Twist in Sh660m Fastjet-Fly540 wrangle as licence is withdrawn

Twist in Sh660m Fastjet-Fly540 wrangle as licence is withdrawn

Abiria wanaotumia ndege za shirika la ndege maarufu kama Fast Jet zenye bei nafuu kuliko ndege zote nchini, huenda wakakosa huduma hiyo kutokana na shirika hilo kuwa hatarini kufungwa kutokana na kukiuka mkataba uliokuwepo kati yake na Fly540 Aviation Ltd. Sakata hilo limekuja baada ya kampuni ya Fly540 kutangaza kuondoa leseni yake iliyotoa kwa FastJet ili kuendesha shughuli za usafirishaji ktk anga la Tanzania, Angola, Kenya na Ghana.

Kuondolewa kwa leseni hiyo kunamaanisha kuwa FastJet sasa itapaswa kisheria kusimama kutumia alama au chapa zote za Fly540 Ltd, kampuni ambayo inasemekana iliuza hisa kwa mkataba ambao FastJet wameukiuka.

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga, Fadhili Manonga, amethibitisha kupokea barua toka kwa makampuni yote mawili yaliyowekeana pingamizi za kisheria, huku Fly540 ikiitaka FastJet kuacha kutumia alama na chapa zake katika shughuli zake hapa nchini.

Source Tanzania Daima la Feb.08, 2013

ile ofisi pale samora pembeni ya steers ina nuksi kila co ya ndege inayopitia pale aidumu.hahahahaha community airline,540,fastjet na kabla ya hapo kuna nyingine nyingi zilipita hapo.poleni wazee wa 32,000.vya raisi huwa havidumu
 
Ah wapi! Fastjet wanaendelea kama kawaida. Chanzo cha hizo habari ni bwana 540 mwenyewe (Don Smith) kutaka kutumia media ili apate dongo nono baada ya kununuliwa. Fasject wapo na hivi karibuni wataongeza route.
 
yani kila Mtanzania mlalahoi anapoanza kuona unafuu mahali basi haikiwii kutoweka. Kuna watu wameletwa duniani kuhakikisha wenzao hawapumui
 
Ah wapi! Fastjet wanaendelea kama kawaida. Chanzo cha hizo habari ni bwana 540 mwenyewe (Don Smith) kutaka kutumia media ili apate dongo nono baada ya kununuliwa. Fasject wapo na hivi karibuni wataongeza route.

kwa hiyo unataka kutuambia kwamba Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga Fadhili Manonga nae anatudanganya???
 
Abiria wanaotumia ndege za shirika la ndege maarufu kama Fast Jet zenye bei nafuu kuliko ndege zote nchini, huenda wakakosa huduma hiyo kutokana na shirika hilo kuwa hatarini kufungwa kutokana na kukiuka mkataba uliokuwepo kati yake na Fly540 Aviation Ltd. Sakata hilo limekuja baada ya kampuni ya Fly540 kutangaza kuondoa leseni yake iliyotoa kwa FastJet ili kuendesha shughuli za usafirishaji ktk anga la Tanzania, Angola, Kenya na Ghana.

Kuondolewa kwa leseni hiyo kunamaanisha kuwa FastJet sasa itapaswa kisheria kusimama kutumia alama au chapa zote za Fly540 Ltd, kampuni ambayo inasemekana iliuza hisa kwa mkataba ambao FastJet wameukiuka.

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga, Fadhili Manonga, amethibitisha kupokea barua toka kwa makampuni yote mawili yaliyowekeana pingamizi za kisheria, huku Fly540 ikiitaka FastJet kuacha kutumia alama na chapa zake katika shughuli zake hapa nchini.

Source Tanzania Daima la Feb.08, 2013

hata community airline ilianza kwa makeke kama ya fastjet wakuu
 
ile ofisi pale samora pembeni ya steers ina nuksi kila co ya ndege inayopitia pale aidumu.hahahahaha community airline,540,fastjet na kabla ya hapo kuna nyingine nyingi zilipita hapo.poleni wazee wa 32,000.vya raisi huwa havidumu
huwezi ukawa unatoa huduma chini ya bei ya wastani ya soko utegemee kudumu mkuu
 
kwa hiyo unataka kutuambia kwamba Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga Fadhili Manonga nae anatudanganya???

Fastjet walitoa statement na wanasema bwana 540 hana mamlaka kisheria kuzuia kitu maana alishapewa chake!
 
Hii habari ingenihusu zaidi kama ingezungumzia daladala.
 
Fastjet walitoa statement na wanasema bwana 540 hana mamlaka kisheria kuzuia kitu maana alishapewa chake!

Taarifa inajieleza kwamba kuna mkataba ambao waliwekeana ili kuuziana share. Mmojawapo wa parties ktk mkataba akikiuka au kwenda kinyume na contract basi upande wapili unaruhusiwa kisheria kusitisha/kuvunja huo mkataba. Atakeamua kwamba hakuna alieenda kinyume na contract ni mahakama, na sio boss wa FastJet.
 
Serikali ya ccm haipendi kabisa kuona wananchi wa kawaida mnapanda ndege! Haipendi yani mfanane na wao! Haiwezekani, naamini tungekuwa na serikali ''INAYOJALI WANANCHI'' wangewapa hata mkataba wa muda! Lakini ni ngumu kwa mlala hoi wa nchi hii kupata nafuu hata ya usafiri mkiwa chini ya ccm.
 
Mbona hizi Habari zimekanushwa na Manager wao jana...
 
mhhh sasa haka ticket kangu ntawah kukatumia kweli? yalaaaaaaa usafiri wetu
 
Ah wapi! Fastjet wanaendelea kama kawaida. Chanzo cha hizo habari ni bwana 540 mwenyewe (Don Smith) kutaka kutumia media ili apate dongo nono baada ya kununuliwa. Fasject wapo na hivi karibuni wataongeza route.
Umeona eeh? Fly 540 ndio wameeneza huo upuuzi kwa waandishi wa habari walionunuliwa. TCAA hawajasema lolote kuhusu kufunga license ya Fastjet, mgogoro unakuzwa na 540. Fastjet is there to stay!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
kweli narudi tena kwa MOHAMED na NAJMNISA mwanza -dar? kha!!!!!!!:target::target::target:
 
Back
Top Bottom