Ubalozi wa Marekani nchini umeendelea kuwasisitizia Wananchi wake waliopo nchini kuwa uwezekano wa kupata Corona nchini ni mkubwa

Ila hawa Wamarekani ni kama wamechanganyikiwa, juzi hapa karibia Taifa lao zima lilikuwa na maandamano dhidi ya ukatili wa mauaji lakini hakuna aliyewaigilia juu ya mkusanyiko mkubwa wa watu tena mbaya zaidi wao ndio wanakesi nyingi dhidi ya COVID 19. Yani walivyo washenzi wanaangalia ya watu wakati kwao hali ni Tete kutokana na maandamano wamepata kesi elfu 19.

Hakuna aliyesema kitu ila ya watu wanayajua sana, wazuie kwanza maandamano dhidi ya ubaguzi ndio waje waseme hovyo kabisa hawa.
 
Corona ipo Dar nimemzika juzi Shangazi yangu kipenzi aliezaliwa na baba yangu. Alikua awezi kupumua kabisa. Bado najiuliza ameipataje..? Hata mimi kohoni nasikia sipaelewi leo. Siasa zao za kutaka pesa za watalii, zinatumalizia wazee wetu.
 
Mkuu Retired ni halali tu kuchekwa kwenye basi, kwasababu umekuwa kituko, maandishi yako tu hapa yanaonyesha kuwa umekuwa kituko.
Tumshukuru Mungu kuwa hali sio mbaya, Mungu amejibu maombi yetu.
Wewe si ni CCM nami sishangai kuandika hivyo. Kwahiyo Mungu ana upendeleo. Nilitegemea ulete scientific arguments kumbe unaleta talalila za Ndugai! Na most likely waliokuwa kwenye bus ni CCM! wanasikliza Jiwe anasema nini . sensible people like CDM will never do that!
 
Watanzania Acheni viherehere hii haiwahusu nyie fateni Maneno na Miongozo ya viongozi wenu, Wamarekani watafuata miongozo ya viongozi wao.
 
Hawa nao wanachosha, na sasa naanza kuelewa Kwa nini wanaingia mgogoro wa kiuchumi na biashara kila mara na nchi ya China,

Kinachowasumbua ni kijicho!
 
Mkuu Retired ni halali tu kuchekwa kwenye basi, kwasababu umekuwa kituko, maandishi yako tu hapa yanaonyesha kuwa umekuwa kituko.
Tumshukuru Mungu kuwa hali sio mbaya, Mungu amejibu maombi yetu.
Watu wanakufa kwa wingi kimyakimya ili kuonyesha rais amefanikiwa
 
Ukweli ni kwamba hao watu wao hawataki kurudi huko kwao maana toka walipoanza kuwaambia warudi si ingekuwa washarudi, waje wawasombe kilazima wawapeleke wakaandamane huko.
ULE MSAFARA WA VIONGOZI WA SERIKALI YETU KWENDA UBALOZINI ULIKUWA NA UJUMBE GANI KWA HUU UBALOZI? HUO UJUMBE ULIELEWEKA? KWANI TAKWIMU ZA CORONA NCHINI ZIKOJE? HUU UBALOZI UNA HOJA KWELIKWELI
 
Siku akiugua Mmarekani corona hapa Bongo hakika kipele kitakuwa kimepata mkunaji...tutakomaje.
 
ULE MSAFARA WA VIONGOZI WA SERIKALI YETU KWENDA UBALOZINI ULIKUWA NA UJUMBE GANI KWA HUU UBALOZI? HUO UJUMBE ULIELEWEKA? KWANI TAKWIMU ZA CORONA NCHINI ZIKOJE? HUU UBALOZI UNA HOJA KWELIKWELI
Solution ni kwamba waje wawasombe tu na kuwarudisha huko paliko salama wakakusanyane ili kuongeze nguvu ya maandamano.
 
Hahaaaa! Hawa watu bana!

Huko Marekani sasa hivi hakuna cha Corona wala bibi yake Korona.

Sasa hawa watu wa ubalozi wanaleta za kuleta.

Watanzania endeleeni na maisha yenu kama kawaida.

George Floyd kaimaliza hiyo Corona.
Wewe ngabu mbeba mabox maarufu na wewe unawakandia mabosi wako? au na wewe walishakuwekea goti shingoni...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…