FatherOfAllSnipers
JF-Expert Member
- Mar 13, 2019
- 1,692
- 4,442
Assalam Aleykum!
Habari zenu wakuu,
mimi nachukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwenda kwenye Ubalozi wa nchi ya Palestina hapa Nchini Tanzania kwa kuokoa maisha yangu.
Nilikuwa katika zunguka zunguka zangu hapa jijini kutafuta mkate wangu wa kila siku, nikiwa na njaa pamoja na kiu ya maji huku nikiwa
Sina hata senti mfukoni mwangu japo ya kuniwezesha kununua andazi.
Ghafla nikatokea kwenye ubalozi wa Palestina hapa Dar es salaam,
ubalozi huu umeweka maji safi ya kunywa nje ya geti lao, ambapo mwenye uhitaji anaruhusiwa kunywa, kunawa n.k bila kuomba ruhusa,
Kwakweli hili ni jambo kubwa sana kwangu nimeliona,
bila shaka sote tunafahamu ni kiasi gani jua linawaka hapa jijini kwetu,
Kwa kitendo cha ubalozi kuweka maji safi kabisa na salama ya bure kwenye ubalozi wao wameokoa Maisha yangu.
Ni jambo zuri na lenye ubinadamu linalo faa kuigwa hata na balozi zingine ikiwemo ubalozi wa Israeli hapa Tanzania,
na hata taasisi zingine waige mfano huu wa serikali ya Palestina kupitia ubalozi wao hapa Tanzania.
Habari zenu wakuu,
mimi nachukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwenda kwenye Ubalozi wa nchi ya Palestina hapa Nchini Tanzania kwa kuokoa maisha yangu.
Nilikuwa katika zunguka zunguka zangu hapa jijini kutafuta mkate wangu wa kila siku, nikiwa na njaa pamoja na kiu ya maji huku nikiwa
Sina hata senti mfukoni mwangu japo ya kuniwezesha kununua andazi.
Ghafla nikatokea kwenye ubalozi wa Palestina hapa Dar es salaam,
ubalozi huu umeweka maji safi ya kunywa nje ya geti lao, ambapo mwenye uhitaji anaruhusiwa kunywa, kunawa n.k bila kuomba ruhusa,
Kwakweli hili ni jambo kubwa sana kwangu nimeliona,
bila shaka sote tunafahamu ni kiasi gani jua linawaka hapa jijini kwetu,
Kwa kitendo cha ubalozi kuweka maji safi kabisa na salama ya bure kwenye ubalozi wao wameokoa Maisha yangu.
Ni jambo zuri na lenye ubinadamu linalo faa kuigwa hata na balozi zingine ikiwemo ubalozi wa Israeli hapa Tanzania,
na hata taasisi zingine waige mfano huu wa serikali ya Palestina kupitia ubalozi wao hapa Tanzania.