Tutakukumbuka Mzalendo ambaye hukupenda kusikia ukweli na hoja kinzani

Tutakukumbuka Mzalendo ambaye hukupenda kusikia ukweli na hoja kinzani

Watanzania tukafumbia Macho Mengi sana.. ila ilipofikia Hatua akaweka Miradi ambayo Haina hata "Feasibility Study" na Haijulikani "Return Period " ya investments ilofanyika itakuwa miaka Mingapi.. Pengine isingekuwepo kabisaa.. Basi ndipo wadanganyika tukaduwaa..

Mwendazake akaenda mbali zaidi kwa kujaza Yale MAJINGA MASUKUMA ndipo watanzania tukazika rasmi ndoto zetu.

Hatukuwa na Tumaini tena.

Najua kabisa Sote tutakufa lakini Asante Mungu Umemchukua, Malizana nae Huko.
Aiseeeee
 
Ulikuwa ni uzalendo wa aina yake na wa kwake pekee. Maajabu, leo hii watu wote wapo kimya.
Waliosifu wamebaki wakiinamisha vichwa kwa aibu, wengine wakila matapishi yao.
Tujiandae kupokea chanjo ya korona
 
Mwaka 2015 mara baada ya Mh. Rais kuapishwa, kila mwezi takwimu zenye kuvunja rekodi kuhusu makusanyo ya kodi zilikuwa zikitangazwa na watu wakiweka vifua mbele kwamba nchi yetu inaelekea kuwa donor country.

Muda ulivyozidi kwenda, tulishuhudia sekta mbalimbali zikisinyaa. Biashara za kati zilitoweka na Waziri wa Fedha wa wakati huo alikiri biashara kufungwa.

Taasisi na Jumuiya za Kimataifa zikajikuta zinalumbana na Serikali kwenye takwimu. Wizara ya Fedha ilikuwa ikitoa taarifa zenye kuonyesha uchumi unakuwa kwa kasi wakati Taasisi za Kimataifa zikionyesha kwa wakati fulani, uchumi ule ulikuwa haufiki hata asilimia 5%. Ikapita miswada ya kuzuia machapisho mbalimbali na asasi za kiraia zikafungwa midomo.

Hilo likiendelea, serikali ikazidi kujinadi kwenye usafiri wa anga kwamba inatengeneza faida kumbe hali ni tofauti. Kwenya huduma za Afya tukaambiwa Serikali tukaambiwa ilitenga fedha zaidi ya bil. 200 kwa ajili ya dawa mwaka, kumbe haikupeleka hata senti. Mapambio yakaendelea kufurahisha Watanzania.

Wakati watu wakistaajabu hayo, ukafika uchaguzi ambao haukuwa na hamasa na aliyekuwa Mh. Rais alipiga kampeni chache lakini yeye na Wabunge wake walishinda kwa kishindo. Itakumbukwa waliokuwa wasimamizi wa Uchaguzi walionywa, kama umepewa hiyo nafasi na mimi, ole wako ashinde mwingine.

Wale waliochagua upinzani miaka ya nyuma walitahadharishwa, wakichagua upinzani, maendeleo ni ndoto.

Ajira kwa vijana, hali ikawa mbaya zaidi. Watunga sheria na sera, waliwahimiza vijana kujiajiri lakini hawakuandaa mazingira ya kujiajiri.
Pamoja na haya, hofu ikatanda. Mitandao ikazimwa. Kukosoa kukakoma maana matokeo yalikuwa wazi. Mapato hayakutangazwa tena. Watu mitaani walinong'ona hali ilivyo. Wafanyabiashara wakubwa wakakodi vijana wawauzie mali zao maana maduka hayakuwa na maana tena.

Pamoja na hayo, JPM alikuwa Mzalendo wa aina yake.
Dictator Joseph Stalin alikuwa anajiita Koba meaning man of steel. Hawa watu wanapendaga kujiita majina ya kibabe waonekane kama immortal. Na kitu Koba wetu alifanikiwa kabisa kuwafanya wajinga wamuone immortal hakuna aliyeamini amekufa daadeki.

Ilipofika ile aaa kumi na mbili jioni mazishi yalipoisha watu wakaanza kuzagaa kama kuni ndio niliamini yametimia maana hata mie sikuwa naamini. Nilikuwa na joy and fear asije kuinuka mule kwenye jeneza ukasikia murizani nimekufa mabeberu nyie (in Koba's voice) 😃😃😃😃😃

Alale panapomstahili.
 
Mwaka 2015 mara baada ya Mh. Rais kuapishwa, kila mwezi takwimu zenye kuvunja rekodi kuhusu makusanyo ya kodi zilikuwa zikitangazwa na watu wakiweka vifua mbele kwamba nchi yetu inaelekea kuwa donor country.

Muda ulivyozidi kwenda, tulishuhudia sekta mbalimbali zikisinyaa. Biashara za kati zilitoweka na Waziri wa Fedha wa wakati huo alikiri biashara kufungwa.

Taasisi na Jumuiya za Kimataifa zikajikuta zinalumbana na Serikali kwenye takwimu. Wizara ya Fedha ilikuwa ikitoa taarifa zenye kuonyesha uchumi unakuwa kwa kasi wakati Taasisi za Kimataifa zikionyesha kwa wakati fulani, uchumi ule ulikuwa haufiki hata asilimia 5%. Ikapita miswada ya kuzuia machapisho mbalimbali na asasi za kiraia zikafungwa midomo.

Hilo likiendelea, serikali ikazidi kujinadi kwenye usafiri wa anga kwamba inatengeneza faida kumbe hali ni tofauti. Kwenya huduma za Afya tukaambiwa Serikali tukaambiwa ilitenga fedha zaidi ya bil. 200 kwa ajili ya dawa mwaka, kumbe haikupeleka hata senti. Mapambio yakaendelea kufurahisha Watanzania.

Wakati watu wakistaajabu hayo, ukafika uchaguzi ambao haukuwa na hamasa na aliyekuwa Mh. Rais alipiga kampeni chache lakini yeye na Wabunge wake walishinda kwa kishindo. Itakumbukwa waliokuwa wasimamizi wa Uchaguzi walionywa, kama umepewa hiyo nafasi na mimi, ole wako ashinde mwingine.

Wale waliochagua upinzani miaka ya nyuma walitahadharishwa, wakichagua upinzani, maendeleo ni ndoto.

Ajira kwa vijana, hali ikawa mbaya zaidi. Watunga sheria na sera, waliwahimiza vijana kujiajiri lakini hawakuandaa mazingira ya kujiajiri.
Pamoja na haya, hofu ikatanda. Mitandao ikazimwa. Kukosoa kukakoma maana matokeo yalikuwa wazi. Mapato hayakutangazwa tena. Watu mitaani walinong'ona hali ilivyo. Wafanyabiashara wakubwa wakakodi vijana wawauzie mali zao maana maduka hayakuwa na maana tena.

Pamoja na hayo, JPM alikuwa Mzalendo wa aina yake.
Tukimkumbuka magufuli lazima ukweli usemwe huwezi kubadilisha historia ya mtu ulioyaandika ni ukweli mtupu umesahau na benki kuu kamuweka mtu hata hana taaluma ya mambo ya fedha ili amuwendeshe anavyotaka tumshukuru mungu kwa hatua aliyoichukuwa.
 
Dictator Joseph Stalin alikuwa anajiita Koba meaning man of steel. Hawa watu wanapendaga kujiita majina ya kibabe waonekane kama immortal. Na kitu Koba wetu alifanikiwa kabisa kuwafanya wajinga wamuone immortal hakuna aliyeamini amekufa daadeki.

Ilipofika ile aaa kumi na mbili jioni mazishi yalipoisha watu wakaanza kuzagaa kama kuni ndio niliamini yametimia maana hata mie sikuwa naamini. Nilikuwa na joy and fear asije kuinuka mule kwenye jeneza ukasikia murizani nimekufa mabeberu nyie (in Koba's voice) [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]

Alale panapomstahili.
Mkuu umenifanya nicheke kwa sauti kubwa usiku huu[emoji23][emoji23][emoji23]
Daa, jamaa alikuwa anaumiza jamii kwa mgongo wa uzalendo
 
Jamaa alitisha kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 wapinzani nchi nzima walikosea taratibu za uchaguzi km kujaza fomu nk... jamani hata soni hakuwa nayo..... alafu anamaliza kwa kusema "Mniombee"...hakika Mungu yupo akaona isiwe tabu ngoja nikupumzishe.....Pumzika kwa Amani JPM nyuma yako mbele yetu..
 
Back
Top Bottom