Mwaka 2015 mara baada ya Mh. Rais kuapishwa, kila mwezi takwimu zenye kuvunja rekodi kuhusu makusanyo ya kodi zilikuwa zikitangazwa na watu wakiweka vifua mbele kwamba nchi yetu inaelekea kuwa donor country.
Muda ulivyozidi kwenda, tulishuhudia sekta mbalimbali zikisinyaa. Biashara za kati zilitoweka na Waziri wa Fedha wa wakati huo alikiri biashara kufungwa.
Taasisi na Jumuiya za Kimataifa zikajikuta zinalumbana na Serikali kwenye takwimu. Wizara ya Fedha ilikuwa ikitoa taarifa zenye kuonyesha uchumi unakuwa kwa kasi wakati Taasisi za Kimataifa zikionyesha kwa wakati fulani, uchumi ule ulikuwa haufiki hata asilimia 5%. Ikapita miswada ya kuzuia machapisho mbalimbali na asasi za kiraia zikafungwa midomo.
Hilo likiendelea, serikali ikazidi kujinadi kwenye usafiri wa anga kwamba inatengeneza faida kumbe hali ni tofauti. Kwenya huduma za Afya tukaambiwa Serikali tukaambiwa ilitenga fedha zaidi ya bil. 200 kwa ajili ya dawa mwaka, kumbe haikupeleka hata senti. Mapambio yakaendelea kufurahisha Watanzania.
Wakati watu wakistaajabu hayo, ukafika uchaguzi ambao haukuwa na hamasa na aliyekuwa Mh. Rais alipiga kampeni chache lakini yeye na Wabunge wake walishinda kwa kishindo. Itakumbukwa waliokuwa wasimamizi wa Uchaguzi walionywa, kama umepewa hiyo nafasi na mimi, ole wako ashinde mwingine.
Wale waliochagua upinzani miaka ya nyuma walitahadharishwa, wakichagua upinzani, maendeleo ni ndoto.
Ajira kwa vijana, hali ikawa mbaya zaidi. Watunga sheria na sera, waliwahimiza vijana kujiajiri lakini hawakuandaa mazingira ya kujiajiri.
Pamoja na haya, hofu ikatanda. Mitandao ikazimwa. Kukosoa kukakoma maana matokeo yalikuwa wazi. Mapato hayakutangazwa tena. Watu mitaani walinong'ona hali ilivyo. Wafanyabiashara wakubwa wakakodi vijana wawauzie mali zao maana maduka hayakuwa na maana tena.
Pamoja na hayo, JPM alikuwa Mzalendo wa aina yake.
Muda ulivyozidi kwenda, tulishuhudia sekta mbalimbali zikisinyaa. Biashara za kati zilitoweka na Waziri wa Fedha wa wakati huo alikiri biashara kufungwa.
Taasisi na Jumuiya za Kimataifa zikajikuta zinalumbana na Serikali kwenye takwimu. Wizara ya Fedha ilikuwa ikitoa taarifa zenye kuonyesha uchumi unakuwa kwa kasi wakati Taasisi za Kimataifa zikionyesha kwa wakati fulani, uchumi ule ulikuwa haufiki hata asilimia 5%. Ikapita miswada ya kuzuia machapisho mbalimbali na asasi za kiraia zikafungwa midomo.
Hilo likiendelea, serikali ikazidi kujinadi kwenye usafiri wa anga kwamba inatengeneza faida kumbe hali ni tofauti. Kwenya huduma za Afya tukaambiwa Serikali tukaambiwa ilitenga fedha zaidi ya bil. 200 kwa ajili ya dawa mwaka, kumbe haikupeleka hata senti. Mapambio yakaendelea kufurahisha Watanzania.
Wakati watu wakistaajabu hayo, ukafika uchaguzi ambao haukuwa na hamasa na aliyekuwa Mh. Rais alipiga kampeni chache lakini yeye na Wabunge wake walishinda kwa kishindo. Itakumbukwa waliokuwa wasimamizi wa Uchaguzi walionywa, kama umepewa hiyo nafasi na mimi, ole wako ashinde mwingine.
Wale waliochagua upinzani miaka ya nyuma walitahadharishwa, wakichagua upinzani, maendeleo ni ndoto.
Ajira kwa vijana, hali ikawa mbaya zaidi. Watunga sheria na sera, waliwahimiza vijana kujiajiri lakini hawakuandaa mazingira ya kujiajiri.
Pamoja na haya, hofu ikatanda. Mitandao ikazimwa. Kukosoa kukakoma maana matokeo yalikuwa wazi. Mapato hayakutangazwa tena. Watu mitaani walinong'ona hali ilivyo. Wafanyabiashara wakubwa wakakodi vijana wawauzie mali zao maana maduka hayakuwa na maana tena.
Pamoja na hayo, JPM alikuwa Mzalendo wa aina yake.