Uamuzi wa Rayvany kuondoka WCB utampelekea kupata anguko kubwa katika mafanikio yake.

Uamuzi wa Rayvany kuondoka WCB utampelekea kupata anguko kubwa katika mafanikio yake.

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2021
Posts
630
Reaction score
1,262
images (1) (4).jpeg
UAMUZI WA RAYVANY KUONDOKA WCB UTAMPELEKEA KUPATA ANGUKO KUBWA KATIKA MAFANIKIO YAKE:

Ikumbukwe kuwa Rayvany alishajiondoa WCB lebo mama iliyomkuza tangu alipoondoka kwa Madee akiwa msanii mchanga.

Dhumuni la Rayvany kuondoka WCB pengine ni yeye kupata mafanikio makubwa kuliko yale aliyokuwa akipata pale WCB.
Ukweli unaouma ni kwamba Rayvany amekurupuka na atapata anguko kubwa lisiloelezeka.

Kumbuka kuwa WCB wanatoa 40% kwa wasanii wao huku wao wakibaki na 60%.
Asilimia hizi anazopewa msanii kazi yake ni savings, kula, kuhudumia afya yake, mazoezi, malazi, mavazi,chakula, usafiri n.k, ikiwa na maana kwamba msanii unatunzwa kama mfalme huku akimiliki mali za kifahari,

Asilimia za lebo kazi yake ni kumtengenezea msanii mazingira mazuri ya kazi, kulinda usalama wake, kulipia vibali vya serikali, kulipa wasimamizi wa lebo mishahara yao, kugharamikia promotion, kulipa hasara zote msanii anazotengeneza, nk
Majukumu haya ya Lebo ya WCB ni magumu sana ndio maana wasanii wengine au lebo nyingine zinashindwa kufika mbali na hata wakati mwingine kufa kwasababu ya kushindwa kumudu gharama za kusimama katika tasnia ya muziki.

Wale wanaomtetea Rayvany na kushutumu WCB hawana tofauti na mtu anayethamini mkungu wa ndizi huku akilaani mgomba pasipokujua asingeona ndizi bila mgomba.

Diamond Platnumz amekuwa akifanya mema mengi yasiyohesabika lakini adui zake ni wote wanaompiga vita hawana sababu nyingine zaidi ya wivu wa maendeleo yake.

Kwanini nasema kuwa kitendo cha Rayvany kuondoka WCB kitakuwa anguko katika maisha yake?
Sababu ni kuwa walipo ondoka wasanii wenzake waliomtangulia, Diamond Platnumz alipata maumivu makali na akachukua hatua ikiwemo kuwa makini kusaini wasanii n.k
Hakuna mtu ambaye atakuwa tayari kuumizwa kila siku lazima afike mahali akatae kuumizwa.

Wasanii waliopita waliondoka kwa shari na dharau kumbuka kuwa katika maisha unapomsaidia mtu alafu badae akakudharau ni maumivu kiasi gani utapata!
Hivyobasi hutakuwa tayari kuumizwa tena hata machozi ya maumivu yanaweza kumlaani aliyekusaliti na akakosa Mafanikio.
 
Kila mtu ana malengo yake na ndoto zake.
Acha aondoke kama ela ya kuvunja makataba kalipa. Haya haya ndio alikuwa akiambiwa Diamond kipindi anataka kinukisha na Clouds kuwa ataisha, lakini akakaza akaondoka.
Huwezi kaaa sehemu moja maisha yako yote wakati unajiona sehemu nyingine.
Life is all about taking risks
 
View attachment 2329009
Kumbuka kuwa WCB wanatoa 40% kwa wasanii wao huku wao wakibaki na 60%.
Asilimia hizi anazopewa msanii kazi yake ni savings, kula, kuhudumia afya yake, mazoezi, malazi, mavazi,chakula, usafiri n.k, ikiwa na maana kwamba msanii unatunzwa kama mfalme huku akimiliki mali za kifahari,
Chawa wa ndomo mna matatizo makubwa sana ya akili
Asilimia za lebo kazi yake ni kumtengenezea msanii mazingira mazuri ya kazi, kulinda usalama wake, kulipia vibali vya serikali, kulipa wasimamizi wa lebo mishahara yao, kugharamikia promotion, kulipa hasara zote msanii anazotengeneza, nk
Majukumu haya ya Lebo ya WCB ni magumu sana ndio maana wasanii wengine au lebo nyingine zinashindwa kufika mbali na hata wakati mwingine kufa kwasababu ya kushindwa kumudu gharama za kusimama katika tasnia ya muziki.

Wale wanaomtetea Rayvany na kushutumu WCB hawana tofauti na mtu anayethamini mkungu wa ndizi huku akilaani mgomba pasipokujua asingeona ndizi bila mgomba.
Nadhani kitu ambacho hamtaki kusema na ambacho kinakimbiza wasanii WCB ni aina ya mikataba Yao ilivyo.

Ukweli ni kuwa WCB hakuna MSAADA Wala CHA BURE.

Mkataba wao ni COMMISSION BASED and TAMAAA BASED.

Yaani Iko hivi, ukiwa Wasafi una idadi kadhaa tu ya nyimbo ambazo unapaswa kutoka ( yaani zitakazogharamiwa na Lebo Kwa budget zao ).

Ikitokea wewe mwenyewe kama msanii ukaona unahitaji kufanya zaidi, yaani KUREKODI NGOMA zaidi na Video zaidi UTAJILIPIA MWENYEWE.

Na hata UKIJILIPIA mwenyewe BADO hizo NGOMA siyo MALI YAKO. Ni MALI ya Wasafi Kwa 100%

Wa kwako ni mgawo ule ule wa 40%.

Yaani Kwa lugha rahisi hakuna msanii WCB anaemiliki Master ya UBUNIFU wa NGOMA zake. Ukitaka inafanyika biashara mpya, yaani kama Harmonize alivyonunua HAKI zake Kwa 600M.

Huyo Rayvanny mpaka Sasa Wasafi ndio wamiliki HALISI wa Kila kitu chale mpaka Jina ( Rayvanny ).

Kwasasa kajitoa kwenye shows tu, ila atafanya shows akipata pesa atafanya NGOMA zake na kushoot video akimaliza atapeleka Wasafi wakuwekee kwenye digital platforms zote halafu anasubiria kupewa 40% ya mapato hata kama hayuko kwao.

Na kibaya zaidi, kadri Anavyoendelea kupeleka mgoma ndivyo bei ya kununua hiyo Master inavyoongezeka.

Kama kweli kaambiwa milioni 800 asubirie kuambiwa tena bilioni na nusu.

In short, ndani ya WCB utakula ulichoingiza, hakuna Cha BURE. Hata ukipewa gari mtakatana kwenye kipato chako.

Kama huingizi pesa utakufa njaa.
Diamond Platnumz amekuwa akifanya mema mengi yasiyohesabika lakini adui zake ni wote wanaompiga vita hawana sababu nyingine zaidi ya wivu wa maendeleo yake.
Kati ya vitu alivyofanikiwa kufanya huyu Domo ni kuwabrainwashi myumbu kama nyie Kwa unafiki wake.

Anyway, jaribuni basi kuwa na kauli Moja kama Ndomo anasaidia wasanii au anafanya biashara.
Kwanini nasema kuwa kitendo cha Rayvany kuondoka WCB kitakuwa anguko katika maisha yake?
Sababu ni kuwa walipo ondoka wasanii wenzake waliomtangulia, Diamond Platnumz alipata maumivu makali na akachukua hatua ikiwemo kuwa makini kusaini wasanii n.k
Hakuna mtu ambaye atakuwa tayari kuumizwa kila siku lazima afike mahali akatae kuumizwa.

Wasanii waliopita waliondoka kwa shari na dharau kumbuka kuwa katika maisha unapomsaidia mtu alafu badae akakudharau ni maumivu kiasi gani utapata!
Hivyobasi hutakuwa tayari kuumizwa tena hata machozi ya maumivu yanaweza kumlaani aliyekusaliti na akakosa Mafanikio.
Huna akili.

Anyway, hapa simtetei Rayvanny lakini anaweza kupotea kweli kwasababu anacheka watu ambako wako serious kweli kumpoteza.

Ogopa sana huyo Domo. Ni kipumbavu sana kinachopenda kuonekana mbele za media kuwa kinatoa MSAADA na kupenda kuabudiwa na kushukuriwa lakini kina roho mbayaaaaaaaa.

Rayvanny asiposhtuka ATAPOTEA kweli.
 
Bila shaka utakua maskini sana......
Chawa wa ndomo mna matatizo makubwa sana ya akili

Nadhani kitu ambacho hamtaki kusema na ambacho kinakimbiza wasanii WCB ni aina ya mikataba Yao ilivyo.

Ukweli ni kuwa WCB hakuna MSAADA Wala CHA BURE.

Mkataba wao ni COMMISSION BASED and TAMAAA BASED.

Yaani Iko hivi, ukiwa Wasafi una idadi kadhaa tu ya nyimbo ambazo unapaswa kutoka ( yaani zitakazogharamiwa na Lebo Kwa budget zao ).

Ikitokea wewe mwenyewe kama msanii ukaona unahitaji kufanya zaidi, yaani KUREKODI NGOMA zaidi na Video zaidi UTAJILIPIA MWENYEWE.

Na hata UKIJILIPIA mwenyewe BADO hizo NGOMA siyo MALI YAKO. Ni MALI ya Wasafi Kwa 100%

Wa kwako ni mgawo ule ule wa 40%.

Yaani Kwa lugha rahisi hakuna msanii WCB anaemiliki Master ya UBUNIFU wa NGOMA zake. Ukitaka inafanyika biashara mpya, yaani kama Harmonize alivyonunua HAKI zake Kwa 600M.

Huyo Rayvanny mpaka Sasa Wasafi ndio wamiliki HALISI wa Kila kitu chale mpaka Jina ( Rayvanny ).

Kwasasa kajitoa kwenye shows tu, ila atafanya shows akipata pesa atafanya NGOMA zake na kushoot video akimaliza atapeleka Wasafi wakuwekee kwenye digital platforms zote halafu anasubiria kupewa 40% ya mapato hata kama hayuko kwao.

Na kibaya zaidi, kadri Anavyoendelea kupeleka mgoma ndivyo bei ya kununua hiyo Master inavyoongezeka.

Kama kweli kaambiwa milioni 800 asubirie kuambiwa tena bilioni na nusu.

In short, ndani ya WCB utakula ulichoingiza, hakuna Cha BURE. Hata ukipewa gari mtakatana kwenye kipato chako.

Kama huingizi pesa utakufa njaa.

Kati ya vitu alivyofanikiwa kufanya huyu Domo ni kuwabrainwashi myumbu kama nyie Kwa unafiki wake.

Anyway, jaribuni basi kuwa na kauli Moja kama Ndomo anasaidia wasanii au anafanya biashara.

Huna akili.

Anyway, hapa simtetei Rayvanny lakini anaweza kupotea kweli kwasababu anacheka watu ambako wako serious kweli kumpoteza.

Ogopa sana huyo Domo. Ni kipumbavu sana kinachopenda kuonekana mbele za media kuwa kinatoa MSAADA na kupenda kuabudiwa na kushukuriwa lakini kina roho mbayaaaaaaaa.

Rayvanny asiposhtuka ATAPOTEA kweli.
 
Uipende kuwaaminisha watu ujinga, ya kwamba nje ya hiyo lebo ya Wasafi, basi hakuna maisha. Hata itokee akaanguka, wewe utapata hasara gani. Mwache mtu ajichagulie maisha yake anayopenda kuishi.

Mbona Harmonize hajaanguka? Na badala yake kapata mafanikio makubwa zaidi! Kwa taaifa yako huyo dogo atafanikiwa sana tu. Na ushahidi ni siku ya Azam Festival.
 
Ndio watumishi wa serikali wanavyoamini, kwamba wakiamua kuacha kazi kwishaaa.
 
Ndio watumishi wa serikali wanavyoamini, kwamba wakiamua kuacha kazi kwishaaa.
Inawezekana pia , sio lazima uache kazi ili ufanye mambo mengine. Unaweza endelea na kazi na huku una michongo mingine. Hata wafanya biashara huwa na vyanzo vingi kikibuma hiki unaishi kwenye hiki
 
View attachment 2329009UAMUZI WA RAYVANY KUONDOKA WCB UTAMPELEKEA KUPATA ANGUKO KUBWA KATIKA MAFANIKIO YAKE:
Ikumbukwe kuwa Rayvany alishajiondoa WCB lebo mama iliyomkuza tangu alipoondoka kwa Madee akiwa msanii mchanga.

Dhumuni la Rayvany kuondoka WCB pengine ni yeye kupata mafanikio makubwa kuliko yale aliyokuwa akipata pale WCB.
Ukweli unaouma ni kwamba Rayvany amekurupuka na atapata anguko kubwa lisiloelezeka.

Kumbuka kuwa WCB wanatoa 40% kwa wasanii wao huku wao wakibaki na 60%.
Asilimia hizi anazopewa msanii kazi yake ni savings, kula, kuhudumia afya yake, mazoezi, malazi, mavazi,chakula, usafiri n.k, ikiwa na maana kwamba msanii unatunzwa kama mfalme huku akimiliki mali za kifahari,

Asilimia za lebo kazi yake ni kumtengenezea msanii mazingira mazuri ya kazi, kulinda usalama wake, kulipia vibali vya serikali, kulipa wasimamizi wa lebo mishahara yao, kugharamikia promotion, kulipa hasara zote msanii anazotengeneza, nk
Majukumu haya ya Lebo ya WCB ni magumu sana ndio maana wasanii wengine au lebo nyingine zinashindwa kufika mbali na hata wakati mwingine kufa kwasababu ya kushindwa kumudu gharama za kusimama katika tasnia ya muziki.

Wale wanaomtetea Rayvany na kushutumu WCB hawana tofauti na mtu anayethamini mkungu wa ndizi huku akilaani mgomba pasipokujua asingeona ndizi bila mgomba.

Diamond Platnumz amekuwa akifanya mema mengi yasiyohesabika lakini adui zake ni wote wanaompiga vita hawana sababu nyingine zaidi ya wivu wa maendeleo yake.

Kwanini nasema kuwa kitendo cha Rayvany kuondoka WCB kitakuwa anguko katika maisha yake?
Sababu ni kuwa walipo ondoka wasanii wenzake waliomtangulia, Diamond Platnumz alipata maumivu makali na akachukua hatua ikiwemo kuwa makini kusaini wasanii n.k
Hakuna mtu ambaye atakuwa tayari kuumizwa kila siku lazima afike mahali akatae kuumizwa.

Wasanii waliopita waliondoka kwa shari na dharau kumbuka kuwa katika maisha unapomsaidia mtu alafu badae akakudharau ni maumivu kiasi gani utapata!
Hivyobasi hutakuwa tayari kuumizwa tena hata machozi ya maumivu yanaweza kumlaani aliyekusaliti na akakosa Mafanikio.

Samahani mwandishi, wewe Bado unaishi kwenu yaani kwa Wazazi wako?
 
Na harmonize mlisema hafiki mbali ataanguka lakini Leo hii ana wachezesha amapiano, mna kosea Sana kudhani msanii hawezi toboa nje ya hao wahuni, weka akiba ya maneno alafu shuhudia mchezo unavyo kwenda
 
Naanza kumuelewa Alikiba kwanini anampeleka kiswahili ndomokaya
 
Back
Top Bottom