Tutaje tozo ambazo zimependekezwa kwenye msaada wa bajeti ambazo zinaweza leta maumivu Ili zirekebishwe kabla ya vilio kusikika kuanzia July 1

Tutaje tozo ambazo zimependekezwa kwenye msaada wa bajeti ambazo zinaweza leta maumivu Ili zirekebishwe kabla ya vilio kusikika kuanzia July 1

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2022
Posts
9,436
Reaction score
10,944
Serikali imetoa mapendekezo ya Bajeti yake Kwa mwaka 2024/25 yenye zaidi ya Shilingi Trilioni 49.3 na kuainisha vyanzo vya pesa hiyo na matumizi yake.

Ni vyema Sasa Wananchi na wadau tujikite kutoa maoni ambayo yatasaidia mjadala wa Bajeti Ili kama Kuna tozo unaona haiko sawa uibainishe na njia Mbadala.

Binafsi Kwa sehemu kubwa Bajeti ya Serikali nimeona Iko vizuri isipokuwa kasoro ndogo ndogo.

Mojawapo ya tozo iliyopendekezwa na ambayo haijabainishwa wazi jinsi gani itatozwa na watatozwa kina nani ni hii inaitwa tozo ya miundombinu (infrastructure levy).Waziri anasema itaingia mfuko wa Dharura Ili kupata hela za ku deal na majanga lakini haijabainishwa wazi kama itatozwa kwenye Mafuta,au Kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri au Kwa utaratibu gani.

Wakati wa mjadala ni vyema ielezwe itakuwa kiasi gani na watakaotozwa ni kina nani.

Aidha account hiyo in case pesa haijatumika usalama wa pesa hizo itakuaje? Na nani watakuwa na amri ya kutoa hizo hela? Na Je tunaweza kufahamishwa ni kiasi gani kinatarajiwa kupatikana?

Kimsingi maswali ni mengi maana isijekuwa ni account ya kupigia pesa zetu Kwa sababu Nchi hii Viongozi Kwa sehemu kubwa hawaaminiki.

Naomba kutoa hoja 👇👇

Screenshot 2024-06-14 082635.jpg
 
Serikali imetoa mapendekezo ya Bajeti yake Kwa mwaka 2024/25 yenye zaidi ya Shilingi Trilioni 49.3 na kuainisha vyanzo vya pesa hiyo na matumizi yake.

Ni vyema Sasa Wananchi na wadau tujikite kutoa maoni ambayo yatasaidia mjadala wa Bajeti Ili kama Kuna tozo unaona haiko sawa uibainishe na njia Mbadala.

Binafsi Kwa sehemu kubwa Bajeti ya Serikali nimeona Iko vizuri isipokuwa kasoro ndogo ndogo.

Mojawapo ya tozo iliyopendekezwa na ambayo haijabainishwa wazi jinsi gani itatozwa na watatozwa kina nani ni hii inaitwa tozo ya miundombinu (infrastructure levy).Waziri anasema itaingia mfuko wa Dharura Ili kupata hela za ku deal na majanga lakini haijabainishwa wazi kama itatozwa kwenye Mafuta,au Kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri au Kwa utaratibu gani.

Wakati wa mjadala ni vyema ielezwe itakuwa kiasi gani na watakaotozwa ni kina nani.

Aidha account hiyo in case pesa haijatumika usalama wa pesa hizo itakuaje? Na nani watakuwa na amri ya kutoa hizo hela? Na Je tunaweza kufahamishwa ni kiasi gani kinatarajiwa kupatikana?

Kimsingi maswali ni mengi maana isijekuwa ni account ya kupigia pesa zetu Kwa sababu Nchi hii Viongozi Kwa sehemu kubwa hawaaminiki.

Naomba kutoa hoja 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C8KS5f4oToZ/?igsh=MTJ5cG1uemJ6ZXN2aw==

Tuliachie Bunge la kina msukuma na kibajaj watajadili usituchoshe akili zetu
 
Tozo yoyote anatozwa mtumiaji wa mwisho, hao wengine ni madalali wa kuikusanyia serikali tu
Sasa wakisema wanaweka kwenye Kila gari kuanzia mmiliki binafsi Hadi wa biashara hapo si unaona hata wewe itakuhusu huwezi ku pass over kama wafanyabiashara?
 
Ww piga kelele na hayo unayoona ni kasoro, lakini kutoa maoni eti yajadiliwe kwenye hilo bunge kibogoyo la majizi ya kura ni kupoteza muda.
Bunge kibogoyo ndio Bunge gani? Mbona Bunge linajadili na Serikali inatekeleza?

Pili hata humu jf maoni yatasikika,wewe taja kasoro na utoe njia Mbadala
 
Kuna tozo ya kwenye gas asilia hasa kwenye magari yanayowekewa gas na hii itarudisha nyuma jutihada za watu kutumia gas kwenye magari
Hii mimi naona wamefanya makusudi kukwamisha, wafanya biashara wa mafuta wapo nyuma ya mpango huu.
 
Hii mimi naona wamefanya makusudi kukwamisha, wafanya biashara wa mafuta wapo nyuma ya mpango huu.
Mimi naona hiyo wako sawa Kwa sababu wamesema inalenga kuleta usawa kati ya wanaotumia Mafuta na gesi.

Hata hivyo bei ya gesi Iko chini sana hata wakiongeza hiyo 380 haitafika 2,000 kwa Lita .

Mwisho wamesema ni hela ya mfukonwa Barabara.
 
Kuongeza Kodi kwenye mafuta ya kula kutoka nje wakati capacity ya viwanda vya ndani ni ndogo!!!
Hapo wako sawa Kwa sababu wakulima wa Mikoa inayolima alizeti wamelalmika kukosa soko na bei kupromoka Toka mwaka Jana ambapo Waziri wa Kilimo alisema.

Pia wamesema wataagiza kile tuu ambacho kitaonekana ni pungufu yaani quorta badala ya kuwa na uhuru wa Moja kwa Moja.
 
Back
Top Bottom