Ubakaji sasa ni tatizo la Dunia

Ubakaji sasa ni tatizo la Dunia

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Kulingana na Takwimu za ubakaji kwa kila Nchi 2021(Rape statistics by country 2021). Takwimu zinaonesha kuwa inakadiriwa asilimia thelathini na tano 35% ya Wanawake Duniani wamepitia ubakwaji, jaribio la ubakwaji, au usumbufu wa kingono katika maisha yao.

Katika Nchi nyingi zinaweka taarifa za ubakaji zinaonesha kuwa ni Wanawake wachache sana( chino ya asilimia arobaini 40% ya Wanawake wote Duniani wanaotafuta msaada wa kisheria baada ya kubakwa na chini ya asilimia kumi 10% ndiyo wanaotafuta msaada a kisheria.

Lakini pamoja na watu kusikia kila mara uhusiano na ubakaji kwa wanawake, wanaume pia wamekuwa wakipitia changamoto ya ubakwaji kila siku.

Wanawake wenye umri kati ya miaka 16 mpaka 19 ndiyo wahanga wakubwa wa matukio ya kubakwa Duniani, Wasichana waliofikia umri wa kuingia vyuoni yaani miaka 18 mpaka 21 hawa huwa hatarini mara tatu zaidi.

Marekani asilimia sabini (70%) ya matukio ya ubakaji hufanywa na watu wanaofahamika kwa wahanga. Takwimu zinaonesha kiwango cha ubakaji Marekani kuwa 27.3 lakini matukio ya ubakaji yamekuwa yakiwekewa usiri mkubwa kutokana na wahanga kuhofu, kuogopa kukaripiwa, kuogopa wanafamilia kufahamu, kesi kutokutiliwa uzito katika utekelezaji wa sheria. Inakadiriwa kuwa asilimia tisa 9% ya wabakaji walihukumiwa adhabu ya kifo, asilimia tatu 3% kuingia kifungoni huku asilimia ofisini na saba 97% ya wabakaji wakiwa huru mitaani.

Afrika ya kusini ndilo eneo linaloongiza kwa ubakaji Duniani kwani inakadiriwa uwa na matukio 132.4 ya ubakaji kwa kila idadi ya watu laki moja 100,000 ( 132.4 incidents per 100,000 people).

Utafiti uliofanywa na " South African Medical Research Council ulionesha inakadiriwa kuwa kwa kila mwanaume mmoja kati ya wanne walioshiriki katika kutoa taarifa za utafiti kufikiri kufanya tendo la ubakaji. Licha ya Bunge la Afrika ya kusini kupitisha na kuboresha sheria zinazohusiana na mahusiano ya kingono mwaka 2007 bado kiwango cha ubakaji kimeendelea kuongezeka.

Tanzania takwimu zinaonesha kiwango cha kesi 12.6 kwa watu 100, 000 kuripotiwa mwaka 2011 ,mwaka 2015 kiwango kilipungua na kuwa kesi 10.9 kwa watu 100,000. Mwaka 2016 Mamlaka ya Takwimu " National Bureau of Satatistics ilionesha kesi 7645 za ubakaji ambazo 7180 zilikuwa za Tanzania Bara na kesi 465 zikiwa za Zanzibar.

Hali hii inaonesha kupungua kwa kesi hakumaanishi kupungua kwa ubakaji ila kutokana na kasumba ya usiri na utekelezaji mbovu wa sheria katika Nchi mbalimbali ubakaji umeendelea kuwa mwiba na tatizo la kidunia.

111216756-women-bondage-lift-hands-against-violence-against-women-image-blur-international-wom...jpg


Screenshot_20210330-161159_Chrome.jpg


Screenshot_20210330-161226_Chrome.jpg
 
Pia kumbuka hizo ni record ambazo zimerekodiwa polisi, madawati ya jinsia na sehemu nyinginezo. Lakini kuna watu ambao hawasemi kama walishapitia hayo aidha kwa kuona aibu au mengineyo.

Kwahiyo record inaweza ikawa kubwa zaidi.
 
No ni kwamba kwa sasa wanawake wana sauti / wanasikilizwa na wana sehemu ya kuongea.

Kwenye hii duania ya mwenye nguvu kumdimimiza asiye na nguvu..., Amini nakwambia mwanamke amekuwa akinyanyaswa tangu enzi na enzi (it just happened kwamba mwanaume alijiwekea kwamba yeye ndio yupo juu) na kwa kutumia hata baadhi ya maandiko ili kusupport huo unyampara..... basi amekuwa akifanikiwa.

Ingawa kwa sasa hii trend imekuwa ngumu sana kwa wanaume hujui useme nini au ufanye sababu a friendly gesture inaweza ikatafsiriwa kama sexual harassment.
 
No ni kwamba kwa sasa wanawake wana sauti / wanasikilizwa na wana sehemu ya kuongea...

Kwenye hii duania ya mwenye nguvu kumdimimiza asiye na nguvu..., Amini nakwambia mwanamke amekuwa akinyanyaswa tangu enzi na enzi (it just happened kwamba mwanaume alijiwekea kwamba yeye ndio yupo juu) na kwa kutumia hata baadhi ya maandiko ili kusupport huo unyampara..... basi amekuwa akifanikiwa.

Ingawa kwa sasa hii trend imekuwa ngumu sana kwa wanaume hujui useme nini au ufanye sababu a friendly gesture inaweza ikatafsiriwa kama sexual harassment...
friendly gesture imenifurahisha sana.
 
Pia kumbuka hizo ni record ambazo zimerekodiwa polisi, madawati ya jinsia na sehemu nyinginezo. Lakini kuna watu amabao hawasemi kama walishapitia hayo aidha kwa kuona aibu au mengineyo.

Kwahiyo record inaweza ikawa kubwa zaidi.
Naam..takwimu zinaonesha Nchi nyingi kuna hii hali ya kelele za ukimya ......noise of silence!..
Taarifa zinazoripotiwa ni chache mno ukiachilia mbali zinazogeuka kuwa dili kwa wale jamaa wale.
 
Imran Khan alipanga kupitisha sheria ya kuwahasi wanaume wanaobaka baada ya ubakaji kuendelea kukithiri nchini Pakistan.
Kule wengine wanafanya unyanyasaji wa kijinsia kama njia ya kutoa adhabu mfano binti akikosea kuvaa au asiposalimia.


Hata hapa bongo utasikia mtu anasema mpe mimba huyo, mle .... Hizi zote ni sexual arrasment, bado dunia haijaja na mpango madhubuti wa kupambana na hizi cases ila itakuja siku. The world must be civilized
 
Imran Khan alipanga kupitisha sheria ya kuwahasi wanaume wanaobaka baada ya ubakaji kuendelea kukithiri nchini Pakistan.
Kule wengine wanafanya unyanyasaji wa kijinsia kama njia ya kutoa adhabu mfano binti akikosea kuvaa au asiposalimia.


Hata hapa bongo utasikia mtu anasema mpe mimba huyo, mle .... Hizi zote ni sexual arrasment, bado dunia haijaja na mpango madhubuti wa kupambana na hizi cases ila itakuja siku. The world must be civilized
daah..mifano uliyoitoa imeniumiza sana, kumbe hali ni tete mno.
 
Ni kweli kabisa ubakaji ni mkubwa kwani kuna wengine wamepewa kazi na vyeo kwa kutoa papuchi bila hiyari yao nao ni ubakaji.
 
Ila mjue ubakaji wa kimagharib nao nitofauti na ubakaji tunaoujua wa kumpiga ngwala mdada na kutumia real physical power kutia dudu, nichi nyingi hasa zilizoendelea hata mke wako akisema hajisikii ukamlazimisha upige kimoja, huo ni ubakaji, mtoto wa miaka kumi na saba aliemtaani hata kama aliishia la saba akasota hana mpango mwengine ukiolewa huo ni ubakaji
Mfano Marekani, ukijifanya unamautani ukampiga mtu busu akishtaki kua ulitaka kumkisi kwa lazima huo ni ubakaji na kama ni mwanafunzi unafukuzwa chuo kabisa

Ni hayo tu ndugu zangu najua wanaopiga papuchi kwa kulazimisha hata kwa wapenzi wao niwengi au tuko wengi, wotetutaitwa wabakaji uko majuu
 
Ila mjue ubakaji wa kimagharib nao nitofauti na ubakaji tunaoujua wa kumpiga ngwala mdada na kutumia real physical power kutia dudu, nichi nyingi hasa zilizoendelea hata mke wako akisema hajisikii ukamlazimisha upige kimoja, huo ni ubakaji, mtoto wa miaka kumi na saba aliemtaani hata kama aliishia la saba akasota hana mpango mwengine ukiolewa huo ni ubakaji
Mfano Marekani, ukijifanya unamautani ukampiga mtu busu akishtaki kua ulitaka kumkisi kwa lazima huo ni ubakaji na kama ni mwanafunzi unafukuzwa chuo kabisa

Ni hayo tu ndugu zangu najua wanaopiga papuchi kwa kulazimisha hata kwa wapenzi wao niwengi au tuko wengi, wotetutaitwa wabakaji uko majuu
ukifasiri ubakaji utaona hakuna ubakaji wa kimagharibi wala wa Kiafrika ubakaji ni uleule. Ukipata muda pitia SOSPA Act Na 4 ya mwaka 1998.
kuna maneno wanayatumia sana wenzetu " against ones consent "..
nadhani umeelewa.
 
ukifasiri ubakaji utaona hakuna ubakaji wa kimagharibi wala wa Kiafrika ubakaji ni uleule. Ukipata muda pitia SOSPA Act Na 4 ya mwaka 1998.
kuna maneno wanayatumia sana wenzetu " against ones consent "..
nadhani umeelewa.

Hio consent unayosema ndo nilichoeleza kua hata mke akiwa hayuko tayari kufanya ukamlazimisha upige kimoja huo ni ubakaji

Na wengi wanafanya
 
Hio consent unayosema ndo nilichoeleza kua hata mke akiwa hayuko tayari kufanya ukamlazimisha upige kimoja huo ni ubakaji

Na wengi wanafanya
Ah..ah..kumbe tupo pamoja sana ila mifano yako daah..
 
Hio consent unayosema ndo nilichoeleza kua hata mke akiwa hayuko tayari kufanya ukamlazimisha upige kimoja huo ni ubakaji

Na wengi wanafanya
Ah..ah..kumbe tupo pamoja sana ila mifano yako daah..
 
Back
Top Bottom