Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Haaaahaha kwani huyo Kapuya mwenyewe pamoja na uprofesa ni mtu mwenye akili kweli??? Huyo Kapuya watakua ni wale watu toka sekondari hadi chuo kikuu ni watu wa madesa na connection mwisho wake wanatusua kibahati lakini upstairs ni zero. Simba huzaa Simba hata siku moja hawezi zaa mbuzi.
 
Lyatonga si ndy alituchomesha akawaribia wabongo viza UK
Entry
Bandika bandua watu walizipiga sana

Ova
Sio Lyatonga aliechomesha alikua Hassan Diria akiwa waziri wa mambo ya nje wapemba/waunguja +wabara wajanja wajanja wengi walikimbilia Kenya then wanaruka mamtoni, ndio akawashtua waingereza mchongo wakauziba wakafuta entry wakaweka viza kuanzia 1996.
 
Wanamuziki wa Congo wanakwama wapi? Mbona wanaonekana wana hela ila bado wana ishu za kusifia sifia watu ovyo kama vile machawa?
acha tukuelimishe kidogo.
kwa mziki wa rhumba ambao asili yake ni congo, kutaja majina ya watu na kuwasifia ni utamaduni wa siku nyingi. umeanza kitambo sana tangu enzi za kina franco luambo makiadi.

kwao kutaja majina ya watu mashuhuri kwenye nyimbo ni lifestyle, ni sehemu ya ufahari kwa pande zote mbili, anaetaja na anaetajwa(win win situation).ni platform ya kujitengenezea brand ktk jamii, ni sehemu ya kuonyesha uwezo wako wa kipato na mamlaka. pia ni sehemu ya ku establish close friendship kati ya wanamuziki na anaetajwa.

wapo wanaotajwa bila hata ya kuombwa fedha na wanamuziki. wanamuziki wenyewe wanajisikia proud kutaja majina hayo.

kuna track moja ya franco ilitoka mwanzoni mwa miaka 80s, inaitwa "candidat na biso mobutu"(itafute youtube),humo ndani mwanzo mwisho franco anamsifia aliyewahi kuwa rais wa taifa hilo mobutu sese seko.

tukija kwenye suala la kipato,wanamuziki wa congo level ya akina mpiana, koffi na werra wapo vizuri sana kifedha, usiwachukulie poa. baadhi yao wanamiliki majumba paris na brussels.
 
Franco alikuwa Sungura inasemekana alikuwa na bifu na Rais Mobutu akakimbilia Ufaransa, basi uchaguzi ulipokaribia ndio Franco akatowa hiyo nyimbo ya kumsifu kumpamba na kumuabudu mobutu.

Mobutu baada ya kusikia hiyo nyimbo alimpigia simu Franco na kumuomba arudi nyumbani azunguke naye kwenye kampeni kama Kapteni Komba na CCM.
Baada ya Franco kukubali proposal ya Mobutu basi alitumiwa ndege kubwa Ufaransa kwa heshima yake imrudishe nyumbani Zaire.
 
Usichanganye mambo. Tchatcho ni aina ya muziki uliobuniwa na Koffi enzi hizo. Akawa anaupromoti kwenye nyimbo zake. Ila Chacho anayeongelewa ni mtu kwa jina la Chacho Mbala.
ahsante sana kwa uafafanuzi nimekuelewa vizuri sana mwamba[emoji123]
 
asante kwa dondoo kaka.[emoji1431][emoji1431][emoji1431]
 
Kapuya ana akili za darasani,sema ujana wake hakula sana bata! Lakini baada yakupata pesa na akapata nafasi serikalini ndiyo akaamua kula bata! Sasa ndiyo maana kwenye matukio ya ajabu ajabu jamaa alikua anaonekana
 
Umesema kweli kabisa mkuu! Wanamziki wengi sana wa Congo hua wanataja majina ya watu maarufu! Kuna wimbo mmoja nadhani ni Masuwa wa JB Mpiana,kuna sehemu anamtaja mtoto wa Mobutu,nadhan anaitwa Joseph aka Sadam Sele,ukisikiliza vibaya unaweza sema anamtaja Sadam Hussein aliyewahi kua Rais wa Iraq
 
Ha hah ila Wakongo na njaa zao wakiamua kukupamba utapewa kila aina ya cheo,wewe warushie buku 10 tu na usikose kwenye dansi lao.ila shida wakikuzoiea wanahamishia shida zao kwako.
Sema wacongo kwa kutunga majina wako vizuri. Imagine kuna mtu wakawa wanamwimba "ASKOFU WA KWANZA" 😄😄. Hadi kuna mdau hapa kauliza kama huyo Askofu ana uhusiano na kanisa
 
Edhi = Enzi
 
huyo jamaa jina lake lilitajwa sana na wenge BCBG katikati na mwishoni mwa miaka ya 90 kabla ya viongozi wa kundi hilo(jp mpiana na werrason)kutofautiana.

alikuwa ni mtoto kipenzi wa rais wa nchi hiyo mobutu seseseko. jina lake halisi ni Kongulu Mobutu, ila wanamuziki kwa kunogesha, walimpachika jina la sadam hussein(wenyewe wakitamka sadam sene) wakifananisha ushupavu wake na rais wa iraq sadam hussein baada ya kuwashinda wamerakani ktk vita ya desert storm iliyopiganwa miaka ya 90.

Kongulu aka "sadam sene" alikuwa very powerful and fearful enzi za utawala wa baba yake halafu bata boy sana.jiji la Kinshasa na viunga vyake vilikuwa kwenye himaya yake, hakuna aliyeweza kuleta vyoko mbele yake.alifariki mwaka 1998.

hapa JF kuna nyuzi kadhaa zinazomzungumzia,moja wapo ni hii hapa.unaweza kuipitia ili upate mawili matatu kumuhusu:Fahamu machache kuhusu special presidential division: Kikosi maalumu kilichomlinda Mobutu Seseseko enzi za utawala wake
 
Wana pesa mno,magari aliyonayo koffi olomide, fally na JB mpiana wasanii wetu hawana,hao jamaa Wana ma Bentleys,Ferrari,rolls Royce, mtu Kama JB mpiana alikuwa na Mercedes Benz mwaka 1999 huko
Wafuatilie YouTube uone mijengo yao
Mercedes Benz model ipi?maana hata hapa bongo watu wa kawaida tu hizi Mercedes(C-200,C-230,,E-240,E-320) walikua nazo, Mwenye S-class miaka ndio angetisha sana
 
Kizaizai naona hali si nzr sahv
Ashukuru Ana kibanda kigamboni
Alafu kizaizai kama anajua kusoma
Na kuandika labda atakuwa amejifunza sahv

Ova
Kizai zai chokq mbaya anapanda boda boda saivi...kigambon nyumba aliuza baada yakumwuzia bmw mtoto wa wazir flan zenj ,bmw ilikua na gia box mbovu ikaamuliwa arudishe pesa akawa hana ndo akauza nyumbq yake kigamboni....kuandika wala kusoma hajui muda wote alikua anatembea na chawa wakusoma mesej zikiingia nakujibu
 
Duh kumbe kauza kibanda
Sasa kwa wakati huu utamtaoeli
Nani kiboya,kila mtu anakuwa mjanja
Yah nilishasema humu jamaa hajuwi
Kusoma wala kuandika,namjua kizaizai tokea anaoshaga magari mjini hapa
Na nilishawahi kumchanaga ktk vitu muhimu ajifunze kusoma na kuandika tu,vitamsaidia mbeleni
Sema wasiyojua kusoma na kuandika wanakuwaga wajuaji sanaaa

Ova
 
Mercedes Benz model ipi?maana hata hapa bongo watu wa kawaida tu hizi Mercedes(C-200,C-230,,E-240,E-320) walikua nazo, Mwenye S-class miaka ndio angetisha sana
Mercedes 200 , cabriolet, MERCEDES 190, Mkuu lakini zilikuwa Ni gari nzuri Sana Sina hakika Kama Kuna wasanii huku walikuwa nazo au wanazo
 
Usifanye masihara na mtu asiyejua kusoma na kuandika halafu amekulia mjini. Huwa wanajitahidi kuwa wajanja sana. Kuna jamaa nilifahamiana naye zamani alikuwa anafanya biashara ya madawa ya mifugo. Alikuwa anazijua dawa balaa tena yeye Wafugaji walikuwa wanapenda bidhaa zake (alikuwa hana duka ni mkono kwa mkono) kwa sababu walimchukulia ni msomi. Akiwa na bidhaa dawa mpya ananitafuta nimtafsirie matumizi kwa Kiswahili na mambo mengineyo kwenye bidhaa, hapo ananipanga nimuone labda ni Kingereza tu cha kwenye bidhaa ndiyo kinampa shida (kwa sababu mdomoni kuchanganya this na that yupo vizuri), akitoka hapo akienda kwa wafugaji hata wale wakubwa wanachukua bidhaa chapu. Siku moja ndiyo rafiki ananiambia jamaa kusoma na kuandika hajui, nilishangaa sana! Halafu alikuja kuoa Mwalimu wa shule ya msingi hahaaa!!
 
Umemsahau fikir madinda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…