Tuwe Makini wasichana tutadanganywa mpaka lini??

Tuwe Makini wasichana tutadanganywa mpaka lini??

mimi ni mwanaume, stori yako kama yangu, imenigusa sana. mimi nilimfuma mtarajiwa wangu ktk mazingira hayo, akina dada nao pia noma. nimem mwaga mwaaaah! nawe fanya hivo, utapona
Nashukuru wana jf kwa makaribisho mazuri,
hivi inakuwaje mwanaume anakuwa muongo anakudanganya for two years kwamba hajaoa, then unakuja unagundua kaoa ,ana mke na watoto
Mie nimedanganywa na sasa niko kwenye maumivu makali ili niweze kuendelea na maisha,nilikutana nae chuoni yeye anasoma masomo ya juu zaidi yangu, akasema yuko single na mipango yote ya kuoana tukimaliza chuo alikuwa ananiambia.

Yeye alitangulia kumaliza lakini alikuwa anasafiri anakuja kuniangalia chuoni, baasi nilipomaliza kwa vile tunakaa mikoa tofauti nikaamua kumzukia kwa suprise huko anapoishi, nilienda nilipofika mojakwa moja hadi ofisini, kastuka sana, tukatoka nikajua napelekwa kwake akaishia hotelini, jioni alipokuja ndio akanimwagia hilo shuzi, eti sorry,hivi kweli binadamu wamekuwa na roho mbaya kiasi hiki?nawaasa wasichana wenzangu wawe makini sana na hawa wenzetu kwani sio kila kitu wanachosem ni kweli....sasa nikaamua kukatisha mawasiliano kabisa kwa kipindi kirefu kiasi
juzjuz kaja na mpya kaniomba anioe mke wa pili kwamba hawezi ishi bila mimi, marafiki zangu wanavutana wengine wanasema nikubali na wengine wanasema niendelee na msimamo wangu, je wewe mwana jf mwenzangu unasemaje?????
 
Angekwambia ukweli ungemchuna sana.
Hapo yenyewe tu bado ulimchuna akulipie gharama za masomo. Kwa hiyo acha na yeye ajifaidie.

Nyie mnaomshauri mmeolewa?

Porojo tu.
Mnadanganyika kila siku, halafu kujifanya uhodari wa kushauri.

Halafu bado anajifanya anataka ushauri.

Huwa hamuwakubali watu wakweli nyie.
Acha muendelee kuumizwa kwani mnapenda makuu mno.
We humuoni mtu alivyo kiuchumi, hujiulizi huko nyuma koooote alikopita hajapata mtu kweli. Tamaa zenu zinawaponza.

Cha muhimu jamaa kapata alichokipata, MBWECHE. na binti pia kapata alichokipata, MAFAO na gharama za masomo.
Mnapenda sana kukuta mambo tayari yapo mazuri.
Hampendi kuanza na mtu kapuku ili mjenge wote maisha.
Dawa yake ndio hiyo.

Ulistahili ulichokipata.
Kwani unaonekana ulikuwa unajilazimisha kudanganywa.

Mwenzenu bado anampenda mtu wake.

Ndo ameshajitangaza hivyo kuwa yuko singo na anatafuta mwenza. Changamkia tenda hiyo.

Mnakuwa hamna shuli nyingine za kufanya zaidi ya mapenzi.

Atampata wapi?

Watu kama nyie ndo huwa mnapatikana kirahisi mno.

Vile vile ameshatumika sana, kwa hiyo jamaa wa watu atakayefuatia maskini atakuta kitu kimetumika sana. Uonevu huu.

Wivu autoe wapi na yeye kiu yake ni kuolewa.

Ndo kilichokuponza hicho.

Wanaume hawapatikani kirahisi hivyo.

Ili umfate wewe

Na amefanikiwa kumchezea.
Atakaefuata nae hivo hivyo.

Kupenda makuu ndo kunakowaponza hawa.

Upekue wee umekuwa CID

Mwache mwenzio apate ndoa naye. hata kama atakua mke wa saba, cha muhimu atimize azma yake ya kuolewa.

Ulistahili ulichokipata

Watu kama nyie ndio rahisi sana kudanganywa. Huenda hapo ulipo umeshadanganywa mpaka basi.

And that is the price they are paying for.

Hata akiwa mke mmoja, zamu zipo tu.
Duh jamaa nahisi kama ndio huyo mme wa mtu au mwaonaje wakuu, cheki majibu yake utadhani ana uhasama na SaraM
 
mimi ni mwanaume, stori yako kama yangu, imenigusa sana. mimi nilimfuma mtarajiwa wangu ktk mazingira hayo, akina dada nao pia noma. nimem mwaga mwaaaah! nawe fanya hivo, utapona
Pole na wewe kwa kudanganywa, yaani mke wa mtu nae kakudanganya au ni msichana tu
 
Yaani nina wivu wa hatari mwanajamii, nilipenda hasa

sikutegemea mambo ambayo tulishakaa tukayamaliza kama ungekuja kuyaleta humu watu watujadili. mi naendelea kukushauri uendelee na msimamo wako ulioniambia kuwa tutaoana. am still saying am sorry.
 
Nyumba Kubwa...thanks for this

My only problem ni kwamba wengine wanakuwa too cautions kiasi wkamba wanamistake a genuine relationship na hizi za kimazabe mazabe....the fact is...kwa baadhi yetu tunapokuapproach tunakuwa tumeshafanya some decisions kwamba huyu ndiye, sasa bahati mbaya kama unakuwa umetokea kwenye hali kama hii, inakuwa rahisi 'kumfukuza' yule anayekupenda kwa dhati. Madhara yake ni kwamba unakuwa umepoteza nbahati nyingi kwa hili, na sometimes wengine huwa haturudi nyuma hasa baada ya kufanya kila juhudi....of course kwa kukubaliana na 'ukweli' kuwa pengine hupendeki so why hang on? nadhani umenipata walao ama nimejikanyaga kanyaga (hasa akiwepo lovebird wangu AshaDii akili huwa hainikai sawa)
Sasa hapa kifanyike nini ili niepuke kufanya hii mistake yaani nisijudge watu wrong?
 
Ushauri kwa wadada:
1. sio kila urafiki wa mapenzi lazima uishie kwenye kuoana,
2. Ingekuwa 1 hapo juu ni sahihi, basi maneno mabuzi na vicheche visingekuwepo,
3. Mwanaume anapokutongoza usitangulize maneno, 'nataka kuolewa sitaki kuchezewa,
4. Kama mwanaume humtaki na wala huna haja ya hata kumfanya rafiki yako wa kawaida, usijenge mazoea ya kuonana naye,
5. Unapohisi mwanaume amekuvutia na anaweza kuwa mpenzi wako, mpe masharti ya kufuata ili akuhakikishie kuwa atakuoa, lakini wakati hu huo ujue nafasi yako katika uhusiano huo. Usije ukamkubalia kusex eti kwa sababu ameonyesha nia ya kukuoa kwa hiyo ili afurahi basi ni bora umuonjeshe,
6. Kununuliwa vitu vizuri vya thamani sio uthibitisho kwamba wewe ni mke wake kama bado hamjaenda mbele ya DC, shekhe, mchungaji au Paroko/padri,
7. kama humtaki usichukue na vitu/zawadi anazokupa. Ikiwa mwanzoni ulimwambia humpendi, na mwanaume akachukulia hivyo lakini wewe ukaendelea kumtumia kwa ajili ya kupata mahitaji yako, ni sawa na kujidhalilisha hivyo lazima mwanaume awe ameoa au lah, atahakikisha gharama zake zilete dividends.

Nilichungulia kidogo tu, naenda zangu!
Ndyoko, dont judge me wrong here, huu uhusiano ulianza kawaida sana kama mingine, na kumbuka ni yeye ndio aliyekuwa anasema mambo ya kunioa, na mie kwa kujua ni mpenzi wangu nilijua tungeishi wote milele sababu nilimpenda sana huyu kaka,sikuwa na sababu ya kuwaza otherwise
 
sikutegemea mambo ambayo tulishakaa tukayamaliza kama ungekuja kuyaleta humu watu watujadili. mi naendelea kukushauri uendelee na msimamo wako ulioniambia kuwa tutaoana. am still saying am sorry.
Mtego wa noti, acha kunitega bwana
 
Achana na mme wa mtu.Alikudanganya,sasa unamwaminije anaposema bila wewe hatoishi?Tumia akili vizuri angalia ten years to come.Eti uwe mke wa pili jaribu,nakuambia UTAJUTA.Kama ulikuwa huwajui waganga wa kienyeji utawajua.ACHANA NA MME WA MTU
 
Mme wa mtu wa nini? achana naye utakuja juta, alikudanganya ili akutumie tu, anza masha upya utapata wako wa peke yako
 
Nashukuru wana jf kwa makaribisho mazuri,
hivi inakuwaje mwanaume anakuwa muongo anakudanganya for two years kwamba hajaoa, then unakuja unagundua kaoa ,ana mke na watoto
Mie nimedanganywa na sasa niko kwenye maumivu makali ili niweze kuendelea na maisha,nilikutana nae chuoni yeye anasoma masomo ya juu zaidi yangu, akasema yuko single na mipango yote ya kuoana tukimaliza chuo alikuwa ananiambia.

Yeye alitangulia kumaliza lakini alikuwa anasafiri anakuja kuniangalia chuoni, baasi nilipomaliza kwa vile tunakaa mikoa tofauti nikaamua kumzukia kwa suprise huko anapoishi, nilienda nilipofika mojakwa moja hadi ofisini, kastuka sana, tukatoka nikajua napelekwa kwake akaishia hotelini, jioni alipokuja ndio akanimwagia hilo shuzi, eti sorry,hivi kweli binadamu wamekuwa na roho mbaya kiasi hiki?nawaasa wasichana wenzangu wawe makini sana na hawa wenzetu kwani sio kila kitu wanachosem ni kweli....sasa nikaamua kukatisha mawasiliano kabisa kwa kipindi kirefu kiasi
juzjuz kaja na mpya kaniomba anioe mke wa pili kwamba hawezi ishi bila mimi, marafiki zangu wanavutana wengine wanasema nikubali na wengine wanasema niendelee na msimamo wangu, je wewe mwana jf mwenzangu unasemaje?????
pole sana ndio ukubwa
 
Pole sana dada, usiwaze wala kupata pressure maisha lazima yaendelee. Sikushauri uingie ktk maisha ya zam zam kupeana unyumba, tulia, jipe muda pia ongeza vigezo vya kumpata huyo mwingine na usikimbilie mahusiano mapya mapema.
Amin kuwa Mungu hajakutupa riziki yako ipo palepale. Kuwa na iman, subira na uvumilivu kwan ukipapalika utahisi Mungu kakutupa au umepewa kisogo na dunia.
 
Hata usikubal shoga yangu, mchunie 2 angekuwa na nia nzur angekwambia tangu mwanzo kuwa anakupenda ingawa ana mke, ww ndio u decide. Pole mwaya utampata wako il uwe unalala na kuamka nacho.
 
....mungu haajakuleta kwa bahati mbaya,kwa nini uwe mke wa pili?najua unaumia lakini yataisha.piga moyo konde na anza upya
 
msichana fikiria kwa makini sana kabla hujaingia kwenye dunia ya uke wenza, utajutia maisha yako yote
 
Ndyoko, dont judge me wrong here, huu uhusiano ulianza kawaida sana kama mingine, na kumbuka ni yeye ndio aliyekuwa anasema mambo ya kunioa, na mie kwa kujua ni mpenzi wangu nilijua tungeishi wote milele sababu nilimpenda sana huyu kaka,sikuwa na sababu ya kuwaza otherwise
<br />.ucpende kujipa uhakika na guys wa sikuhz na sidhan km ndo unaanza mapenzi.
<br />
 
We mdada nadhan ulikuwa huwajui guys na hujawah kuumizwa.baada ya kukukuta hayo utakuwa mzoefu na mapenz.mapenz bana ukiumizwa ndo unafunguka akili.hongera kwa kufikia hatua hiyo
 
We mdada nadhan ulikuwa huwajui guys na hujawah kuumizwa.baada ya kukukuta hayo utakuwa mzoefu na mapenz.mapenz bana ukiumizwa ndo unafunguka akili.hongera kwa kufikia hatua hiyo
Ni kweli kabisa mkuu bila kuumizwa huwezi elewa kabisa haya mapenzi, maana utakuwa unayachukulia kwa upande mmoja tu
 
We mdada nadhan ulikuwa huwajui guys na hujawah kuumizwa.baada ya kukukuta hayo utakuwa mzoefu na mapenz.mapenz bana ukiumizwa ndo unafunguka akili.hongera kwa kufikia hatua hiyo
Kweli ukiumizwa unajengeka fulani, na kuwa na machale wakati wote
 
msichana fikiria kwa makini sana kabla hujaingia kwenye dunia ya uke wenza, utajutia maisha yako yote
Nimefikiria tayari na nishaamua kumove on ahsanteni sana kwa mawazo yenye busara wandugu
 
Back
Top Bottom