Tuwe Wakweli, tutapataje Katiba Mpya kama hatutampitisha bila kupingwa Rais Samia 2025 ili akatukamilishie Mchakato kuelekea 2030?

Hivyo kama kweli tunahitaji Katiba Mpya basi 2025 mama Samia apite bila kupingwa na fedha itakayookolewa kwa kutofanya Uchaguzi wa Rais ipelekwe kugharamia Mchakato wa Katiba Mpya.
Kwa kuwa misimamo ya kisiasa siyo sheria ya Musa, kama lisu alivyosema, tukimpitisha Samia bila kupingwa then akabadilisha msimamo huoni kuwa tutakuwa tumeliwa?
 
Hana msimamo mmoja huyo! Usishangae kesho akianzisha uzi wenye mawazo tofauti na hiki alicho shauri! Yeye ili mradi aandike aandike chochote tu hapa JF!
 
Uwe unaelewa,

Namaanisha sababu CCM Haina Nia ya kuruhusu KATIBA mpya na TUME HURU ya UCHAGUZI na wanabuy time Ili tuingie ktk uchaguzi na Tume Ile Ile Ili waibe uchaguzi,

Wananchi na CDM tuungane kuhakikisha Tume huru inapatikana, kabla ya Uchaguzi wowote.
 
Sawa,sasa tufanyeje kwani uwezekano wa kupata Katiba Mpya kabla ya 2025 ni mdogo sana karibia ya hapana. Bora kuingia kwenye uchaguzi kwani japo Katiba ni ile ile lakini mazingjra ni rafiki kulinganisha na yale ya 2020, tupate wabunge ili turudishe nguvu yetu iliyoporwa na yule mwovu. Tusipoweka mgombea Urais maana yake tumesalimisha dhamira yetu ya kushika dola,lazima tuanzie mahali,heri nusu ya shari kuliko Shari kamili.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Kwani Chadema wakisimamisha mgombea wa Urais itamzuia nini Samia kutimiza dhamira yake ya kutupatia Katiba Mpya?

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Unaamini tukipambania vya kutosha kuanzia sasa Hadi Dec hatuwezi lazimisha Rasimu ya Warioba kabla haijaitwa KATIBA pendekezwa kurudishwa mezani, na mchakato kuhuishwa na Tume huru ya Warioba kutumika ktk uchaguzi huo?

Mbona unaongea km mtu aliyekata tamaa?

Kwann unaipa nguvu Serikali uwezo wa kukukandamiza na unakubali kushindwa kutetea HAKI?

Au nawe ni mtia Nia ya kugombea ubunge, una homa ya Uchaguzi?
 
Siyo kukata tamaa lakini si vizuri kujilisha upepo,sina nia ya kugombea nafasi yoyote. Ungejuwa shinikizo analopata Rais toka kwa wahafidhina usingefikiria suala la 'kulazimisha' bora twende gradually kuliko kwenda kwa pupa tukakosa yote, CCM hawana cha kupoteza na wameshatokwa na hofu ya Mungu kwao kutumia mabavu ya vyombo vya dola ni jadi yao.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Wanasiasa wawakee "kiasi", Binafsi hata ile reverse-gear aliyoipiga(ga) Mzee wa Msoga kwa PM-Mstaafu na Kamati yake na kwa namna yule "Spika Mstaafu" alivyokuwa laini kwa andiko pendekezwa sikutegemea.

Acha uchaguzi uendelee kama uchaguzi!
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…