Ubinafsi wetu wanawake ndio chanzo cha wanaume kutuumiza

sijasema wadada wote huumizwa hivyo kuwa selfish,
Weee unaweza ukamtukana mwanaume yeyote kisa umeumizwa na mtu mwenye jinsia hiyo? Acha zako mkuu unahararisha ujinga tu other wise useme demu alikuwa opportunits ntakuelewa.
 
Huyo dada hakumpenda jamaa,ila mwanamke akikupenda NYIEEEE
Back to me mama watoto hana kazi ni mama wa nyumbani,ila can u imagine huwa anabana hela ninayomuachia then ananichukulia zawadi kali sana,,halafu ukichek hela ninayomuachia ni kuduchuu mno
Angalia usije ukawa na msaidizi,mwenyewe unakiri kua hela unamwachia kiduchu,hujiongezi hiyo hela ya ziada inatoka wapi?,bro shutuka mapema

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Kama mwanamke sio Mke Wako na HAUJAMZALISHA WATOTO. usimsomeshe.. usimuanzishie biashara, na hakika usijenge kabisa kwao.. ni hela ya chipsi tu ndio umpe..
Hii comment iwekewe lamination
 
Utaogopa kutendwa mpaka lini.....hata usubiri milele hautompata huyo Malaika.....kama vipi uje nikutende pia........
Naona unajitambua....kweli sisi ni bidhaa adimu sana...yaani nimefikia wakati nawakimbia wanawake wengi sababu mmetumika sana na mnapiga virungu balaa tena vya fasta mno i.e zero waiting time...kwa hiyo nimeamua ni mwendo wa mabikira tu kwa sasa....
 
Mkuu,
wanaume tuko
Tofauti.

Hapa Najaribu kuvaa viatu vya jamaa,

binafsi wengine hatujaumbwa kuomba omba omba au kulia Lia shida kwa wanawake au watu baki.

Sometimes
tunakutana na Changamoto unakaza tu kiume,
Mwanaume kuomba chakula kwa mwanamke Ni fedhea.
(Hasa Kama ushauona KABISA upepo wa mwanamke ulienae ni mtu wa Aina gani)

Honestly,
Jamaa alikua sahii kabisa.[emoji106]
 
Ni kweli kabisa mkuu,
Yamewahi kunikuta
 
Ilinikuta few years ago niliuza geto nikahamia kwa manzi angu nikiwa Sina direction

Asee ilikua nikipakuliwa msosi no addition na manzi alikua mchungu balaa kila muda alikua ananiwakia hatari

Nilikaa one wiki nikaona Ni ungese nikahamia kwa masela geto.
 
Usemayo Ni kweli kabisa,

Nna mwanamke wangu mmoja uyo, Ni mbinafsi wa kutupa.

Leo ndo tumerudiana baada ya wiki Juzi kuzinguana, vibaya mno.
Ananiomba Ela ya kuboost biashara yake afu eti ananiwekea na DEADLINE.

Na deadline line imefika,
Namweleza asubiri nitoke msibani, yeye analazimisha Ela itumwe Kwenye simu sikU Iyo iyo.

Anasema ikishindikana, ataenda kuomba msaada kwingine na nisije mlaumu.
(NMEMJIBU,
" Wee Nenda tu hata hainistui coz utakaoumia ni uchi wako na najua kwangu you are always after your something"

Na Tena anafoka eti,
Nimekua mwanaume asiyena msaada kwake kila anapokwama,

Ila
Anasahau kua hata Iyo biashara inayoleta chokochoko,
-wazo nimempa Mimi, baada ya kuchoka kua ananiomba omba Ela ovyo.
-mzigo wake wa kuanzia nmechangia Zaid ya 50%,
-Kodi ya fremu miezi 6 ya Kwanza nmemlipia mimi,
- anakonunua mzigo nmemuunganisha Mimi.
-usafirishaji wake, ushuru, clearance n.k kwa mizigo yake kila akiagiza nagharamia Mimi maana anaviziaga nnapoagiza mizigo yangu anaomba na yeye mzgo wake nimuunganishie. Kwaiyo hatoi hata Mia.

Yaani uyu kiumbe Hana shukrani kabisa,

Bad enough,
Afu alivoking'anizi eti anataka tuzae mtoto.

Kiukweli,
Nikifanya kosa la kumzalisha mwanamke kichwa box Kama huyu,

Ntakua nmeikosea Sana damu yangu kumchagulia mama MBINAFSI Kama uyu.
 
Kwani unadhani wanaosema mshahara wa mume Mil 1 + mshahara wa mke 3mil = 1mil wanatania.

Mwanamke kukuvumilia na kukulindia heshima uchumi ukiporomoka ni nadra sana.
 
Kwani unadhani wanaosema mshahara wa mume Mil 1 + mshahara wa mke 3mil = 1mil wanatania.

Mwanamke kukuvumilia na kukulindia heshima uchumi ukiporomoka ni nadra sana.

Wanawake wakukaa nyumbani na kupika baac. Akishakuwa na kikazi chake ni rahic sana kukupanda kichwani, baazi wanajitambu na kuona umuhimu wa mumewee.
 
Ndiyo sababu tuliooa wengi tunazuia fursa za kipato kikubwa kwa wake zetu kwa makusudi (ila kwa mbinu yeye asijue) kwani tunajua matokeo yake.

Wanawake waliowengi wakimzidi mwanaume kipato huharibu ndoa zao. Hivyo kama mwanaume unathamini ndoa yako huna budi kumdhibiti mkeo kwenye kipato chake la sivyo utaishia kupata maumivu makali.

Usiombe mkeo aanze kukudharau kwasababu ya kipato,, maumivu yake ni makali kiasi unaweza jimaliza.
 
Sawa ni mama zetu ila wanawake wana ROHO MBAYA SANA, mnaweza kulala njaa ndani (familia) ila mwanamke ana hela.
Unaweza kuhangaishwa na ka hela kadogo mpaka ukapata stress huku mkeo katoka kuvunja KIKOBA na anakusikia unavyojilalamisha kukosa hiyo elfu 50.Huku wewe ndie mtoa hela za marejesho ya hicho KIKOBA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…