Tusker Challenge Cup Updates

Naona hali si nzuri kwa Prison ambao ni wawakilishi wa Mashindano ya kimataifa[Kombe la shirikisho] mwakani. Ingekuwa inawezekana ni bora wasinge eenda tu inaonyesha maandalizi ni F.Ngoja tusubili mpira unadunda.
 
Walau hiyo ni dalili njema kwa timu yetu Simba jamani...yaaani ile duru ya kwanza inaisha tuko nafasi ya 6 iliumiza sana, migogoro isiyokwisha, mara fukuza kocha..nadhani tukianza hivi huenda hata hili kombe likarudi Msimbazi...Simba mbele kwa mbele kazeni buti
 
Ila hii si dalili njema sana kwa Prisons ambayo mwakani tu mapema watashiriki kombe la washindi..Nadhani wanahitaji mkakati mkubwa zaidi wa ushindi katika medani ya mechi za kimataifa.
 
Mimi naiona Prisons kama timu ambayo sio nzuri sana, ila wana faida kwamba wengi wa wachezaji wao wanakua wamekaa pamoja muda mrefu.
Sidhani kama watafanya lolote la maana kombe la shirikisho.
Nadhani ni timu isiyo na mawazo mapya, imeganda.
Sorry, just letting things slip out of the white thing in my head I call a brain.
 
Roya Roy mi naungana na mawazo yako.... Hivi jamani hawezekani wakajitoa tu kwenye hayo mashindano mwakani, naona aibu tupu... juzi juzi nilisoma kwenye gazeti moja eti wanamuomba kocha mkuu wa Yanga awe mshauri wao kwenye mashindano mwakani mmh yangu macho......
 

wadau ,pambano la yanga na mtibwa vp?
 
wadau ,pambano la yanga na mtibwa vp?

Mtibwa 1 Yanga 0
Timu zote zina point 3 , zimefunga/fungwa goli 1.
Inabidi kupigwa kura kupata washindi 2 kesho (according to Kaijage)
 
Mtibwa 1 Yanga 0
Timu zote zina point 3 , zimefunga/fungwa goli 1.
Inabidi kupigwa kura kupata washindi 2 kesho (according to Kaijage)

aise kura! Mkuu Roya Roy huyo Kaijage ametaja wapiga kura ni kina nani?
 
Alisema kitu kama baada ya mechi ya kesho kuna kikao (nadhani cha kamati ya mashindano)....ila sidhani kama itakua ni voting, rather yaweza kuwa kitu kama draw flani (just guess work)
 
Mtibwa yaibana Yanga Tusker Cup, kusubiri shilingi
Habari toka : NIFAHAMISHE Tanzania news portal

Kesho asubuhi nifahamishe itawapa full details za kura hizo
 
...watamchuna ngozi?


Na ukizingatia kwamba leo wamecholewa kwenye mashindano haya......
  1. URA
  2. Mtibwa
  3. Dar 'Young' Africans (au kama Masatu alivyowaita hapo juu)
Hapa ilikua ni kuchagua vikaratasi.
 
Kanda2 mdebwedo!

Watu wa Simba tumewazoea. Zogo ndiyo fani yenu daima. Fujo tu, Yanga akiharibu. Mnafurahia nini hapo nyie? Hizo kura kwa mna yoyote ile haziwezi iangusha Yanga. Piga ua. Tumo. Ole wenu tukutane. Yule mzee wa Magomeni mtammaliza bure........
 
Yanga kazi wanayo hata wakifata alphabeti
Mtibwa
Ura
Yanga
 
Yanga kazi wanayo hata wakifata alphabeti
Mtibwa
Ura
Yanga

Tumeshapigwa chini tayari! Kura za kihuni za kwenye bahasha, Yanga tumeokata iliyoandikwa OUT! Kila la kheri watani wetu. Ndipo pa kumalizia hasira hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…