Tusichoke Kuyajadili Matatizo Ya Simba

kuifikia yanga ni kazi ngumu. jaribu kuanalia mechi ngapi zimebaki kwa timu zote ukiacha hiyo ya wahusika .angalia away games za samba na yanga ila yanga ina mbinu ya kubutua ugenini na kupaki basi huku wakiwavuta maadui eneo lao ili wakijisahau watu wanapiga bao ulinzi unaendelea,
 

Unaongea kama hujala siku tatu.
 
teh teh, nahisi fedha zote zinaishia kwa Okwi, naonaga anajituma zaidi ya wenzie

Hili ndilo tatizo linaloikabili timu ya simba, Timu ipo kwa matabaka ya akina Okwi na waganda wenzake na tabaka la Akina Singano na wabongo wengine.
 
tukubali kuwa na subira hadi vijana watakapokomaa lkn najiuliza tumsubiri messi akomae??

Mi nashangaa sana....kwani pale simba hao tunaowaita vijana ni kina nani? Naona hii ni excuse ya kipumbavu tu
 
Bado Mzimu Wa Wambura Unafurukuta Klabuni.
 
Mi nashangaa sana....kwani pale simba hao tunaowaita vijana ni kina nani? Naona hii ni excuse ya kipumbavu tu

Aliowatumia Lewig Ndo Haohao Aliowatumia Kibaden, Na Haohao Ndio Kawatumia Logarusic, Halafu Wakaendelea Kutumiwa Na Phiri, Sasa Bado Wanaendelea Kutumiwa Na Goran.... Wanasimba Endeleeni Kuwa Wavumilivu Katika Kipindi Hiki Kigumu Hadi Miaka 10 Ijayo, Vijana Watakuwa Wamekua.
 
Matatizo ya mpira wa Tanzania ni mengi. Mikia bado mnakabiliwa na tatizo la viongozi kujifanya ndio makocha. Kama bado lipo Yanga litakuwa ni kidogo sana lakini naamini kwa sasa halipo. Kuna kocha mwingine katimuliwa kwa kukataa kupangiwa timu ya kucheza. Kocha aachiwe abebe mzigo wake ili akivurunda uwe mzigo wake mwenyewe.

Lingine lipo hata kwa Yanga. Tunaajiri makocha wakati tumeisha sajili kwa vigezo vyetu mbuzi kabisa. Wanaweza kuwa wachezaji wazuri lakini wasiendane na mfumo na filosofia ya kocha. Hilo linachangiwa na kutimuatimua za makocha kila wakati. Kocha kumaliza mwaka Yanga na Simba kwa sasa ni ndoto. Wanatimuliwa na kurudishwa baadaye. Tumeishakuwa shamba la bibi. Anatimuliwa analipwa haki zake baada ya miezi sita anakuja tena.

Kwa hili la makocha Azam wameling'amua. Wanampa muda mwalimu afanye kazi yake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…