UAE how dare you?

jMali

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2010
Posts
8,404
Reaction score
4,973
Hivi hawa waarabu hawajui kuwa wanyarwanda (hasa watutsi) ni watu wenye akili kubwa kuliko wote huku Africa? Hawajui wanyarwanda ni wayahudi weusi waliopotea njia kutokea Israeli? Sasa inakuwaje wanabania VISA wanyarwanda halafu manchi ya ajabu ajabu kama Tanzania yanapeta? Yaani Super Power Rwanda ni ya kufananishwa na Burundi na Togo?

Hawajui Rwanda chini ya genius Paul Kagame ni namba moja kwa teknolojia Africa nzima? Hawajui huku Rwanda hakuna mgao wa umeme wala maji? Intaneti ni bure, barabara zetu zote lami! Hawajui Rwanda usalama ni kama huko Dubai tu watu wanalala milango wazi? Hawajui kuwa Rwanda ina viwanda vya magari na smartphone na hivyo ajira huku zipo nje nje? Hawajui kuwa Rwanda inakaribia kurusha satellite yake yenyewe?

Yaani kweli wanadai kuwa watutsi wanakwenda UAE kudangadanga mpaka wanaoverstay na kugeuka wahamiaji haramu? Yaani wanamaanisha kuwa Rwanda ni nchi ya njaa kama Sudan? Haya maendeleo yote hawayaoni au wanawaoneawivu?

Nisaidieni jamani maswali ni mengi.
 
Rwanda bado watu hawajastaarabika, ni nchi ambayo wasipokuwa makini watarudi kuuana.

Kwenye visa za Dubai pale chini wanaandika, "kaa ndani ya Dubai kwa muda ulioruhusiwa ili wakati mwingine tukukaribishe tena"
 
Unaeza nitajia gari za rwanda zilizoko bongo au una semea viwonder vya magari rwanda
 
Hivi wee jamaa jMali si ulifungiwaga (kama siyo kufaga) wewe. Sasa sijui umetokea wapi!!?
CC: Moderator kumekucha huku, zile post za ubaguzi zimerejea kwa kasi ya 5G.
Watu kama nyie ndio mnaonifanya nisitumie JF siku hizi kwa sababu mnaondoa ile dhana ya “The Home of Great Thinkers”.
  1. Sijawahi kufungiwa account tokea nijiunge JF, kama unaweza kuthibitisha hilo karibu!
  2. Fafanua ni kivipi hii thread ni ya kibaguzi ili mods waifunge.
Ukishindwa hayo mawili wewe hufai kuwa great thinker endelea huko instagram!
 
Hivi hawa waarabu hawajui kuwa wanyarwanda (hasa watutsi) ni watu wenye akili kubwa kuliko wote huku Africa? Hawajui wanyarwanda ni wayahudi weusi waliopotea njia kutokea Israeli? Sasa inakuwaje wanabania VISA wanyarwanda

Ubaguzi ni huu hapo ni bold text. Unaongea vitu vizito with confidence wakati wala huna justification hata moja.
Nikikuomba taarifa ya utafiti kuthibisha yafuatayo:
1. wanyarwanda (hasa watutsi) ni watu wenye akili kubwa kuliko wote huku Africa.
2. wanyarwanda ni wayahudi weusi waliopotea njia kutokea Israeli.

Unaweza ukawasilisha hapa JF.
 

Shambulia hoja na si mtoa hoja.
 
Kwanza alivyoandika (hasa watutsi).
Ubaguzi wa kikatili sana ukitegemea genocide iliyotokea hapo Rwanda kwa sababu ya ukabila.
 
Sasa huo ni ubaguzi (racism) au assertions (unverified as they are)? Hapo wanyarwanda wamebaguliwa au wamesifiwa ? karibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…