Tuwape PhD za heshima wazalendo kama Salim Bakhresa, sio wanasiasa wala rushwa

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Tanzania ni nchi ya maajabu sana vyuo vimejaa siasa. Mtanzania mzalendo kama Salim Bakhresa sijasikia vyuo vikitaka kumpa PHD ya heshima badala yake inawapa wanasiasa ambao hawana sifa.

Salim Bakhresa amejenga biashara na kutoa ajira kwa mazingira magumu sana. Hajawahi na wala hana sifa ya kutoa rushwa kwa miaka yote hii. Ni kati ya walipa kodi wakubwa Tanzania. Wamedumisha michezo, afya, ajira na mpaka kusaidia jamii kwa kuwekeza kwenye usafiri wa maji.

Kwa upande mwingine tunatoa PHD za heshima kwa wanasiasa ambao kila mtu anajua hawajachaguliwa kihalali, wala rushwa, wanatumia pesa vibaya, wanateka wapinzani wao, wana ingia mikataba mibaya kwa nchi ya siri. Kila mtu najua hili. Yaani ni wala rushwa wakubwa na wakati mwingine wanatumia madaraka kujitajirisha na mifano tunayo.

Kama jamii tuwapongeze wanao stahili na uzalendo sio kabila, rangi ya mtu au ni jamii gani ya mtu uzalendo ni vitendo. Hawa wanaojifanya wanafanana na sisi ndiyo nyuma nyuma wanakula pesa zetu na kujiona ni bora.
 
Tanzania ni nchi ya maajabu sana vyuo vimejaa siasa. Mtanzania mzalendo kama Salim Bakhresa sijasikia vyuo vikitaka kumpa PHD ya heshima badala yake inawapa wanasiasa ambao hawana sifa...
Sahihi kabisa, ni wakati wa Bakhresa kupewa PhD za heshima, wamechelewa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…