Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 577
- 2,595
Ugonjwa wa Polio husababishwa na virusi vya Polio, ambavyo huenezwa kwa njia ya kula na kunywa maji yaliyochafuliwa na kinyesi chenye vimelea vya ugonjwa.
Ugonjwa huu unaweza kuwapata watu wa rika zote lakini watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 ndiyo wanaoathirika zaidi.
Hushambulia mishipa ya fahamu hatimaye husababisha kupooza kwa misuli, hasa ya miguu, mikono au yote kwa pamoja, na pengine misuli ya kiwambo (diaphragm) na kusababisha kifo.
Njia sahihi ya kujikinga na ugonjwa huu ni kupitia chanjo (OPV) ambayo hutolewa kwa watoto kwa njia ya matone ya kumeza mara nne kwa utaratibu ufuatao-
Chanzo: Mpango wa Taifa wa Chanjo Tanzania
Ugonjwa huu unaweza kuwapata watu wa rika zote lakini watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 ndiyo wanaoathirika zaidi.
Hushambulia mishipa ya fahamu hatimaye husababisha kupooza kwa misuli, hasa ya miguu, mikono au yote kwa pamoja, na pengine misuli ya kiwambo (diaphragm) na kusababisha kifo.
Njia sahihi ya kujikinga na ugonjwa huu ni kupitia chanjo (OPV) ambayo hutolewa kwa watoto kwa njia ya matone ya kumeza mara nne kwa utaratibu ufuatao-
- Chanjo ya kwanza, mara tu mtoto anapozaliwa
- Chanjo ya pili, mtoto akifikisha umri wa wiki 6
- Chanjo ya tatu, mtoto akifikisha umri wa wiki 10
- Chanjo ya nne, mtoto akifikisha umri wa wiki 14
Chanzo: Mpango wa Taifa wa Chanjo Tanzania