Twiga Stars VS Bafana Bafana

1-1 HT bado

Du, broda, ulivyoandika mtu wa hobby ya tofauti na mpira hatakaa akuelewe!
Nadhani unamaanisha goli 1 kwa1, na Half-Time bado!
Asante kwa taarifa, kazi na dawa!
 
wabongo wanausakata ile mbaya, dakika ya 70 bado 1-1
 
jamani msinipasue moyo... uchaguzi unatosha, dk sabini tayari?
 
mh ila muda huu timu yetu imezidiwa kidogo naona kiungo hakipandishi mashambulizi
 
sasa timu yetu ni butuabutua nahisi wanahitaji kutulizana, wasipaniki, tukipata droo kwenye mechi hii itakuwa safi sana kwetu
 
Naona ester chabruma kachokaa, pia mchezaji mwanahamisi shurua anapewa kadi nyekundu kwa second yellow anadaiwa ali-dive
 
Mpira umeisha ijapo bado kidogo tufluke kupata goli

final score banyanabanyana 2-twiga stars 1

timu zingine kwenye kundi ni nigeria na mali, kwa hiyo kazi ipo sana

nasikia wachezaji wa twiga wanalalamika wewe nini bwana? Sijui wanamwambia nani
 
Mpira umeisha ijapo bado kidogo tufluke kupata goli

final score banyanabanyana 2-twiga stars 1

timu zingine kwenye kundi ni nigeria na mali, kwa hiyo kazi ipo sana

nasikia wachezaji wa twiga wanalalamika wewe nini bwana? Sijui wanamwambia nani

ok, thanx for update...
 
MKwasa anahojiwa anawapongeza wachezaji wake, ila analalamikia ua muzi haukuwa mzuri, anadai ile red card haikuwa sahihi badala yake sisi tulistahili kupata penati

anawaheshimu mali na nigeria kwamba wana timu nzuri ina ana uhakika watashinda mechi zijazo
 
Dada zetu wanaujua mpira na wamecheza kwa malengo haswa! sikutegemea kiwango kile.. Banyana wameshinda kwa taabu pamoja na wachezaji wao wenye utata kama wawili hivi wamekaa kidume dume hivi:smile-big:
 
Twiga Stars wamecheza vizuri sana. Viwango ni vizuri...style yao ya mashambulizi ya kushtukiza ni tamu mno. Kama refa asingewakatisha tamaa na mafilimbi yake ya offside...sasa hivi tungekuwa tunaimba akanana, na kucheza kiduku.
Tatizo kubwa nililoliona katika dakika kumi za mwisho ni kupoteza muda kana kwamba wanatafuta droo hivi. Hii ilipelekea mashambulizi mengi langoni mwao.

Twiga wanatakiwa wajue kwamba, Tanzania kwa kufika pale hatuna cha kupoteza. Wacheze mpira wao, na nina uhakika wanaweza wakafanya vizuri katika mechi zijazo.

Hongera dada zetu.
 
si mbaya kivile ila wakaze but waache tabia ka za kaka zao
hawawezi kulinda magoli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…