Tuzungumzie alichofanya Ramos kwa Salah

Tuzungumzie alichofanya Ramos kwa Salah

Mkuu Sisi mashabiki tunaendaga uwanjani kuangalia burudani. Hatuendi kuangalia mieleka pale.
Beki ukipitwa na forward tunasubiri tuone uhodari wa kipa langoni.
Sasa we ukipitwa unapiga mieleka.

Ile sio football hata kdg.
Am telling you that.
Mechi mhimu kama ile sio ya kumlalamikia ramos hata kidogo mkuu.
 
Mechi mhimu kama ile sio ya kumlalamikia ramos hata kidogo mkuu.
Hamna anayemlalamikia Ramos. Hapa tunaongeaga ukweli Tu.
Mechi ya Jana watu wameenda kuangalia burudani itakayotolewa na wachezaji wote 22 Kwa kila upande.
Sasa we kumuumiza mchezaji mwingine Kwa makusudi unategemea nini.

Ndio mana unaona watu wanampa lawama hasa yeye Kwa kuwa mechi ya Jana ilikuwa ina uzito wake zaidi.

Mbona akimchezeaga rafu Messi huwa inapotezewa Tu kawaida.

Kumkosa Mo Jana kuna kitu kilipungua.
Yule ni mchezaji wa muhimu Sana.

Tuache ushabiki wa kimaandazi.
Elewa alichokifanya Ramos sio cha kiungwana.
Umeona Nani ameunga mkono Kwa aliyoyafanya.
 
Hivi mngepata kadi nyekundu hii mechi si mngeua mtu??
11 vs 11, mnatoka povu la hatari. Hii ndio maana mimi nilitaka liver wafungwe maana mnajifanya mnajua sana kuongea, katoka Mo Salah kwa faulu ya kawaida tu ila bahati mbaya timu nzima imeshindwa cheza sababu ya kutegemea mtu mmoja, sasa mnatafuta mchawi!
Na mpigwe tu, msimu wa tatu huu kwa Klopp akiwa Liver, kwa gundu na midomo ya mashabiki wa liver, ataendelea kuchukua ubingwa wa gengen pressing tu.
Umemeza debe la Omo,ninachojua hata Madrid wenyewe hawajafurahia huu ubingwa,una doa.
 
Yaani Salah kageuzwa kisingizio cha kushindwa Liverpool ha haa haaaa, maana kila "mpinzani" wa Madrid ukimgusa tu, Salah, sijui Ramos mhuni, blah blah kibao. Ila inasaidia kupunguza maumivu. Poleni sana wote ambao hamkutaka Madrid ashinde. Hongereni Madrista wote.
 
Umemeza debe la Omo,ninachojua hata Madrid wenyewe hawajafurahia huu ubingwa,una doa.
Endelea kujipa moyo, ndoo ya 13 na imewekwa kwenye historia. Mo Salah ni nani kwa Madrid wasifurahie ubingwa wa jasho lao?? Aliumizwa CR7 europe cup na maisha yakaendelea, alipewa kadi nyekundu BECKHAM wa Uingereza kombe la dunia na maisha yakaendelea sembuse Mo Salah huyu ambaye bado hajashinda hata kombe moja??

Povu anatoa aliyeumizwa na kipigo cha jana sio mimi, mimi nimefurahishwa na Liver kuukalia.

Angalia hii kitu hapa kisha uendelee kujipa moyo kuwa Madrid hawajasherehekea.


Endelea kujipa moyo!



Hii video clip ya chini NAWAKUMBUSHA MACHUNGU YA JANA, tutasiriba chumvi kwenye hivyo kidonda mpaka kipone sasa.
 
Kama kuna jambo lililoumiza wapenzi wa mpira wasio washabiki wa mpira, ni kitendo cha Ramos kufanya niseme dirty game au faulo mbaya ambayo alimfanyia Mo Salah

Binafsi pia nilijiskia vibaya, ila sasa tuzungumzie kwamba wengine wanasema bahati mbaya, wengine wanasema alidhamiria na wengine wanasema ilikua ni game plan baada ya kuona wanashambuliwa kwa dakika nyingi za mwanzoni kabla ya yeye kuumizwa na kutoka.

Sasa kwa taarifa zilizopo ni kwamba ameumia sana kwenye mifupa ya bega na huenda akakosa michuano ya kombe la dunia,

Tukiacha ushabiki, hivi ile haikua makusudi kweli? Kwanini aliung'ang'ania mkono hadi kwenda chini. ?

Huko kwenye akaunti yake ya instagram anatukanwa sana ila jamaa anachekelea tu, nafikiri angetumia fursa hii kutoa neno la kuomba radhi, ila wanasema hii sio mara ya kwanza kufanya hivyo kwa wachezaji hasa katika mechi za fainali.
KWa aliyewahi kucheza mpira hawezi kushangaa lile tukio hata kidogo. Kazi ya beki ni kufanya kila awezalo kupunguza nguvu ya washindani wao. Na kazi ya foward ni kufanya kila awezalo kupata bao, iwe kwa kujirusha au hata kusababisha kupigwa. Lengo ni BAO.
Kutengeneza frastration ni moja ya burudani pia. Unakumbuka yule wa simba alitemewa mate? Unajua kwa nini? Inawezekana alimpima oil mshikaji kimtindo, refa hakuona. Kwa hasira akampa kohozi la uso. Akala nyekundu, simba wakapeta.
Unakumbuka Zizou alivyofanywa na Materaz kwenye ile fainali kati ya ufaransa na Italy? Alitukanwa, akaghadhika akampa jamaa ''ndoo'', akala red. Italy wakachukua ubingwa huku france wakiwa pungufu. Hiyo ndio fabo mzee, ni kawaida sana ile.
 
Hamna anayemlalamikia Ramos. Hapa tunaongeaga ukweli Tu.
Mechi ya Jana watu wameenda kuangalia burudani itakayotolewa na wachezaji wote 22 Kwa kila upande.
Sasa we kumuumiza mchezaji mwingine Kwa makusudi unategemea nini.

Ndio mana unaona watu wanampa lawama hasa yeye Kwa kuwa mechi ya Jana ilikuwa ina uzito wake zaidi.

Mbona akimchezeaga rafu Messi huwa inapotezewa Tu kawaida.

Kumkosa Mo Jana kuna kitu kilipungua.
Yule ni mchezaji wa muhimu Sana.

Tuache ushabiki wa kimaandazi.
Elewa alichokifanya Ramos sio cha kiungwana.
Umeona Nani ameunga mkono Kwa aliyoyafanya.
Mkuu tuyaache hayo weather jamaa hakufanya fair au laa.

Ubingwa nani kachukua?
 
Kama kuna jambo lililoumiza wapenzi wa mpira wasio washabiki wa mpira, ni kitendo cha Ramos kufanya niseme dirty game au faulo mbaya ambayo alimfanyia Mo Salah

Binafsi pia nilijiskia vibaya, ila sasa tuzungumzie kwamba wengine wanasema bahati mbaya, wengine wanasema alidhamiria na wengine wanasema ilikua ni game plan baada ya kuona wanashambuliwa kwa dakika nyingi za mwanzoni kabla ya yeye kuumizwa na kutoka.

Sasa kwa taarifa zilizopo ni kwamba ameumia sana kwenye mifupa ya bega na huenda akakosa michuano ya kombe la dunia,

Tukiacha ushabiki, hivi ile haikua makusudi kweli? Kwanini aliung'ang'ania mkono hadi kwenda chini. ?

Huko kwenye akaunti yake ya instagram anatukanwa sana ila jamaa anachekelea tu, nafikiri angetumia fursa hii kutoa neno la kuomba radhi, ila wanasema hii sio mara ya kwanza kufanya hivyo kwa wachezaji hasa katika mechi za fainali.
Wewe ni shabiki mkuu, mpira unaujua kwa kuangalia kwenye Tv.
 
😀😀😀😀😀😀😀...watu Madrid City huko wanakula pilau la ushindi wewe unajipa tumaini hapa. Mm mmoja wao nafurahia sana na hakuna doa. Ramos, super captain "mutu mbaya" imetumwa kazi naimeifanya kazi.
Wakipenda wamuite Sergio Ramos JAMBAZI. Jamaa ni super captain.
 
Kudadadeq, Ramos unalaaniwe popote uliko, Huwezi kumfanyia Mwafrika mwenzetu kitu kama hii... AlaH...!!
FB_IMG_15274153750901923.jpg
 
Ronaldo akiwa na off day mchezoni kuna mashine zingine zafanya kazi.
Hapa sioni haja ya kumlaumu Karius kwa kushindwa zuia michomo ya Bale, jamaa ni kama HULK.
20180527_184039.png
 
Hamna anayemlalamikia Ramos. Hapa tunaongeaga ukweli Tu.
Mechi ya Jana watu wameenda kuangalia burudani itakayotolewa na wachezaji wote 22 Kwa kila upande.
Sasa we kumuumiza mchezaji mwingine Kwa makusudi unategemea nini.

Ndio mana unaona watu wanampa lawama hasa yeye Kwa kuwa mechi ya Jana ilikuwa ina uzito wake zaidi.

Mbona akimchezeaga rafu Messi huwa inapotezewa Tu kawaida.

Kumkosa Mo Jana kuna kitu kilipungua.
Yule ni mchezaji wa muhimu Sana.

Tuache ushabiki wa kimaandazi.
Elewa alichokifanya Ramos sio cha kiungwana.
Umeona Nani ameunga mkono Kwa aliyoyafanya.
mkuu humu kuna ushabiki maandazi bora tujikalie kimya tunaambiwa hatujui mpira wao ndo wanajua mpira na sheria 17 za soka.
tena lait angefanya jambo ambalo lingepelekea mchezaji kupoteza maisha basi zingeandikwa rip nyingi sana na wao wangeandika kwamba walimpenda sana ila bado wangesifia ujembe wa aliyefanya
hawababaishi hawa ndugu kwenye maeneo ya kujidai kama samaki samaki na vibanda umiza hua tunakaa nao sana tunawajua mashabik maandazi tena utamjua kwa kua mropokaji ovyo tu muda wote na anachoongea hakina mantiki, wenye kuujua mpira unakuta tumetulia na wine zetu barrridi tunawaangalia tu na kucheka.
 
Ulipotoa maelezo ulikua unatakaje!?
yani nauliza ulitaka niandike nini maana nilichoandika mimi wewe umesema nimeandika pumba sijui ujinga ndo nakuuliza ulitakaje sasa??

ngoja nikuambie kitu mkuu, mpira ni kama vile vitabu tunavyosoma darasani kama Ngoswe, Takadini, Three Suitors One Husband, Pass Like A Shadow and all stuffs like that na siku ya mtihani kila mtu atakuwa na jibu lake tho kitabu mlisoma pamoja.

same to mpira wote tumeangalia kwa pamoja tukio tumeangalia kwa pamoja mimi nimeona nilichopresent hapa wewe pia umeona ulichoona tho hujakiwakilisha.

ubaya zaidi unataka kunilazimisha kile unachoamini wewe na mimi niamini hicho hicho na hapo ndio unapokosea.

NARUDIA TENA FOOTBALL IT'S ALL ABOUT PHYSICAL CONTACT

uje na hoja usije kama mlevi unakosoa bila kuja na hoja....hoja upingwa kwa hoja.

Get Well Soon Salah
 
Back
Top Bottom