Uchaguzi 2020 Tuungane kwa umoja wetu kama Taifa tuikatae CCM, miaka 59 imetosha

Uchaguzi 2020 Tuungane kwa umoja wetu kama Taifa tuikatae CCM, miaka 59 imetosha

Hakuna sababu ya kuendelea kung'ang'ania kitu kisichokuwa na faida 50+ yrs inatosha.
Na hata wakiendelea kuongoza hii nchi miaka elfu ijayo hakuna jipya litakalofanyika la tofauti na hapa uwezo wao ulipoishia.Wakae pembeni wajivue gamba walilokaa nalo toka uhuru labda watapata akili mpya.
 
Ingependeza ungesema ni Operation vunja Jiwe....Au Operation Mwaga Pombe.
Au ungesema ni TAL v. Jiwe, ukisema CCM hapo utaleta uchama. Watu wengi wanapigia chama kuliko mtu.
 
Mabadiliko ni muhimu.Lazima kuje akili mpya ili ifanye mabadiliko ya hali na mifumo iliyokwisha haribika.Haijalishi itatumika muda gani kulingana na aina ya maboresho yanayohitajika na waliopo wameshakaa vyakutosha na uwezo umeshaisha.Lakini pia lazima ijulikane kua yoyote anaweza kuongoza kwahiyo ukipewa nafasi ukazingua unakaa pembeni anakuja mwingine.
Kuna wajinga wanafikiri wapinzani wana magic button watakayoibonyeza halafu hizo ndoto za maendeleo zitimie overnight.

Wewe chagua tu unayejisikia kumchagua hayo unayoyaota hakuna guarantee yakuisha au kufanyiwa kazi.

Liberia, Nigeria,DRC na Malawi walikochagua upinzani kuna jipya gani so far?

Wanaijeria bado wanafia Mediterranean Sea wakienda Ulaya,Boko Haram bado ipo, Liberia imeshuhudia internet ikizimwa kwa mara ya kwanza chini ya George Weah.
 
Na hata wakiendelea kuongoza hii nchi miaka elfu ijayo hakuna jipya litakalofanyika la tofauti na hapa uwezo wao ulipoishia.Wakae pembeni wajivue gamba walilokaa nalo toka uhuru labda watapata akili mpya.
They have reached their capacity limit. Hawana jipya.
 
Na hata wakiendelea kuongoza hii nchi miaka elfu ijayo hakuna jipya litakalofanyika la tofauti na hapa uwezo wao ulipoishia.Wakae pembeni wajivue gamba walilokaa nalo toka uhuru labda watapata akili mpya.
They have reached their capacity limit. Hawana jipya.
 
Ninamuona Magufuli aliyepambana na CCM yake mwenyewe kwa machozi. Haikuwa kazi rahisi kupambana na watu wa nyumbani mwake mwenyewe. CCM kama familia ndio waliofukuza machinga na mama ntilie kama mbwa katika nchi yao wenyewe, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake.
Madereva walikunywa viloba, ajali zikaua sana, tukasema Freemason wanatoa sadaka, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Yaliuzwa majenereta kwà kila duka, na wenyewe majereta wakauziwa mafuta, umeme ukachezewa, yakaundwa makampuni ya kuiuzia umeme TANESCO. Watu walipiga ela, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Wanasiasa waligawana maeneo mahekali kwa mahekali, waligawana maeneo ya madini, maeneo ya mbuga za wanyama, vyura walisafirishwa, walishindana kumiliki fukwe za bahari. Masikini hawakuwa na thamani. Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Mafuta yalipita bandarini bila kulipiwa kodi, makampuni yakabinafsishwa kwa bei chee. Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Leo hospitali za serikali zinajaa vijana wanaotibiwa baada ya kuathirika na madawa ya kulevya, kutokana tabia za watawala, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Sarafu za shilingi mia tano mia tano zilisafirishwa kwenda china, na biashara ilifanywa na watanzania, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Nchi nyingi zilipata sifa ya kuuza madini ya Tanzania, Magufuli akasema hapana, leo anaonekana hafai kwa sababu ya usisiem wake. Mema yake yanayeyushwa na wapenda madaraka.
Ndugu watanzania tusije jikuta tunakimbilia Pete iliyopakwa rangi ya dhahabu huku tukikanyaga dhahabu yenyewe. Sina tatizo na upinzani, ila nataka kusema kwamba unapotaka kubarisha gari uwe na sababu iliyo bora sana. Tusiongozwe na chuki wala mihemuko au ushabiki. Tukumbuke kwamba siasa is about our life and the future of this nation. Wish you uchaguzi mwema. Wakati wote Magufuli alipambambana CCM yake mwenyewe.


CLEMENCE MWANDAMBO MWALIMU WA CHEKECHEA. karibu Mbeya.
 
Kama kichwa chako kinamsaada katika maisha yako hebu jiulize maswali haya halafu ukisha jipa majibu uiangalie upya post yako.
Chukulia CHADEMA wameshinda uchaguzi mkuu wa October:-
i) Ma RC watawatoa wapi?
ii) Ma DC watawatoa wapi?
iii) makatibu tarafa watawatoa wapi?
iv) ma DAS watawatoa wapi?
v) ma balozi watawatoa wapi?
vi) ma RAS watawatoa wapi?
vii). siasa inayoilinda nchi hii je wanaijua? Na kwa muda gani?
viii) Je, nchi itaongozwa kwa utulivu wa kina kama tulionao au ndio kila mmoja ataongoza kivyake kwakuwa watakuwa wageni katika maswala ya kuongoza nchi?
ix) Je,ndani ya chama wanachaguana kwa kuangalia uwezo wa mtu katika nafasi anayoitaka au wanaangalia anayeweza kuongea?
x)................?

Baada ya hapo tuweke ushabiki pembeni.



MAGUFULI4LIFE.
Rubbish..
Tz ilipopata uhuru Nyerere alipata wapi hao??
 
Kama kichwa chako kinamsaada katika maisha yako hebu jiulize maswali haya halafu ukisha jipa majibu uiangalie upya post yako.
Chukulia CHADEMA wameshinda uchaguzi mkuu wa October:-
i) Ma RC watawatoa wapi?
ii) Ma DC watawatoa wapi?
iii) makatibu tarafa watawatoa wapi?
iv) ma DAS watawatoa wapi?
v) ma balozi watawatoa wapi?
vi) ma RAS watawatoa wapi?
vii). siasa inayoilinda nchi hii je wanaijua? Na kwa muda gani?
viii) Je, nchi itaongozwa kwa utulivu wa kina kama tulionao au ndio kila mmoja ataongoza kivyake kwakuwa watakuwa wageni katika maswala ya kuongoza nchi?
ix) Je,ndani ya chama wanachaguana kwa kuangalia uwezo wa mtu katika nafasi anayoitaka au wanaangalia anayeweza kuongea?
x)................?

Baada ya hapo tuweke ushabiki pembeni.



MAGUFULI4LIFE.

Kwahiyo hizo nafasi zikijazwa na watu wapya itatoa Ajira mpya kwa wengine wenye mawazo na mbinu mpya za maendeleo...
 
CCM kuendelea kutawala Tanzania ni aibu, kashfa isiyo na mfano. Kazi ni moja tu oktoba kuitosa 'baharini ' itokomee kusikojulikana daima milele.
 
Kuyapata uliyoorodhesha tunahitaji mgombea jasiri mwenye uthubutu huu:

View attachment 1527407
Huo ndiyo ulio ukweli.

Huyo ndiye ambaye atakaye tuvusha.
Vyote hivyo Mh.Lissu anavyo na zaidi,lakini huko CCM mpya hayo hayajadiliki maana wametekwa na Uncle Meko na timu yake.Bila kuiondoa madarakani hatuwezi kuota mambo ya haki za binadamu.
 
Magu ni Hadi atacha kuwatumikia wananchi, hajawahi kushindwa na hatoshindwa kamwe na mpinzani awaye yote, hii yote ni Kwa sababu historia yake ya utendaji na uthubutu wake, Unambeba, huwezi kushindana na mtu ambaye historia yake inamzungumza Kwa mengi mazuri, na Watanzania sidhani kama wanaweza kumwachia huyu mtu kizembe kizembe kiasi hiki, kisa tu kuna mtu anayebebwa na tukio la kuumizwa katka maisha yake

Wapinzani sio kwamba ni wabaya, hapana, ni watu wazuri, wanajua wanataka nini, Nia zao ni njema Kwa ajili ya nchi yetu!

Na mawazo na hotuba ya Mh Lisu Jana, ni hotuba moja nzuri na mpya masikioni mwa wengi, inaacha maswali na kiukweli inapaswa ishughurikiwe na KUFANYIWA KAZI sasa!

Ila,kumwacha Magufuli, itakuwa ni bonge la Ujinga nchini, Kwa vitu vingi vikuubwa alivyothubutu kuvianzisha na kuvifanya Kwa kipindi hiki kifupi, Dunia na washindani wa nchi yetu hasa majirani zetu watatucheka

Nchi yetu inawatu wengi mahiri na wazuri, Lisu ni mtu mahiri na mzuri Kwa vitu vingi, ika Kwa sasa! Hapana, angojee Kwanza, sababu, ni wetu, kakutana na mtu mwingine mzuuri zaidi basi
 
Mfumo ndio unaokwenda kubadirishwa jipe muda kusikiliza mipango ya baadhi ya wagombea wanazungumzia tatizo la mfumo mbovu wa utawala ndiyo msingi wa umasikini wetu na huo ndiyo kubadilishwa CCM haiwezi kuubadilisha sababu unainufaisha. Kama wanavyokataa katiba mpya na tume huru.
 
Hahahaha, alot of funny.

Kwamba CCM, Ikitoka madarakani hivyo vyote ulivyoviandika vitakuwa sawa.

Acha kuota mchana(day dreaming) mkuu.

Bado mfumo wetu ni mbovu.

Madaraka ni matamu, hata upinzani ukiingia umaweza nogewa na kuwasahau hao uliowaandika.
Daah dish limeyumba
 
Hahahaha, alot of funny.

Kwamba CCM, Ikitoka madarakani hivyo vyote ulivyoviandika vitakuwa sawa.

Acha kuota mchana(day dreaming) mkuu.

Bado mfumo wetu ni mbovu.

Madaraka ni matamu, hata upinzani ukiingia umaweza nogewa na kuwasahau hao uliowaandika.
Ila utamu wa madaraka wa awamu ya 5 umezidi hadi figisufigisu kwa wagombea kumbe wagombea wanatakiwa wajue karate na kutumia silaha?
 
Wasalaam, CCM imetuongoza watanganyika kwa takribani miaka 59 na kuongeza umasikini miongoni mwetu. CCM imepoteza dira hakuna Sera au mawazo mbadala inafaa sasa ipumzike sababu za kuipumzisha ni hizi;

1. Rushwa (wajumbeee)
2. Umasikini wa kutupa (wanyonge)
3. Maslahi duni kwa Watumishi wa Umma (watawala maisha ya peponi anasa)
4. Ukandamiza wa Uhuru na democrasia
5. Usiri ktk mikataba ya madini na gesi (bunge mhimili wa ccm sio taifa)
6. Elimu duni kwa watt wa malofa
7. Ukosefu wa ajiri (wahitimu vyuo vikuu)
8. Utapeli kwa wakulima (korosho)
9. Polisi kunyanyasa RAIA (kesi za kubambika)
10. Ubaguzi (kurisishana madaraka, kutesa wapinzani)

Tukutane Oktoba 28. Delete CCM kwa manufaa ya mama Tanzania, maana maendeleo yana vyama.
Wote tuseme sasa 'basi'

sore but ccm is here to stay 2100 ndo wnaweza kufikiria vyama vingine
 
Back
Top Bottom