Tuunganishe mawazo wandugu

Tuunganishe mawazo wandugu

Nicorandil

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2022
Posts
258
Reaction score
749
Habari za usiku ndugu?

Natumai mu wazima wa afya.

Nimekuwa nikiwaza namna nzuri ya kuwekeza pesa yangu niliyoipata hivi karibuni, 3m. Nikataka kuiweka katika fixed account lakini kila nikiwaza benki kukaa na pesa yangu kwa mwaka na zaidi halafu kunipa 9.5percent rate naona ni ndogo.

Hivyo nikawaza kuiweka walau nusu UTT na nusu katika fixed account. Tena nikapata wazo kutembelea bureau de change nakuigeuza dollar ili isishuke thamani. Kama mnavyoona mawazo ni mengi lakini naamini wapo watu watakaonipa mawazo mazuri zaidi au kuboresha ya kwangu.

Katika yote sijaongelea kufanya biashara kwa sababu sina mpango huo kwa sasa kutokana na kuwa na kitu kingine kinachohitaji uwepo wangu muda wote na vile vile sina matumizi nayo kwa sasa ila nataka kulinda thamani yake au iongezeke. Asanteni na karibuni.
 
Duh! Tafuta rafiki aliyepo machimbo ya dhahabu mwaminifu akununulie dhahabu isiyo na process kama 27g zitunze utauza huko baadae. Japo kdg ni complicated kwa mtu mgeni ila kwangu ndio njia nzuri ya kutunza fedha.
 
Una huyo mtu muaminifu kwenye hayo masuala ya madini?
Ndio ila tafuta mwenyewe binafsi siwezi kutoa msaada wowote zaidi ya wazo hilo tu, tafuta mwenyewe ktk chain yako
 
Utunzaji wa uhakika wa pesa ambayo huna kazi nayo In a long run ni kwenye ardhi tu! Period

Kua makini tu usije pigwa kwenye ununuzi maana ma dalali Kila siku wanaushangaza ulimwengu
 
Ooh Hela utunze, duuh.

Haya sawa katoe sadaka Kwa bwana muumba wako utaikuta ikiwa mara70 yake huko mbinguni.
 
Ebu kanunue kiwanja au itumie tu kama huwezi small business.

Pesa ndongo hivyo uweke utt au fixed ni kujisumbua tu na kupoteza muda. Hakuna utakacho ambulia be smart!
 
Habari za usiku ndugu?

Natumai mu wazima wa afya.

Nimekuwa nikiwaza namna nzuri ya kuwekeza pesa yangu niliyoipata hivi karibuni, 3m. Nikataka kuiweka katika fixed account lakini kila nikiwaza benki kukaa na pesa yangu kwa mwaka na zaidi halafu kunipa 9.5percent rate naona ni ndogo.

Hivyo nikawaza kuiweka walau nusu UTT na nusu katika fixed account. Tena nikapata wazo kutembelea bureau de change nakuigeuza dollar ili isishuke thamani. Kama mnavyoona mawazo ni mengi lakini naamini wapo watu watakaonipa mawazo mazuri zaidi au kuboresha ya kwangu.

Katika yote sijaongelea kufanya biashara kwa sababu sina mpango huo kwa sasa kutokana na kuwa na kitu kingine kinachohitaji uwepo wangu muda wote na vile vile sina matumizi nayo kwa sasa ila nataka kulinda thamani yake au iongezeke. Asanteni na karibuni.
Mkuu kabla ya yote, ebu fanya basi angalau ata 10000 uninbless ndo tuongee vizuri 😁 serious ujue
 
Back
Top Bottom