Tuzungumzie matatizo ya figo

Tuzungumzie matatizo ya figo

Tule na tunywe nini na tusile na tusinywe nini?

Veggies na fruits, kadhalika kunywa maji ya kutosha kila siku na punguza au acha kabisa processed foods na kemikali zingine. Pia fanya mazoezi, nimewahi kuweka uzi kuhusu mazoezi unaweza kuupitia hapa chini na ukiweza soma comments:

Fitness and wellness - JamiiForums
 
Vipi matumizi yaliyokithiri ya madawa, hayachangii matatizo ya figo? Kuna wale watumiaji wa madawa kama ya pressure (assomex, nk), wapo watumiaji wa ARV, hawa huwa lazima kila siku wameze kidonge kimoja.

Wapo kwenye hatari kiasi gani kupata/kuepuka matatizo ya kufeli figo? Pia ukiwa na matatizo ya ini ni rahisi sana kupata matatizo ya figo. INI, MOYO na FIGO ni viungo vinavyofanya kazi kwa "kupendana", kimoja kikishindwa basi vingine vinapata shida sana ku-cope, hence matatizo yanaongezeka.

😷😷😷
 
75% ya choo kikubwa ni maji. Kuepuka kujikamua na choo kigumu kunywa maji.
Asante kwa ushauri nina mtoto WA mwaka na nusu Kuna siku alikuwa Ana push aja ikawainagoma alilia Sana nikasononeka sikuwai na jinsi ya kumsahidia.. Nafkiri alipewa vyakula vigumu na maji akuwa nayo ya kuyosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwili unajiregulate wenyewe lakini ukishafika 50+ inabidi uwe muangalifu. Wengi katika umri huu hasa kama uliutendea rough ujana
baadhi ya vitu vinahitaji MOT
.

Mupunguza chumvi
Nyama nyejundu
Pombe

Kuongeza mboga matunda na maji.

Medical checkups once a year.
Mkuu hiyo nyama nyejundu mi ndo siijui kabisa nipe mwongozo pls

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunashukuru kwa Taarifa nzuri,

Ushauri wangu kwa wanajamii

1.Tupunguze sana kula chumvi hasa ya kuongeza mezani kwenye chakula.
2.Tunywe angalau lita 2 na nusu za maji kila siku
3.Tupunguze sana kunywa vinywaji vyenye sukari nyingi hasa Soda na Juice ,vilevile vyakula vya wanga tule kiasi kidogo
4.Tufanye mazoezi mara kwa mara angalau nusu saa kwa siku 4 kila wiki
5.Tusitumie madawa ya kienyeji na kunywa ,haya hayana vipimo vinavyotambulika na mara nyingi huathiri figo zetu
6.Madawa ya Antibiotics na Madawa Ya kupunguza maumivu yatumiwe kwa kibali maalum cha Daktari na sio kununua mwenyewe na kuyabugia.
7.Tujaribu kucheki afya ya mwili mara kwa mara angalau mara 3 kwa mwaka ,hii itasaidia kujua tatizo la mwili kabla halijakuwa serious,tusisubiri kuumwa na ndipo tutafuta hospital ipo wapi.
8. Tusiache mwili mpaka tukawa na uzito usiostahili (Normal BMI)
9 .Tupunguze unywaji wa pombe nyingi na uvutaji wa sigara
Kwa hayo yote hapo juu kwa kiasi kikubwa tutalinda figo zetu
 
Matatizo ya Figo yanatokana Na complications ya organ nyingine ama mfumo wa maisha (Life Styles)

Hizi zinaweza kuwa sababu kuu au vichocheo vya matatizo ya Figo.


1.Uncontrolled high blood pressure (Hypertension). Hii ni pressure ya kupanda , mtu asipotibiwa mapema mwisho wa siku hupelekea tatizo la Figo. Ni vizuri kuepuka vyanzo vinavyopelekea presha.


2. Ugonjwa wa Kisukari (Diabetes)


3.Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kutuliza maumivu , Dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI (ARVS).Hapa ndio maana waathirika wa HIV hupimwa Figo Na Ini zao mara Kwa mara ili kuangalia utendaji kazi wake maana dawa za ARVs zina madhara Kwa hizo organ , kama wataona hazipo vizuri mgonjwa hupunguziwa dozi.

4.Matumizi ya vilevi vikali , beer Kwa muda mrefu . Pombe zinachosha Figo zako , tumia Kwa kiasi.

Matatizo ya Figo , Moyo Na Ini yanaendana Na ukipata mojawapo basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata lingine maana hizi organ zinafanya kazi Kwa kushirikiana



Sent from my Iphone using Tapatalk
 
Mleta Maada ameingia Mitini

Sent from my GT-N7000 using Tapatalk
 
Vipi matumizi yaliyokithiri ya madawa, hayachangii matatizo ya figo? Kuna wale watumiaji wa madawa kama ya pressure (assomex, nk), wapo watumiaji wa ARV, hawa huwa lazima kila siku wameze kidonge kimoja.

Wapo kwenye hatari kiasi gani kupata/kuepuka matatizo ya kufeli figo? Pia ukiwa na matatizo ya ini ni rahisi sana kupata matatizo ya figo. INI, MOYO na FIGO ni viungo vinavyofanya kazi kwa "kupendana", kimoja kikishindwa basi vingine vinapata shida sana ku-cope, hence matatizo yanaongezeka.
Kwa ARV kila mgonjwa akienda clinic anafanyiwa check up ikiwemo kidney function. Kama kuna madhara anabadilishiwa dawa Hii ni kwa magonjwa yote ya long term.
 
Mi nahisi kamaanisha zile dagaa ambazo huwa na mchanga pamoja na mawe mara nyingi ili mtu uzipike inabidi utoe vichwa na uoshe na maji moto
labda ndio maana kasema dagaa za shuleni.
maana mtaani huwa tunazitengeneza katika umaridadi na uzingativu wote.
 
Watu wengi huepuka usumbufu wa kuamka usiku lakini saa bora kabisa ya kunywa maji ni kupata glass kabla hujaingia kitandani. Wakati mwili ume pumzika maji haya yata kusaidia kuweka sawa mapigo ya moyo na usafirishaji wa damu.

Utaamka ukojoe na wanaofanya hivi hupata choo kikubwa mara tu wanapoamka asubuhi.

View attachment 1037338
Let me start doing this,huwa nakunywa maji mengi sana ninapoamka asubuhi,ila hii glass ya usiku huwa ninaikwepa kwa kuogopa kuamka usiku..
 
Kwa ARV kila mgonjwa akienda clinic anafanyiwa check up ikiwemo kidney function. Kama kuna madhara anabadilishiwa dawa Hii ni kwa magonjwa yote ya long term.
Lakini tukubali tu kuwa ina a long run lazima zile dawa zitakuwa na madhara kwa mtumiaji tu. Mbona sasa watu wengi wanaotumia ARVs wanapata shida ya kidney failure? Na Kwa nini hypertension inasababisha kidney failure?
 
Watu wengi huepuka usumbufu wa kuamka usiku lakini saa bora kabisa ya kunywa maji ni kupata glass kabla hujaingia kitandani. Wakati mwili ume pumzika maji haya yata kusaidia kuweka sawa mapigo ya moyo na usafirishaji wa damu.

Utaamka ukojoe na wanaofanya hivi hupata choo kikubwa mara tu wanapoamka asubuhi.

View attachment 1037338
Kawaida yangu kunywa maji mengi usiku
 
Lakini tukubali tu kuwa ina a long run lazima zile dawa zitakuwa na madhara kwa mtumiaji tu. Mbona sasa watu wengi wanaotumia ARVs wanapata shida ya kidney failure? Na Kwa nini hypertension inasababisha kidney failure?
Mara nyingi ukianza kupata matatizo option ni dawa bora ambazo ni ghali hii hutegemea status na sehemu ulipo. Kama uko nchi za Scandinavia huko serikali inagharamia hata zikigharimu US$3,000 kwa mwezi.
 
Back
Top Bottom