Tusio na magari tukutane hapa

Huu ndio ukweli mchungu sana ambao watu wengi wenye magari hawapendi kuusema na hawatausema mbele ya watu wasiokuwa na magari.

1/Kununua gari kumewapelekea kwenye madeni kutoka kwenye taasisi za kipesa. Walikuwa hawajawahi kukopa benki lakini kupitia gari walikopa. Na mikopo hiyo ni ya muda mrefu na yenye riba.

2/Gari limepelekea utumwa wa matumizi ya Pesa ili kulihudumia hilo gari au kwenda sambamba na maisha ya kumiliki gari. Gharama za maisha kwao zimekuwa juu wakati huo huo kipato chao ni kile kile au kimepungua.

3/Furaha na Amani ya kumiliki gari ni kidogo sana tofauti kabisa na mategemeo na matazamio yao kabla ya kumiliki hilo gari au mapema wakati ndio wameanza kulimiliki. Kiufupi gari limeleta karaha pia katika maisha yao.

4/Wengi wanajuta kimoyomoyo kuhusu maamuzi ya kununua gari wakati walipaswa kufanya baadhi ya mambo mengine kwanza au aina ya gari walioamua kuimiliki haikuwa sahihi kwao.

5/Kumiliki kwao gari hakukuwafanya kujisikia kupata utoshelevu bali kumeongeza uhitaji wa kutaka kumiliki gari tofauti na hilo au kumeleta unyonge fulani mbele ya watu wengine wenye magari mazuri na bora zaidi yao.
 
Mkuu Acha kupiga ikulu basi
 
Umetoa ukweli tupu!

Lakini wenye magari licha ya kukutwa na hizi kadhia, wanaenjoy sana maisha tofauti na sisi tusonayo
 
Napendaga sana daladala , nikiwa nimepanda nipo nyuma mdada mwenye chur* awe mbele yangu alafu tubanane huwa nataman safari iendelea kutwa nzima
Hii ID yako maana yake ndio hii nayoiujua mimi au
[HASHTAG]#Vupua[/HASHTAG]
 
We jamaa Sijui umewaza nini..but usijali utapataa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…