Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 1,117
- 3,153
TUSIINGIZE UDINI, SUALA LA BANDARI NI URITHI WA WATANZANIA
Watu wanakuja na hoja za Uarabu, Uislamu na Ukristo hizi ni hoja binafsi na sisi Watanzania hatuna hizi kasumba za udini wala ukabila, ni vijihoja vinavyotaka kututoa kwenye reli tuache kudai mkataba wenye tija kwa Watanzania, hizi hoja zenu za udini tunazikemea, ni hoja binafsi sio za Watanzania na hazina mashiko katika suala la uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam, pelekeni hoja zenu za udini kwenye mabaraza ya dini mkakubaliane na Serikali,kwa sasa tupo kwenye suala la bandari, tunataka mkataba wenye tija kwa Watanzania, sio mkataba wa kuwauza Watanzania kama ule wa Chifu Mangungo wa Msovelo.
Kuna watu wanataka kuhalalisha kosa kwa kosa, hili nalo hapana, kama mikataba ya nyuma haijapita bungeni na huu Mungu katujalia umepita bungeni, na Watanzania tumeuona sijui umevuja au umeachiwa watu wausome na tumegundua makosa makubwa ya kutweza utu wa Mtanzania, ndio tuuachie uendelee hivyo hivyo kwa kuwa mikataba mingine uko nyuma haikupita bungeni, hili si sahihi, tulichokigundua kibovu lazima kirekebishwe na kiwekwe kwa maslahi mapana ya Watanzania.
#Maslahi ya Mtanzania kwanza.
Watu wanakuja na hoja za Uarabu, Uislamu na Ukristo hizi ni hoja binafsi na sisi Watanzania hatuna hizi kasumba za udini wala ukabila, ni vijihoja vinavyotaka kututoa kwenye reli tuache kudai mkataba wenye tija kwa Watanzania, hizi hoja zenu za udini tunazikemea, ni hoja binafsi sio za Watanzania na hazina mashiko katika suala la uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam, pelekeni hoja zenu za udini kwenye mabaraza ya dini mkakubaliane na Serikali,kwa sasa tupo kwenye suala la bandari, tunataka mkataba wenye tija kwa Watanzania, sio mkataba wa kuwauza Watanzania kama ule wa Chifu Mangungo wa Msovelo.
Kuna watu wanataka kuhalalisha kosa kwa kosa, hili nalo hapana, kama mikataba ya nyuma haijapita bungeni na huu Mungu katujalia umepita bungeni, na Watanzania tumeuona sijui umevuja au umeachiwa watu wausome na tumegundua makosa makubwa ya kutweza utu wa Mtanzania, ndio tuuachie uendelee hivyo hivyo kwa kuwa mikataba mingine uko nyuma haikupita bungeni, hili si sahihi, tulichokigundua kibovu lazima kirekebishwe na kiwekwe kwa maslahi mapana ya Watanzania.
#Maslahi ya Mtanzania kwanza.