Hii kauli ilithibitisha kuwa CCM imefanikiwa kufikia kiwango cha juu cha ujeuri kiasi cha kutohitaji tena ridhaa ya wananchi kubaki madarakani. Na inawezekana Watanzania wengi kufikiri kuwa hili ni tatizo la “wapinzani” - wao hawahusiki. Na hapa ndipo lilipo janga la taifa letu “national tragedy”. watu kufikiri kinachoendelea kwenye siasa ni matatizo ya Magufuli vs Lissu & Kabwe, Gwajima vs Mdee, Tulia vs Sugu, n.k.
Watanzania wangefahamu kuwa nchi kama Equatorial Guinea, Central African Republic na Congo DR zilipitia hatua hizi hizi kufikia majanga ya kitaifa yanayozitesa hadi leo, wasingepuuza (ignore) na kujivua wajibu wa kusimamia viongozi wa kisiasa kiasi cha kuwapa jeuri ya aina hii. Labda siku maumivu yakikolea kwa wengi, ndipo unafiki utawekwa pembeni.
Ndio maana nimeshauri wafanye haya hapa chini vinginevyo hawatoboi:
Ndugu ndugu wapinzani,
Mumeona jinsi munavyo enguliwa na hao NEC bila sababu za msingi.
Mumeona jinsi haki yenu ya uchauguzi isivyopatikana kwa watu wetu kuengulia kwa sababu ya msingi (Breaches of Fundamental rights)
Mumeona jinsi mapingamizi yenu yanatupwa bila sababu za msisngi...
Hivi kweli mnavyoona mtapa haki sawa huko mbeleni? Thubutu
Kwa nini msiwafunguliwe kesi ya ubaguzi hao NEC na muiombe mahakama iistopishe NEC kuendesha au kusimamia zoezi zima la uchaguzi huu?
Kuendelea nayo hii NEC ya sasa maana yake ni kwamba :
1. Mumekubaliana na figisu zote za NEC za sasa
2. Mumekubali kwamba wakisha tangaza matokeo (Uraisi) hamtaweza kuyapinga au kuyahoji mahala popote Tanzania maana ni kinyume na sheria
3. Mumekubali kwamba uchaguzi utakuwa free na fair ingawaje yale yale yaliyotokea serikali za mitaa yanajirudia.
4. Mkiishitaki NEC kwa certificate of urgent (breaches of fundamental rights ) kwa kuwapendelea CCM au kwa kutofuata sheria za uchaguzi na kanuni zake kinachoweza kufanyika ni kati ya haya yafuatayo:
1. Mahakama kuwarudisha wagombea wote walionguliwa kwa sababu za magumashi
2. Mahakakam kuisimamisha NEC kuendela na zoezi zima la uchaguzi mpaka hapa watakopo kuwa wameonyesha kwamba wao sio biased
3. Mahakama kuagiza tume huru itayounda na watu huru...
Hii ndio njia pekee iliyobakia kwa sasa hadi 28 October.
Tarehe nyingine ya uchaguzi inaweza kupangwa (kama itakavuo amuliwa na mahakama) ili kurekebisha dosari zote za uchaguzi kurekebishwa...
Hamuwezi kuendelea na ushaguzi huu ili hali ubaguzi wa haki zenu za msingio ziko wazi... referee wenu- NEC- hana uwe3zo tena wa kusimamia zoezi zima la uchaguzi utao kuwa free an fair maana tayari amekwisha onesha uwezo wake - hana uwezo huo kwa kuusimamia
Ni ushauri tu na maoni yangu binafsi... si lazima mmchukue... msipotaka hivyo, hakuna njia ya kuyahoji matokeo wala ukiukwaj wa taratibu maana mtakuwa mmekubaliana na yote NEC iliyowafanyia...