mnyongeni
Senior Member
- Dec 6, 2011
- 141
- 24
Habari wana jf, labda nitoe tu historia kwa ufupi... mimi ni mmoja wa wahitimu wa chuo kikuu mwaka juzi (2011),na kada niliyoisomea ni ya ualimu. ( kwa sasa ni mwalimu), mnamo mwaka 2008 nilipomaliza form six, nilipo omba vyuo nilipata kuchaguliwa vyuo viwili yaani kozi ya ualimu na mass communication.na nilichaguliwa elimu kwani aliyekuwa ananielekeza kujaza form aliniambia niweke education kama first choice, sikuwa na jinsi kwani uelewa ulikuwa ni mdogo wa nini nifuate...... Malengo yangu yalikuwa natamani sana kusomea video shooting and editing (kwani nilitamani sana kuwa mtengeneza movie na music video). ila nilijikuta nakosa elimu ya maelekezo ya ni jinsi gani nitaweza kufikia ndoto yangu., Nilipo washirikisha wazazi walikataa kata kata mimi kusoma mass communication kwani waliponda sana wakisema uandishi wa habari hauna dili ( sana sana baba, kwani yeye by that time alikuwa ni afisa elimu vifaa na takwimu (SLO)) sikuwa na jinsi kwani nilipoendelea kubisha baba alitaka kunizira kuwa nilienda mass communication nikikwama nisimuhusishe kwani aliamini naweza kosa mkopo, na education mkopo ulikuwa ni wa kufikia. siyo siri nilienda chuo kishingo upande, mwaka wa kwanza karibia wote nilikuwa ni wa kulalamika tu, second year nikaaza kurecover. nikamaliza 2011, mwaka 2012, nikaajiriwa wilaya moja hapa tz, kama walimu wa o level kwenye shule moja ya kata. kiukweli nafundisha ndiyo ila moyo wangu na mapenzi hayako kwenye ualimu kabisa.... pia maslahi madogo... mshahara wenyewe full makato, na ukipata mshahara inabidi usubiri mpaka mwisho wa mwezi ndo uione hela nyingine... kiuhalisia nafikiria kuachana na ualimu naomba nisaidiwe yafuatayo
1. nikitaka kurudia ndoto zangu ni chuo gani ntaweza kusomea fani ya video shooting & editing niwe professional wa movie?
2. ni fani gani nyingine at least inalipa kwa mtu wa combination ya HKL?
ntashukuru endapo nitapata ushirikiano wa dhati.
1. nikitaka kurudia ndoto zangu ni chuo gani ntaweza kusomea fani ya video shooting & editing niwe professional wa movie?
2. ni fani gani nyingine at least inalipa kwa mtu wa combination ya HKL?
ntashukuru endapo nitapata ushirikiano wa dhati.