mbaya unaoua moyo wa uwekezaji kwa CMSA siku hizo kushindwa kuwachukulia hatua wahusika. Hata majuzi vitabu vyao vya mahesabu vilikuwa na misleading information lakini DSE bado ikaishia kurushiana maneno badala ya kuwachukulia hatua. Mambo yaleyale yametokea kwa Precision Air kuingia IPO ikiwa na mahesabu yenye warakini! CMSA na DSE inabidi waongeze umakini na udhibiti katika kusimamia Sheria ya Uwekezaji wa Pamoja, Sheria ya Masoko ya Hisa na Mitaji ama sivyo watu watapoteza imani kabisa na masoko ya dhamana na hisa.

References:

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Truth at last emerges from NICOL leadership wrangle [/TD]
[TD="class: buttonheading, align: right"] [/TD]
[TD="class: buttonheading, align: right"] [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD] Written by STAFF REPORTER[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: createdate"] Monday, 04 February 2013 07:34[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] The long standing wrangle in the top leadership of the National Investment Company Limited (NICOL) involving one of its former directors, Reginald Mengi, was laid to rest last week during the extra-ordinary meeting of the shareholders held in Dar es Salaam.

Mengi who is IPP Executive Chairman, was alleged to have pushed NICOL to acquire shares in a Moshi based pharmaceutical factory, Inter-chem Pharmaceutical and Beverages Limited (IPBL) in which his younger brother owned shares. ...."Yes, the issue generated a lot of storm in the Board and Mengi was even accused of being jealous of his brother by seeking to undermine him," Dr Kaunda said, adding that the decision to invest in the pharmaceutical factory was nonetheless pushed through by the Board, prompting Mengi's resignation from the NICOL Investment Committee.

Records some of which were made available at the shareholders' meeting show that .....On August 3 2007 Mengi resigned from the chair of NICOL's Investment Committee following his prolonged opposition to NICOL's investment in the pharmaceutical firm alluding conflict of interest – in that his younger owned shares in it.

In his resignation letter to NICOL Board Chairman, Mengi, among others, bitterly criticized the manner the IPBL investment was pushed through saying the investment proposal was not even submitted to the Investment Committee as it was required. In other words, Mengi said in his letter of resignation, the proposal was "approved by the Board without the recommendation of the Investment Committee of which I am the Chairman." .........on September 3 2009 Mengi officially resigned as director of NICOL Board. However Mengi continued to remain a NICOL's shareholder.

One shareholder, Judge Mark Bomani stood up and said after all the issue of NICOL's plan to buy shares was not even presented to the Investment Committee which Dr Mengi chaired.

"This alone exonerates Dr Mengi and the committee from any involvement in pushing the deal through," said Judge Mark Bomani, who was also former Attorney General.

Judge Bomani who was member (director) of the first NICOL Board and its Vice Chairman said he resigned from the Board due, to among other reasons, the controversy surrounding NICOL's investment in IPBL.

Another NICOL shareholder Athumani Ramadhani Athumani even begged Mengi to use his business experience to supply his experts to advise NICOL so as to see it overcome its present challenges.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]NICOL yamsafisha Mengi
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD] Imeandikwa na Christopher Gamaina, Dar es Salaam[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: createdate"] Jumanne, Januari 29, 2013 16:31[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Kampuni ya Taifa ya Uwekezaji (NICOL), imemsafisha mfanyabiashara maarufu nchini, ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni za IPP, Reginald Mengi kuhusu tuhuma za kuidhoofisha kampuni hiyo. Mwenyekiti mpya wa Bodi ya NICOL, Gideon Kaunda na mmoja wa waanzilishi wa kampuni hiyo, Jaji msataafu Mark Bomani wamemsafisha Mengi katika Mkutano Mkuu wa wanahisa uliofanyika Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Awali kabla ya kusafishwa, Mengi alitishia kuondoka mkutanoni iwapo Mwenyekiti hangemweleza msimamo wa NICOL kuhusu tuhuma zilizokuwa zikielekezwa kwake kwamba ameiua kampuni hiyo.
"Mengi yameelezwa mitaani kwamba Mengi kaua NICOL. Kama bado hayo yapo niombe mamlaka niondoke hapa [mkutanoni]," alisema Mengi na kuendelea:
"Yaliyoelezwa kuhusu mimi ni uongo. Wanasiasa wameingilia, Naibu Waziri mmoja ameshiriki kueneza habari hizo, sasa hali hiyo inanipa shida, nataka kujua hali ilivyo juu yangu ndani ya NICOL nione kama ninaendelea kukaa, au nitoke."
Akijibu hoja hiyo, Kaunda alisema kitendo cha Mengi kuhudhuria mkutano huo (kama mwanahisa) kinadhihirisha kwamba yaliyosemwa juu yake ni ya uongo.
"…mimi sikubaliani na shutuma hizo, vyombo vya habari vina matatizo yao, sina tatizo na Mengi ni mwanahisa na mwanzilishi wa NICOL, hilo naomba tuliache na tutoke hapa tumelielewa vizuri," amesema.
Naye Jaji Bomani katika kumtetea Mengi alisema: "Ninapenda kumsafisha Mengi, alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji [ya NICOL]. Aliposikia tuhuma zinazomkabili aliandika barua ya kujiuzulu."
Kwa upande mwingine, Kaunda ameuambia mkutano huo kwamba malumbano baina ya wanahisa wa NICOL yamesababishwa na uozo wa uongozi wa zamani wa kampuni hiyo.
Baada ya majadiliano, mkutano huo wa wanahisa wa NICOL umeazimia kwamba Mwenyekiti wa zamani wa kampuni hiyo, Felix Mosha alazimishwe kukabidhi ofisi viongozi wapya washike hatamu.
"Mosha akishindwa kuachia ngazi na kukabidhi ofisi kwa hiari tutamtoa kwa lazima kuiokoa NICOL," amesisitiza Kaunda.
Inaelezwa Mosha ameongoza NICOL kwa kipindi cha miaka 10 huku kampuni hiyo ikikabiliwa na matatizo lukuki ikiwamo hasara ya Sh bilioni 9.874 kati ya mwaka 2007 na 2009.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Kwenye hii acquisition, insider (Dr. R. Mengi) acted in favor of NICOL and its shareholders. Kwanza kwa ku-declare interest kufuatia udugu wa damu na mwenye Kiwanda. Pili akaenda mbali zaidi kupinga huo uwekezaji na alipoona wenzake kwenye Kamati ya Uwekezaji hawamuelewi na badala yake wanamuona kama mtu mwenye wivu wa maendeleo ya mdogo wake, akaamua kujiuzuru ujumbe wa hiyo Kamati. Kwa hiyo hii kama ni kuwa insider dealing haikuwa mbaya. Ilikuwa njema ya kuokoa pesa za wanahisa.

Hata mie naona ni udhaifu mbaya unaoua moyo wa uwekezaji kwa CMSA siku hizo kushindwa kuwachukulia hatua wahusika. Hata majuzi vitabu vyao vya mahesabu vilikuwa na misleading information lakini DSE bado ikaishia kurushiana maneno badala ya kuwachukulia hatua. Mambo yaleyale yametokea kwa Precision Air kuingia IPO ikiwa na mahesabu yenye warakini! CMSA na DSE inabidi waongeze umakini na udhibiti katika kusimamia Sheria ya Uwekezaji wa Pamoja, Sheria ya Masoko ya Hisa na Mitaji ama sivyo watu watapoteza imani kabisa na masoko ya dhamana na hisa.

References:

Haimaanishi kuwa moja kwa moja Insider ni Reginald Mengi, but upo uwezekano katika hao waliopingana na ushauri wa Mengi wapo waliokula njama kununua kampuni ambayo inakufa kwa bei kubwa na kupoteza kiasi kikubwa cha hela za NICOL ambazo kamwe haziwezi kurudi na zilizotoka kwa wavuja jasho waliopoteza nguvu zao kwa miaka mingi kuzipata. Na yet hakuna mamlaka ya serikali iliyojaridbu kujiridhisha kama kuna element yoyote ya wrong doing.

Kwa mtazamo wangu CMSA na DSE ni majanga ya kitaifa ambayo yanaundwa na watu ambao kwa kiasi kikubwa hawakuwahi kufanya biashara. Ni watu ambao walikuwa maofisini kwa miaka mingi, hawana competence katika kufanya biashawa wao wenyewe. Hatu Wall Street hapa Tanzania, lakini kama nchi lazima tungezitafutia experts wa kiwango cha juu hizi taasisi ili zisukume mbele gurudumu. Nionavyo mimi hata wale waliopeleka fedha zao Precission wanaelekea kule kule kwa NICOL, haiwezekani kampuni iliyopata faida mwaka mmoja uliopita iangukie kwenye biggest loss in aviation industry.

Athari za kutokuwa na usimamizi imara katika masoko ndio hizo zinadidimiza uchumi na hivyo watu wengi kushindwa kupeleka fedha zao kwenye MF. Mfano mkubwa kuna vijana wa Kitanzania kwa mamia sasa hivi wananunua maplot makubwa ya mashamba huku hawajui hata watayafanyia nini. Nilishuhudia jamaa yangu akitoa milioni 20 miaka miwili iliyopita kununua shamba ambalo hadi leo ni pori na sidhani kama amelitembelea katika huu mwaka. Hiyo hela angeipeleka katika mutual funds huenda angejipatia ka return kidogo, lakini the risk is too high. Vijana wanaona heri wamiliki ardhi ambazo huenda watakufa na kuziacha hazina hata mti wa mwembe kuliko hizo Mutual Funds
 
Back
Top Bottom