Tuwafahamu wajumbe wa Task Force ya Msajili

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Itakuwa ni kujidanganya mchana kweupe, kudhani kuwa hali ya kisiasa nchini ni shwari na kuwa kazi inaendelea.

Taarifa rasmi kutokea katika mkutano huo wa kusaka tahfifu katika siasa kwa wadau ni kama ilivyo hapa chini:





Hiyo ndiyo habari yenyewe.

Kama vipi kuwafahamu wajumbe hawa zaidi majina ikiwamo wasifu, mafungamano yao kisiasa, kuaminika katika jamii, vigezo vya kuwamo, nk ingependeza zaidi.

Tukawe na Christmas njema yenye tafakari ya yaliyo mema kwa taifa letu.
 
 
Tungekuwa na umoja wakujadiliana vipaumbele vya Nchi na siyo vipaumbele vya kila anaeingia kukalia kiti kubwa nakuvishwa mamlaka
 
Tungekuwa na umoja wakujadiliana vipaumbele vya Nchi na siyo vipaumbele vya kila anaeingia kukalia kiti kubwa nakuvishwa mamlaka

Vikwazo ni viroboto, wahuni na matapeli waliojaa upande wa pili
 
Tume huru ya uchaguzi bila katiba mpya ni sawa na kuziba mashimo ya panya kwa mikate!

Maana Tanzania uchaguzi ni mfumo sio tume tu.Nguvu ya Rais na wateule wake, polisi, TISS, Jeshi, Tume, Tamisemi na wengineo lazima viangaliwe kwa pamoja kupitia katiba mpya.

Hiki kinachoitwa ni Tume huru ya uchaguzi ni changa la macho kwa wajinga ambao ndiyo wengi kwenye hii nchi.
 

Kwa kweli wanatuona mazuzu kweri kweri:

".. ni sawa na kuziba mashimo ya panya kwa mikate!"

Tume huru na katiba mpya ni kwa mujibu wa matakwa ya wananchi wanaoathirika na utawala madarakani.

Utawala uliopo hauwezi kutoa suluhu ya uozo huu yenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…