Na gia zinavyobadilishwa angani huko wallahi bin Taabana Tanganyika tutaisoma Namba.
Wazanzibari wanatuchukia kwa nguvu zote na kutubagua kwa maksuidi tukiwa huko Zenji.
Ajira za serikali za Zanzibar inabidi uwe mzanzibari na ukilazimisha kuomba watabaki kukushangaa kwenye interview umeenda kufanya nini, wao wanaomba kote kote za huku bara tunazogawana nao na huko kwao kwajili ya peke yao.
JKT wabara wakimaliza mafunzo ni ngumu sana kupenya idara za ulinzi ila Zanzibar wananynyekewa sana kuingizwa idara za ulinzi, wabara wengi wanamaliza JKT pale wanarudi kulima vijijini ama kwenda Suma JKT kupokea mishahara ya laki 2, wachache sana wanatoboa kwenda idara za ulinzi, kwa Wazanzibari yani kumaliza JKT ni shavu.
Ardhi, leseni za udereva, siasa, n.k, mavyo vishazungumziwa sana kuhusu tabia ya vyao kutoguswa.
Hapo ndiyo unajua Karume was genius, Nyerere was a genius. La muhimu ni Muungano, udugu wenu na maslahi yenu ya msingi.
Umetoa mfano JKT, sawa,
mnamaliza kuruta 70,000 wakiwamo Wazenj 17. Hivi kweli unataka watu elfu 70 mkagombee nafasi 7 kulinda Mjimkongwe? On the other hand? Wazenj 7 ukiwapeleka Mbweni wala hawamzibii mtu yeyote ajira. Kwa nini mpiganie "usawa" usio na tija?
Kuna swali la Ardhi. Mkoa wa Lindi, mzuri, green, kinganisha na Pemba ya square kilometre 1500 yaani 30 kwa 50 kms, tayari pamejaa, watu laki 4!.
Mkoa wa Lindi watu milioni 3, pori, square kilometre 20,000 (km 200x100). Waje Wapemba 70 porini Mkuranga? No problem (as long as siyo UAMSHO terrorists). Watalima mahindi, ndizi na machungwa bila shida, wala hatutawaona. On the hand peleka Wachagga au Wamatumbi Wachagga laki 5 Pemba watakaa wapi? Kama wenyeji ni.laki 4 tu, mtaoa wapi?
Mfano wa Wachagga na Wamatumbi ni huo huo, Wamatimbinhawawezi kwenda Kirua Vunjo kumejaa. As long as ni Nji moja, kwa nini tupiganie usawa wa bandia usio na tija?
Of course mambo ya msingi yapo, mtafuata sheria, km currency, sera za diaspora, uhuru wa dini, ulinzi, nk. Kama
ingekuwa Muungano na Kenya hapo ingebidi muwe sawa bin sawa.
Muungano wetu ni wa kikwelikweli, Rais akitoka huku Makamo atoke kule, tuliyaona kwa Mwinyi, tumeyaona kwa Samia. Nyerere na Karume waliona mbali sana, Mungu awabariki.