Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Ili watoto wadogo wa shule za msingi na wenzao wa Sekondari waweze kusoma kwa ufanisi ni lazima wawe wameshiba vizuri. Mwanafunzi anayesoma akiwa na njaa hawezi kuelewa chochote na zaidi sana ataona shule ni sehemu ya mateso.
Chakula bora kwa wakati katika hatua za awali za ukuaji wa mtoto ni muhimu sana hata katika maendeleo ya afya ya akili na mwili.Hili ni jambo lisilopaswa kupuuzwa kama tunataka taifa lenye watu wenye vichwa na miili inayofanya kazi vizuri.
Pia ukosefu wa chakula shuleni ni chanzo kikubwa cha utoro kwa wanafunzi wengi. Ni jambo la kusababusha udumavu na kuwageuza watoto wengine omba omba kwa wenzao.
Serikali ije na mpango wa kutoa chakula bora kwa shule zote za kutwa au kama haiwezi wanafunzi wote wa kuanzia chekechea mpaka darasa la nne wamalize masomo yao saa nne huku wale wengine wote waliobaki wamalize masomo yao saa saba mchana wakajihangaikie wenyewe chakula.
Chakula bora kwa wakati katika hatua za awali za ukuaji wa mtoto ni muhimu sana hata katika maendeleo ya afya ya akili na mwili.Hili ni jambo lisilopaswa kupuuzwa kama tunataka taifa lenye watu wenye vichwa na miili inayofanya kazi vizuri.
Pia ukosefu wa chakula shuleni ni chanzo kikubwa cha utoro kwa wanafunzi wengi. Ni jambo la kusababusha udumavu na kuwageuza watoto wengine omba omba kwa wenzao.
Serikali ije na mpango wa kutoa chakula bora kwa shule zote za kutwa au kama haiwezi wanafunzi wote wa kuanzia chekechea mpaka darasa la nne wamalize masomo yao saa nne huku wale wengine wote waliobaki wamalize masomo yao saa saba mchana wakajihangaikie wenyewe chakula.