Ubaguzi aliouanzisha Hayati Magufuli umeuathiri sana Mkoa wa Manyara

Ubaguzi aliouanzisha Hayati Magufuli umeuathiri sana Mkoa wa Manyara

saigilomagema

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2015
Posts
4,683
Reaction score
7,222
Mkoa wa Manyara uliundwa mwaka 2002 baada ya kuugawa uliokuwa mkoa wa Arusha. Bahati mbaya Baada ya Magufuli kupata urais wa Tanzania alitangaza wazi kuwa mikoa ya Kaskazini itabidi isubiri wakati mikoa mingine wakipelekewa maendeleo. Mwanzoni sikuamini, lakini sahivi ndio nimeamini ile kauli ilikuwa ya kweli na thabiti.

Masikini Mkoa wa Manyara, mkoa wa Manyara una maendeleo gani mpaka usubiri mikoa mingine? Wilaya ya Mbulu ni mojawapo ya wilaya iliyoko mkoa wa Manyara. Mji wa Mbulu ulianzishwa mwaka 1905 siku moja na mji wa Nairobi. Mpaka sahivi navyoandika mji wa Mbulu haujafikiwa na barabara ya lami. Ukiacha wilaya za Babati na Hanang ambazo makao makuu yamepitiwa na barabara za lami kwa sababu tu barabara hizi zinapita kuelekea mikoa mingine ya Dodoma na Singida. Wilaya zingine zote, yaani Kiteto, simanjiro na Mbulu km nilivyotaja ni vumbi tupu kuna nyakati hata hazipitiki. Mkoa wa Manyara hauna soko la kisasa, hauna Stand ya kisasa mabasi ni vumbi na kadogo kweli utafikiri stand ya kijiji nafikiri watanzania wanaopitaga Babati wanafahamu vizuri.

Mkoa wa Njombe ulianzishwa mwaka 2012 miaka 10 baada ya kuanzishwa Mkoa wa Manyara. Leo Njombe wana stand ya mabasi ya kisasa, wana soko la kisasa, Njombe(makao makuu ya mkoa) imeunganishwa na wilaya zake zote kwa barabara za lami. makete, Wang'ing'ombe na Ludewa zimeunganishwa na lami.

Rais samia anapita njia ilelile ya Magufuli hana lolote jipya ubaguzi uleule. Kwanini viongozi wanabagua maeneo ya nchi ileile moja wanayoiongoza? Wanachobagua ni kitu gani. Makabila yanayoishi ndani mikoa athirika? au Ardhi ya mkoa husika? Manyara imewakosea nini Marais wa Nchi hii? Ubaguzi ni dhambi mbaya sana, alituasa baba wa Taifa ubaguzi ni sawa na kula nyama ya mtu!!!
 
Kwani magu ndio raisi wa kwanza nchi hii..waulize waliomtangulia mbona rami hakuna.
 
Umeongea tu kama ilianzishwa 1905 inamaana Magufuli ndio raisi wetu wa kwanza ili awabague acha maneno ya ushabiki maendeleo ya eneo fulani yanaletwa na wananchi wenyewe muache kukaza mlime mnatarajia raisi atawaletea lami na mavi yenu unaongelea Njombe mpaka imepewa hadhi ya mkoa inamaana wameona kuna faida na pato jingi lina toka huko kwanza Manyara yote ni eneo la mbuga huko Babati sijui Mbulu kote ni ushoroba wa kupita wanyama mnawabana wanyama wasiji nafasi.

Next time fikiri kabla ya kuandika mavi mavi Magufuli na Samia ndio maraisi tu ulio waona huyo nyerere mwinyi mkapa kikwete hujawaona na wamekaa kwa vipindi virefu tu na lami haijafika. Mtoa mada unaakili za kifaken tu
 
..magufuli alijitambulisha kama raisi jabali wa miundombinu, hivyo wananchi wa manyara wana haki ya kuuliza kwanini aliwasahau au aliwatenga kwenye miundombinu haswa barabara za lami.
Magufuli hakumaliza miaka yake kumi. Kwa hiyo uwe na busara kidogo unapomlalamikia. Kwa kasi aliyokuwa anaenda nayo ndani ya miaka mitano aliyokuwa amebakisha angewasogezea lami huko.

Acha kumchafua hayati. Kama una malalamiko yafikishe kwa Rais aliyepo madarakani.
 
Magufuli hakumaliza miaka yake kumi. Kwa hiyo uwe na busara kidogo unapomlalamikia. Kwa kasi aliyokuwa anaenda nayo ndani ya miaka mitano aliyokuwa amebakisha angewasogezea lami huko.

Acha kumchafua hayati. Kama una malalamiko yafikishe kwa Rais aliyepo madarakani.

..wanasema alikuwa na kasi ya ajabu ktk miundombinu, midege, ma-flyover, ma-sgr, ma-stieglers gorge, etc etc.

..wananchi wa Manyara wanahoji kwanini kasi hiyo iliwapita mbali?

..Je, wametengwa? Je, kuna mahali walimkosea Magufuli?
 
Mkoa wa Manyara uliundwa mwaka 2002 baada ya kuugawa uliokuwa mkoa wa Arusha. Bahati mbaya Baada ya Magufuli kupata urais wa Tanzania alitangaza wazi kuwa mikoa ya Kaskazini itabidi isubiri wakati mikoa mingine wakipelekewa maendeleo. Mwanzoni sikuamini, lakini sahivi ndio nimeamini ile kauli ilikuwa ya kweli na thabiti.
ii? Ubaguzi ni dhambi mbaya sana, alituasa baba wa Taifa ubaguzi ni sawa na kula nyama ya mtu!!!
Manyara ipo juu sana kushinda Kigoma
Tembea uone
 
Mkoa wa Manyara uliundwa mwaka 2002 baada ya kuugawa uliokuwa mkoa wa Arusha. Bahati mbaya Baada ya Magufuli a Nchi hii? Ubaguzi ni dhambi mbaya sana, alituasa baba wa Taifa ubaguzi ni sawa na kula nyama ya mtu!!!
Unaongea utoto.Hapo Babati Mjini kuna barabara za lami za mitaa zenye taa na zilijengwa kwa mradi wa ULGSP..

Kwenye mradi huo Njombe walichagua stand na Soko nyie mkachagua barabara Sasa ubaguzi upi au hujui unachoongea?

Kuna mradi wa Tactic unakuja kila Halmashauri ina Vipaombele vyake,mkitaka masoko na stand ndio tumieni hizo pesa Sasa.
 
ungeijua njombe, ungeshaacha kuifananisha na mikoa ya ajabu ajabu. uchumi wa kilimo na mazao ya misitu kule yanasababisha mzunguko mkubwa sana wa pesa. kule kuna pesa sio kama huko kwenu swekeni. wacha waendelee

..huwezi kusema mkoa fulani ni " swekeni " hivyo haustahili kuwa na miundombinu.

..na mtoa mada hajasema njombe isiendelezwe, bali ameiasa serikali iukumbuke mkoa wa manyara.
 
..wanasema alikuwa na kasi ya ajabu ktk miundombinu, midege, ma-flyover, ma-sgr, ma-stieglers gorge, etc etc.

..wananchi wa Manyara wanahoji kwanini kasi hiyo iliwapita mbali?

..Je, wametengwa? Je, kuna mahali walimkosea Magufuli?
Hata ukiwa na haraka kiasi gani huwezi kupata mtoto ndani ya mwezi mmoja kwa kuwatia mimba wanawake tisa.
 
kama mkoa ulianzishwa na miji kama nairobi iweje leo usingizie viongozi walioingia juzi

Huu mji ambao ulianzishwa pamoja na nairobi umeshindwa kukua kwa sababu moja tu ya uchawi wa akina andabayo na kutopenda maendeleo, barabarani wamezika sana kondoo na mpaka sasa uchawi umetamalaki japo kwa kiasi umepungua,yaani jifanye et unapambana kutoboa uone yaani vitu vilivyofanyika 2007 wao ndo wanaanza kufanya sasa hivi.

Wanatabia ya mashindano ya kijinga, ubishi na kutunza vitu rohoni yaani wanapenda sana migogoro
na ujinga mwingine waliwahi kupoteza dhahabu kimazingira eti kisa wazungu wanatembea na wake zao, mpaka leo wamekalia uchawi

Asilimia kubwa ya kudumaa kwa maendeleo mkoa huo inachangiwa na wao wenyewe, na ukienda kufanya biashara mji huo wa mbulu kama ni mkabila jipange
 
..huwezi kusema mkoa fulani ni " swekeni " hivyo haustahili kuwa na miundombinu.

..na mtoa mada hajasema njombe isiendelezwe, bali ameiasa serikali iukumbuke mkoa wa manyara.
Kama hawajikumbuki wenyewe, nani atawakumbuka?
 
Ungeijua Njombe, ungeshaacha kuifananisha na mikoa ya ajabu ajabu. uchumi wa kilimo na mazao ya misitu kule yanasababisha mzunguko mkubwa sana wa pesa. kule kuna pesa sio kama huko kwenu swekeni. wacha waendelee
Mikoa ya ajabu ni ipi? Manyara? We huifahamu Tanzania. Njombe iko chini sana kimapato kutoka Manyara ndio maana Njombe imekuwa mkoa miaka kumi baada ya Manyara. Katafute taarifa za serikali, juzi tu waziri Bashungwa alisoma taarifa Manyara ilikuwa ya pili kitaifa. Taafira ya Nov, 2018 aliyoisoma Selemani Jafo km waziri wa TAMISEMI mkoa wa Manyara ulikuwa wa 2 kitaifa katika makusanyo ya mapato. Mbulu ktk kundi la halmashauri za miji kimakusanyo imeongoza kitaifa miaka 3 mfululizo ikiwemo mwaka ulioisha juzi taarifa ilisomwa hivi karibuni na waziri Bashungwa.

Haiwezekani ulinganishe Njombe na Manyara kwa namna yoyote, Manyara ina vyanzo vingi ikiwemo Tanzanite inayopatikana Manyara tu hapa duniani, bado mbuga maarufu za Lake Manyara na Tarangire. Wanafuga mifugo mingi sana kuliko Njombe, wanalima nafaka za aina nyingi ikiwemo na mazao ambayo hayalimwi hata huko Njpmbe. Njombe imeanza kusikika juzi tu hasa mambo yenu hayo ya parachichi.

Halafu watanzania tunatakiwa tuielewe historia ya nchi yetu, unavyozungumzia mji wa Mbulu umeanza mwaka 1905 ieleweke kuwa nchi yetu ilikuwa imegawanywa katika kinachoitwa Provinces kabla ya uhuru. Kulikuwa na Lake Zone province iliyokuwa na wilaya 7 ikiwemo Mwanza, Central province iliyokuwa na wilaya 2 za Singida na Dodoma na Northern province iliyokuwa na wilaya za Mbulu na Arusha. Mbulu ya wakati ule ilkuwa ndiyo wilaya za Babati, Hanang na Karatu ya leo. Mbulu ilikuwa wilaya hata kabla hiyo Njombe yenu haijawa wilaya sijui ilikuwa kata au kitu gani. Bahati mbaya mwaka wa 1963 wilaya nyingi zilizokuwa ndani ya provinces ziliunda mikoa kwa mfano ya Mwanza, shinyanga, Mara, Singida, Dodoma na mengine ila tu northern province haikugawanywa ila iliitwa mkoa wa Arysha bila kugawanywa ktk mikoa miwili ambayo kimsingi ingekuwa mkoa wa Arusha na mkoa wa Mbulu. Hili halikufanyika kwani ndiyo ilikuwa uamuzi wa serikali ya wakati ule ambao haukulalamikiwa ila uliheshimiwa.

Kizungu tunaweza kusema "it is high time" mji wa Mbulu kufikiwa na lami kwa kuheshimu historia yetu na kwa kuwa kila moja wetu anajua barabara ya lami ni kichochea(catalyst) ya maendeleo. Kuunganisha mji wa Mbulu na Tanzania na ulimwengu ni Km 75 tu maana barabara ya lami ilishafika mji wa Karatu tangia kipindi cha awamu ya 3 ya hayati Benjamin W. Mkapa. Hili halihitaji matusi kwani hakuna mwananchi au wananchi wanaoweza kujijengea barabara ya lami isipokuwa serikali, inapotokea mtu anaandika hisia zake tusimkebehei, kumtukana na mambo mengine yasiyofaa ila tumwuunge mkono. Sote twahitaji maendeleo.
 
Mikoa ya ajabu ni ipi? Manyara? We huifahamu Tanzania. Njombe iko chini sana kimapato kutoka Manyara ndio maana Njombe imekuwa mkoa miaka kumi baada ya Manyara. Katafute taarifa za serikali, juzi tu waziri Bashungwa alisoma taarifa Manyara ilikuwa ya pili kitaifa. Taafira ya Nov, 2018 aliyoisoma Selemani Jafo km waziri wa TAMISEMI mkoa wa a zake tusimkebehei, kumtukana na mambo mengine yasiyofaa ila tumwuunge mkono. Sote twahitaji maendeleo.
Umeshafika Njombe au unaisikia tu mimi ni mwenyeji wa Manyara na naifahamu jombe pia, kwa kuishi. sasa kama Manyara haina shida, mnalalamika nini?
 
Manyara kwa njombe bado sana angalia hata wingi wa mapato na bado mkoa wa njombe ndo unazidi kufunguka zaidi
IMG-20220809-WA0018.jpg
 
Ungeijua Njombe, ungeshaacha kuifananisha na mikoa ya ajabu ajabu. uchumi wa kilimo na mazao ya misitu kule yanasababisha mzunguko mkubwa sana wa pesa. kule kuna pesa sio kama huko kwenu swekeni. wacha waendelee


Pesa ipi mkuu ? Njombe ndio mkoa watu wanaishi miaka kidogo kuliko mkoa wowote Tanzania 52.8% wastani
Moja ya mkoa backwards ushirikina na uchawi na matendo ya kikatili hutokea
Ubaguzi, ubinafsi na roho mbaya

Kama shetani angetua Tanzania angeanzia Njombe
 
Tji
Unaongea utoto.Hapo Babati Mjini kuna barabara za lami za mitaa zenye taa na zilijengwa kwa mradi wa ULGSP..

Kwenye mradi huo Njombe walichagua stand na Soko nyie mkachagua barabara Sasa ubaguzi upi au hujui unachoongea?

Kuna mradi wa Tactic unakuja kila Halmashauri ina Vipaombele vyake,mkitaka masoko na stand ndio tumieni hizo pesa Sasa.

Mkuu thibitisha hapo kwenye mkoa kuchagua priorities inaonekana una points but you must substantiate them
 
Ungeijua Njombe, ungeshaacha kuifananisha na mikoa ya ajabu ajabu. uchumi wa kilimo na mazao ya misitu kule yanasababisha mzunguko mkubwa sana wa pesa. kule kuna pesa sio kama huko kwenu swekeni. wacha waendelee
 

Attachments

  • Screenshot_20230817-010352_Chrome.jpg
    Screenshot_20230817-010352_Chrome.jpg
    133.5 KB · Views: 2
Back
Top Bottom