Tusipende kuwahukumu watu tuwanao wamefanikiwa kama hatujui kwa nini wako hivyo kwa ndugu au jamaa zao

Tusipende kuwahukumu watu tuwanao wamefanikiwa kama hatujui kwa nini wako hivyo kwa ndugu au jamaa zao

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
TUSIPENDE KUWAHUKUMU WATU TUWANAO WAMEFANIKIWA KAMA HATUJUI KWA NINI WAKO HIVYO KWA NDUGU AU JAMAA ZAO

Wapo watu tunawatazama wamefanikiwa sana katika maisha yao ila ndugu zake wako nyuma sana kimaisha ukamhukumu katika ubaya tu

Yawezekana hata hao wanaolalamika juu ya huyo mtu hata hapo walipofika ni kwa mkono wa huyo mnayemuona hawawasaidii kitu ila kwakuwa hawezi kuyasema mabaya ya ndugu zake amekubali kusemwa vibaya na kutojibu ili kulinda utu wao ndugu zake na aibu ya familia

Yawezekana amewasaidia sana, amejitoa sana kwa hao watu, amefanya mengi mno ila hapewi thamani, hawazalishi wanachopewa wanakula chote na kuomba tena. Walingeuza msaada kuwa haki yao na waipate kwa wakati na kwa kiwango wanachokitaka bila kujali naye kuwa ana majukumu yake, anahitaji kusogea mbali zaidi kwenye matamanio ya familia aliyonayo

Yawezekana mtu huyo alipooa au kuolewa tu aliacha baadhi ya majukumu, au alipambana akawafikisha mahala fulani ila kwa kuendekeza starehe wakafeli shule au kwenye eneo fulani la maisha linalowapelekea waonekane ni watu wanahitaji msaada chanzo ni wao si yeye huyo. Acheni kumhukumu huyo mtu kama hamuijui sababu ya kwa nini hafanyi hivyo, hana uwezo wa kujibu mashambulizi kaamua tu kaa kimya

Kwahiyo, msiwahukumu watu waliofanikiwa kwa aina ya maisha ya ndugu au jamaa zake wanayoyaishi mkahisi anapenda wawe hivyo ila alishafanya sana au alishafanya kwa nafasi yake kwahiyo jukumu lililobaki ni lao si lake.
1731252043967.jpg
 
TUSIPENDE KUWAHUKUMU WATU TUWANAO WAMEFANIKIWA KAMA HATUJUI KWA NINI WAKO HIVYO KWA NDUGU AU JAMAA ZAO

Wapo watu tunawatazama wamefanikiwa sana katika maisha yao ila ndugu zake wako nyuma sana kimaisha ukamhukumu katika ubaya tu

Yawezekana hata hao wanaolalamika juu ya huyo mtu hata hapo walipofika ni kwa mkono wa huyo mnayemuona hawawasaidii kitu ila kwakuwa hawezi kuyasema mabaya ya ndugu zake amekubali kusemwa vibaya na kutojibu ili kulinda utu wao ndugu zake na aibu ya familia

Yawezekana amewasaidia sana, amejitoa sana kwa hao watu, amefanya mengi mno ila hapewi thamani, hawazalishi wanachopewa wanakula chote na kuomba tena. Walingeuza msaada kuwa haki yao na waipate kwa wakati na kwa kiwango wanachokitaka bila kujali naye kuwa ana majukumu yake, anahitaji kusogea mbali zaidi kwenye matamanio ya familia aliyonayo

Yawezekana mtu huyo alipooa au kuolewa tu aliacha baadhi ya majukumu, au alipambana akawafikisha mahala fulani ila kwa kuendekeza starehe wakafeli shule au kwenye eneo fulani la maisha linalowapelekea waonekane ni watu wanahitaji msaada chanzo ni wao si yeye huyo. Acheni kumhukumu huyo mtu kama hamuijui sababu ya kwa nini hafanyi hivyo, hana uwezo wa kujibu mashambulizi kaamua tu kaa kimya

Kwahiyo, msiwahukumu watu waliofanikiwa kwa aina ya maisha ya ndugu au jamaa zake wanayoyaishi mkahisi anapenda wawe hivyo ila alishafanya sana au alishafanya kwa nafasi yake kwahiyo jukumu lililobaki ni lao si lake.View attachment 3148773
Kwa sasa Mimi ni Muhanga wa jambo hili ulilo andika. Ni kweli ukiwasaidia Ndugu zako wapo watakao chomoka na kufanikiwa Ila wapo pia watakao kuwa tegemezi. Mmoja ni mdogo Wangu - yeye kila ukimpa mtaji baada ya wiki 1 utasikia mtaji umekata.
Unakaa wiki tatu, unamuonea huruma baada ya kusikia kwamba anatafuta pesa ya majini, unaamwambia achana na ujinga huo, nitakupa mtaji - Nipe mchangunuo wa biashara unayotaka kuifanya. Akisikia tu neno mchanganuo- anasema hayo ni mateso, ya nini umpe masharti wakati ni msaada?
Sasa nimemwacha apigike hadi ajitambue Ila maneno ni mengi kwamba simsaidii… nimemshit Kwa kweli- amekuwa shukrani ya punda -
Kala zaidi ya mil 20 zangu kimasihara. Nimeamuka Kwa sasa.
Amekuwa ni bingwa wa kutunga vijistori vya kuonewa huruma na kuishi maisha yaliyo juu ya uwezo wake.
Ngoja kiumane akili za maisha zimrudie ili ajue kwamba ile methali ya mali bila daftari ni ya kweli.
 
Kwa sasa Mimi ni Muhanga wa jambo hili ulilo andika. Ni kweli ukiwasaidia Ndugu zako wapo watakao chomoka na kufanikiwa Ila wapo pia watakao kuwa tegemezi. Mmoja ni mdogo Wangu - yeye kila ukimpa mtaji baada ya wiki 1 utasikia mtaji umekata.
Unakaa wiki tatu, unamuonea huruma baada ya kusikia kwamba anatafuta pesa ya majini, unaamwambia achana na ujinga huo, nitakupa mtaji - Nipe mchangunuo wa biashara unayotaka kuifanya. Akisikia tu neno mchanganuo- anasema hayo ni mateso, ya nini umpe masharti wakati ni msaada?
Sasa nimemwacha apigike hadi ajitambue Ila maneno ni mengi kwamba simsaidii… nimemshit Kwa kweli- amekuwa shukrani ya punda -
Kala zaidi ya mil 20 zangu kimasihara. Nimeamuka Kwa sasa.
Amekuwa ni bingwa wa kutunga vijistori vya kuonewa huruma na kuishi maisha yaliyo juu ya uwezo wake.
Ngoja kiumane akili za maisha zimrudie ili ajue kwamba ile methali ya mali bila daftari ni ya kweli.
Haya mambo acha kaka
Pesa nilizoteketeza Kwa ndugu ningekuwa nimejenga ghorofa la maana hapa town. Wengine nimewajengea nyumba

Kwa sasa ninayoyashuhudia kutoka kwao, imenilazimu nifungamane na wadogo zangu wa tumbo la mama yangu pekee. Hao wengine ni takataka
 
All in all tupambane tuu..
Kumsaidia mtu sio kumpa pesa ila mtafutie connection basi yaishe
 
Ulichoongea ni kweli, usipoujua ukweli bora ukae kimya. Na hawa hawa ndio wa kwanza kukwambia ulikuwa na kazi nzuri lakini ulichezea hela na huna maendeleo. Ndugu ni wabaya sana kiukweli
 
Usimpe mtu hela ya bure kwa kisingizio cha ndugu. Mtaji unaongezwa palipo na mtaji. Na mpe mtu ulipo uwezo wake wa kufikiri. Mfumo ulioumba hii dunia ukitaka kufanikiwa ni lazima sadaka itoke. Kama haupo tayari jiandae kulaumu watu. Lazima kuna pa kujinyima, kujituma, kunyenyekea, kujifunza, kutiii, kutoa shukrani, kwa suala la ndugu wengi wanahtaji msaada wa kusikilizwa zaid na kushauriwa sio fedha. Maana kila binadamu ameshawekea mtaji wake tayari na aliyemuumba. Unatakiwa tu kuupiga jeki. Ikishindikana kuwa na kiasi maana huwez kuwa na huruma kumpita Mungu. Mpaka amemuumba anamuwazia kuliko wewe. Kwa sisi wakristo tumefanikiwa kupata mfano bora zaidi. Kwa uovu wetu ilibidi Yesu aje ili ile adhabu tulitakiwa kuipata aipate yeye. Awe daraja letu kufikia kule tulipotengwa kwa uchafu wetu. So lazima kila mafanikio pawepo na sadaka kwanza. Unatakuwa mchezaji mzuri fanya mazoezi yanauma ila ndio sadaka yenyewe. Unataka kufika Mbinguni acha dhambi ndio sadaka yenyewe. Nk nk nk.
 
Back
Top Bottom