Tuzijadili hoja za Rais Kagame kwa kina, je zina maswali na hoja za kimsingi?

Tuzijadili hoja za Rais Kagame kwa kina, je zina maswali na hoja za kimsingi?

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2012
Posts
20,561
Reaction score
24,428
Umoja wa Mataifa, Congo na Rwanda – Paul Kagame auliza maswali magumu

"Tumesikia kuhusu Walinda Amani Umoja wa Mataifa ndani ya Congo una zaidi ya miaka 30 sasa…"

— Paul Kagame...

Rais wa Rwanda anauliza, UN imekuwa Congo kwa miongo mitatu, lakini mgogoro hauishi. Kuna tatizo gani?

Kagame anahoji: Ikiwa UN ilikusudia kuleta suluhu, kwa nini mgogoro bado unaendelea?

Alitarajia miaka 10 ingetosha kuona matokeo chanya, lakini hali inaendelea kuwa mbaya.

Swali lake kuu: UN inafaidika na nini kutokana na uwekezaji wake mkubwa huko Congo?

Kwa nini wanatumia gharama kubwa lakini suluhisho halionekani?..

Kwa mujibu wa Kagame, UN ina wanajeshi zaidi ya 13,500 ndani ya Congo, lakini bado inashindwa kuimarisha usalama.

Ni vipi chombo kikubwa kama UN kinashindwa kupata suluhisho la kudumu?

Kagame anasema UN inaitumia Rwanda kama ngao ya kuficha matatizo yao ndani ya Congo.

Hii inamaanisha nini? Anaashiria kwamba UN inatumia Rwanda kama kisingizio cha kushindwa kwake?

Mgogoro wa Congo una wahusika wengi, ikiwemo serikali ya DRC, makundi ya waasi, UN, na mataifa jirani.

Kagame anadai kuwa badala ya kutatua mgogoro, UN inaonekana kujikita zaidi kwenye uwepo wake wa kudumu huko...

Hili si swali jipya. Wengi wamehoji kama MONUSCO (kikosi cha UN) kweli kina dhamira ya kurejesha amani au ni sehemu ya mtandao wa maslahi ya kisiasa na kiuchumi.

Kagame anasema wazi kuwa Rwanda inalaumiwa mara kwa mara kuhusu hali ya usalama wa Congo, lakini anahoji kama huo ni mkakati wa kuipunguzia UN lawama kwa kushindwa kwake...

Jibu la maswali haya si rahisi, lakini hoja ya Kagame inadhihirisha swali kubwa:

Je, UN iko Congo kwa amani au kuna ajenda nyingine?

Wewe una mtazamo gani kuhusu nafasi ya UN katika mgogoro wa Congo?

Je, hoja za Kagame zina uzito? Tuendelee kujadili.
 
UN na Kagame wote ni maadui wa Uchumi wa Congo. Wote waondoke tu,

Tatizo ni kwamba, kama UN inashindwa, inabidi jeshi la Congo liondoe wote.
Kagame analetaje ubabe kwenye nchi isiyo yake?
Hata kama ametoa hoja za msingi.
 
UN na Kagame wote ni maadui wa Uchumi wa Congo. Wote waondoke tu,

Tatizo ni kwamba, kama UN inashindwa, inabidi jeshi la Congo liondoe wote.
Kagame analetaje ubabe kwenye nchi isiyo yake?
Hata kama ametoa hoja za msingi.
Ipo hivi, baadhi ya wa tuts nyumbani kwao ni goma na kivu na hawana nyumbani kwingine, kibaya watumike na kiongozi wa kabila toka nchi nyingine (Rwanda), ni sawa na raila aingie madarakani halafu aanze kutumia wajaluo wa mara katika kuleta unstable situations, ndani ya Tanzania, huu ni mfano, wa hali ilivyo!
 
Congo n km shamba la bibi tu kilaa mmojaa anayeingia shamba la bibi anajichumia nakujilimia atakacho ....

Nchi ipo km Haina raisi,Haina raiaa ,aina jeshii🤭🤭
 
UN ipo kujinufaisha kwa mgongo wa kulinda amani..hvo hvo Kagame na UN lao moja.. Linapokuja swala la kugawana maslai ndo kila mmoja anamtupia lawama mwenzake..hvo UN+Kagame wanapaswa kuondolewa haraka huko Congo.
 
Endeleeni kujaa kwenye propaganda zake. Siku akija kuongea hivyo kwa mapandikizi yake aliyoyajaza kule Kahama, Geita, Katavi na Kagera ndo mtajua huyu mtu anatakiwa kudhibitiwa haraka sana
 
Kwa kusema la haki wote ni majizi tu na wana maslahi mapana hapo
Huwezi kukuta mahali UN wapo na kukawa na amani
Wanapelekwa kwa wizi tu
Fukuza wote na wabaki wao wenye nchi tuone kama kutakuwa na vita
Vita gani isiyoisha na yeye mwembamba anataka nini huko kama sio gold
 
Endeleeni kujaa kwenye propaganda zake. Siku akija kuongea hivyo kwa mapandikizi yake aliyoyajaza kule Kahama, Geita, Katavi na Kagera ndo mtajua huyu mtu anatakiwa kudhibitiwa haraka sana
Acha uoga wa kifala, kinachofanyika DRC hakiwezi kufanyika TZ. Sisi ni nchi yenye institutions zilizosimama, huo uoga wa kichoko unasambazwa na Wacongo walioko TZ ili kutusakizia tuwasaidie wakati wao wenyewe hawafanyi jitihada zozote kujisaidia.
Vita ni tofauti na kucheza sebene.
 
UN na yeyote aliye kongo kwa lengo la kuleta amani waondoke,bora Tanzania ikabidhiwe hilo jukumu,
Na sijui raisi wao anawaza nini maana kutatua huu mgogoro ni jambo ambalo liko ndani ya uwezo wake,
Kama ilivyosemekana inawezekana ni moja kati ya wachochezi wa vurugu hizo,
UN WAONDOLEWE HARAKA
 
Endeleeni kujaa kwenye propaganda zake. Siku akija kuongea hivyo kwa mapandikizi yake aliyoyajaza kule Kahama, Geita, Katavi na Kagera ndo mtajua huyu mtu anatakiwa kudhibitiwa haraka sana
Yani yeye ndo atajaa kwenye mfumo wetu alafu atachuchumaa anye tumfute na gunzi la moto
 
JAMBO LA KUSTAAJABISHA SANA NI KWAMBA, RWANDA ANADAI YEYE HAHUSIKI, NA KWAMBA HAO NI WATUTS WA KONGO, MAAJABU NI KWAMBA, IWAJE YEYE AWE NA MAMLAKA YA KUVISIMAMISHA VITA HIVYO WAKATI WOWOTE TENA KWA KAULI TU, / HAPA NDIPO ANAPOJICHANGA YEYE BINAFSI, NA HAPA NDIPO MATAIFA YANAPOTAMBUA UHUSIKA WAKE
 
Back
Top Bottom