Tusaidiane faida na changamoto za kuweka milango ya aluminium kwenye nyumba ya kuishi kama mbadala wa milango ya mbao milangoni?

Tusaidiane faida na changamoto za kuweka milango ya aluminium kwenye nyumba ya kuishi kama mbadala wa milango ya mbao milangoni?

Kama ni mlango wa kuingia ndani ya nyumba Inategemea na usalama uliojiwekea.
Manake kwenye ofisi nyingi za biashara wanatumia hata milango ya vioo .
Ila ulinzi ni madhubuti
Mlangobwa kuongili naweka wa chuma mkuu

Nilifikira vyumbani niweke aluminium vp hapo???
 
Karibuni wakuu.
Kwanza Mlango wa Aluminium ni bei nafuu. Frem moja ya Mlango ubao wa Mninga unapigwa hadi laki 3, Mlango wenyewe laki 6 hadi 8. Jumla gharama za Mlango mmoja ni 1 M, lkn aluminium mlango mmoja i Laki 3-6 kutegemea na unene wa kioo na aina ya chuma.

Pili aluminium inahimili ajali ya moto. Hatuombei mabaya lakini amini nakwambia inapotokea ajali ya moto aluminium yaweza kuwa msaada.

Tatu aluminium ni tiba ya mchwa na wadudu wallnaokula mbao.

Nne Aluminium inahamishika kirahisi kutoka nyumba moja kwenda nyingine pale unapoamua kubadili mazingira maana ni kitendo cha kufungua kwa srewdriver. Lakini mlango ujengewa kwa cement nk.
Tano aluminium ni rafiki wa mazingira. Fikiria ni miti mingapi inapoteza Uhai ili nyumba yako ikamilike? Chukua hatua kwa kutumia aluminium.

Mbao.
Mbao ni aghali.
Mbao zinaleta mvuto endapo utaamua kuweka maua na urembo.
Mbao zinakuza uchumi wa ndani maana zinatengenezwa hapa hapa.
Wakuu Karibu Mihogo ya kuchoma hapa Mtaa wa Mfaranyaki ndani ya Songea nyumbi bombi hapa.
 
Back
Top Bottom