Tusiendekeze Ngono. Tendo la ndoa liwe kwa makusudi ya uumbaji tu

Tusiendekeze Ngono. Tendo la ndoa liwe kwa makusudi ya uumbaji tu

Page 94

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
5,204
Reaction score
15,207
Wasalaam Wakuu.

Katika dunia ya sasa, ngono imekuwa ni kibwagizo katika maisha ya binadamu.

Iwe jinsia ke au me, wote wanapenda kufanya ngono kuliko inavyostahili.

Kufanya mapenzi ni tendo takatifu kwa ajili ya kufanya uumbaji. Yaani kwa ajili ya kuendeleza kizazi. Lakini binadamu wameigeuza kama Starehe.

Tukitazama kwa Wanyama wengine wafugwao na wa mwituni, hufanya mapenzi kwa nia pekee ya kurutubisha na kutungisha mimba. Ikishatimia hawafanyi tena mpaka pale watakapokuwa tayari kupata uzao mwingine.

Kutokana na binadamu kuendekeza ngono kama Starehe, imeleta athari kubwa sana katika uso wa dunia.

Hata jinsia fanano zimeanza kuingiliana kwa sababu ya kupenda starehe. Wanaume kwa wanaume wanageuzana kwa nia tu ya kugundua raha katika kufanya hivyo. Vivyo hivyo kwa wanawake. Kama tungelitumia kwa minajili ya kuendeleza kizazi basi mapenzi ya jinsia moja kamwe yasingelikuwepo abadani.

Kuendekeza ngono kumeleta magonjwa mengi sana katika uso wa dunia. UKIMWI, homa ya ini, kaswende na magonjwa mengi ya kuambukiza ni matokeo ya Starehe ya ngono. Kama ngono isingelidekezwa basi kusingelikuwepo na idadi kubwa ya magonjwa ya zinaa.

Kuendekeza ngono kumeondoa uaminifu, urafiki na undugu. Kama mmoja wa wanandoa ameendekeza ngono na mwenzake kutambua basi mfarakano hutokea baina yao. Uaminifu uliokuwepo hupotea. Undugu huvunjika. Urafiki hufifia. Yote haya ni kwa sababu wahusika wameendekeza Starehe ya ngono.

Kuendekeza ngono kumezalisha sana watoto wa mitaani. Hamu ziliwazidi, wakakutana kutimiziana. Mimba ikafungwa. Hawakujiandaa kumpokea mgeni. Kitakachotokea ni mtoto kukimbiwa na kuanza maisha yake mwenyewe.

Kuendekeza ngono kumepelekea vifo, ulemavu na umaskini. Watu wengi wamejinyonga kwa sababu kushindwa kuhimili ukweli wa walichotendewa. Wengine wamebaka na kuuwa kwa sababu ya mafumanizi. Ngono hugharimu pesa na muda ambao ungetumika kwa ajili ya uzalishaji mali na hivyo umaskini.

Ngono ni kiini cha maovu yote katika uso wa dunia. Tukae mbali nayo.

Kuna jamii moja ambayo, hufanya mapenzi pale tu ambapo wana nia ya kupata mtoto. Pale ambapo baba na mama wataona kwamba mtoto sasa ameshakua, basi mama ataambiwa aache kunyonyesha mtoto. Watafanya kwa wakati kisha mwanamke akishabeba ujauzito, wanahairisha mpaka pale ambapo watakuwa tayari tena kutafuta mtoto mwingine.

Hata wanandoa, msiendekeze sana tendo la ndoa. Lifanyike kwa kiasi.
 
Mkuu acha watu wafurahie kazi ya Muumba. Unadhani kama Mungu angetaka tendo hilo liwe la kuzaliana tu kama ilivyo kwa wanyama angeshindwa kufanya hivyo? Unadhani kwanini baada ya hedhi kuna siku zinazoitwa safe days?
Usimuingilie Mungu Mkuu.
 
My take is, you are correct Mkuu. Sasa hivi mitandao ya kijamii na media zimesexualize karibu kila kitu, kupelekea watu kuwaza sex muda wote. Mfano, jana nilikuwa safarini, kwenye bus wakaweka nyimbo za Bongo Fleva, aisee videos ni uchiuchi tu, yaani unajikuta unawazimia wale vixxen, unaishia tu kuwatamani.

Tukienda social media, hapa ndiyo tatizo kubwa, kuna magroup ya ukahaba Whatsapp, ukiingia instagram kuna models wapo topless tu (hawa ni wa ughaibuni) tukija kibongobongo, unakuta Dada zetu na Mama zetu wadogo wanapiga picha na kuonyesha makalio. Au wanachagua angel ambayo itaonyesha shepu vizuri.

Hii kitu ina madhara makubwa sana. Kuna forum moja ya Marekani, watu walikuwa wanaweka muda wa kuquit social media kabisa, kutokana na kuyaona madhara ya social media. Watu wanaquit au wanapunguza kabisa social media kwa sababu ya oversexualization.

Hebu fikiria wadogo zetu, wanavyoziimba nyimbo za Bongo fleva, ina maana hawa watoto wanaangalia content ambazo kwa age yao hawakutakiwa kuangalia kabisa.

Hapo zamani mwanamke aliweza kufika miaka 25 akiwa na bikira yake, lakini juzi nimekutana na case mtoto wa form two ametoa mimba. Just think mtu amefikia age ya mihemko, na haya yanayoendelea kwenye media, mtoto anatamani ajaribu kila anachokisikia kwenye nyimbo. Just think...

Hii dunia inaendeshwa na watu wachache na wametugeuza puppets kwa faida zao wenyewe. Kuanzia mavazi, tabia, vyakula, mpaka mapenzi na ngono, almost kila kitu, kuna watu wanakupangia.
 
Sijakufanya mjinga Mkuu. Niambie ni wanyama gani hufanya mapenzi kama Starehe?
Dolphin (pomboo) ,nguruwe (pig) na bonobos (jamii fulani ya sokwe).

Mkuu fanya kwanza utafiti ndiyo uje na nyuzi kama hizi , isijekuwa hau perfom (no offence) ndo u nakuja kutaka kuaminisha watu hapa yale unayoona ni sawa.

Nikuulize swali vipi kama mwanamke akifikia menopause(40-50 years) je? Haitakiwi kufanya naye sex tena? Je? Huwa hamu yake inakwisha? Na je? Kwa sisi wanaume huwa hamu pia inakwisha kwenye umri huo?

👆 hapo ndipo utakapogundua ulikurupuka .

N.b
Binadamu si mnyama.
 
Back
Top Bottom