uahauri

Joined
May 9, 2013
Posts
12
Reaction score
0
naombeni ushauri..
mimi nilimaliza kidato cha nne 2010 na nilifanikiwa kupata history- C na civics-C ...mwaka Jana nilirudia(2012)
nikapata geography-C na kiswahili-B
je naweza kwenda government schools??
Na suala lingine mimi nataka kuchukua combination ya HGK je badae itanihusisha na taaluma gani???
naombeni ushauri wenu.!
 
Ukishafanya mtihani kama private candidates hauwezi kupata nafasi ya kusoma serikalini hata kama utapata div one ya point saba. kwa sasa jipange kwenda kusoma private.

Kwa mchepuo unaousoma unaweza kuwa na taaluma nyingi tu kikubwa ni wewe kuamua ukasomee taaluma gani utakapomaliza kidato cha sita ikiwa utafaulu vizuri. kiwango chako cha ufaulu ndio kitakupa uwanja mpana wa kuchagua taaluma nyingi.
 
Mkuu hongera kwa ufahulu mzuri, govt huwezi kupata ila tafuta shule ya private upige msuri. Ushaur soma HGE itakupa uwanda mpana wa kuchagua kozi ya kusoma chuo.
 
Hapo ni private tu kjana hakuna kula ugali wa serikal.We kakomae private hiyo comb utatoka2
 
Tafuta shule ya serikali..kaombe usome lakini mtihani utafanya private..ila hii itakusaidia zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…