Ubingwa na ushindi katika mechi ya Simba na Yanga bora nini?

musami

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2011
Posts
1,434
Reaction score
458
Kama fedha inayoambatana na ubingwa hailingani na fedha inayotumika kwenye usajili,na siku zote bingwa huwa anaishia hatua za mwanzoni kwenye mashindano ya Afrika.Sasa jambo la kujiuliza kipi kinaleta raha,Ubingwa au ushindi katika mechi ya simba na yanga?
 
Yanga bado anaongoza kwa kuchukua ubingwa wa Tanzania,pia Yanga anaongoza kumfunga Simba mechi nyingi
 
Kumpiga Ndala ndo raha !! Hi kila mtu anajua
 
Yanga bado anaongoza kwa kuchukua ubingwa wa Tanzania,pia Yanga anaongoza kumfunga Simba mechi nyingi

Anayecheka mwisho ndiyo Anayecheka zaidi! Kwa mujibu wa utani na soka la bongo kumfunga mtani ndio mpango mzima. Ubingwa ukiwa umefungwa na mtani hauna raha yoyote! Raha mpaka basi kumchapa kandambili! Maumivu ya kufungwa na mtani ni makali sana na hayawezi kupozwa kwa kutwaa taji la vodacom! Ndio maana simba/Yanga ikifungwa na timu nyingine hakuna kizungumkuti na uongozi hauwezi kutikisika, lakini ukifungwa na mtani bakora zinaweza kutembea! na uongozi unaweza kuondolewa, kocha anaweza timuliwa na wachezaji wanabaki roho juu wakihofia kuambiwa wamesaliti timu! Utasubiri sana mambo haya kuisha! Sema tu TFF wamesaidia sana kukingia kifua Viongozi wasipinduliwe kama zamani, kisa ikiwa ni kufungwa na mtani! Pole kandambili, endelea kuuguza maumivu maana mnyama ndiye aliyecheka mwisho, naona Utasubiri sana kusubiri zamu yako ya kucheka!
 
raha mno kumfunga ndala.Yanga kachua 70mln.Kwenye mtani jembe Simba kachukua 77 mln
 
Kwa Tz Yanga apigwe tu.
 
Kwa Tz Yanga apigwe tu.

Mkuu pole sana, lakini ndio hivyo watani Yanga ndio Bingwa tena mapemaaa.....watani endeleeni kuijenga Simba YOSSO.....inshallah ipo siku mtaona mwezi.......ila kwa sasa YANGA ndio habari ya MUJINI!
 
Ukiifunga simba pekee huwi bingwa ila ukikusanya point za kutosha ikiwemo kamfunga Simba utakuwa bingwa.
Mbn ulaya hawasemagi bila kamfunga man au arsenal au Liverpool ubingwa sio mtamu
 
Kwa Yanga ligi ina faida zaidi...Kumbuka Yanga ndio timu inayoongoza kwa mapato ya mechi...Timu ikifanya vizuri mashabiki wengi wanaingia uwanjani hivo timu inavuna mapato zaidi...Pia mdhamini wa timu (Kilimanjaro Premium Lager) anatoa kiasi cha pesa kama pongezi ya Ubingwa
 
Mkuu pole sana, lakini ndio hivyo watani Yanga ndio Bingwa tena mapemaaa.....watani endeleeni kuijenga Simba YOSSO.....inshallah ipo siku mtaona mwezi.......ila kwa sasa YANGA ndio habari ya MUJINI!

Asante! Hongereni, bila simba yanga hamma stori ma bila yanga simba hamna stori na wala ubingwa hautanoga, raha ya ligi ya Tz kwa simba na yanga ni utani wetu!
 
Ukiifunga simba pekee huwi bingwa ila ukikusanya point za kutosha ikiwemo kamfunga Simba utakuwa bingwa.
Mbn ulaya hawasemagi bila kamfunga man au arsenal au Liverpool ubingwa sio mtamu

Ndo maana ile inaitwa EPL na hii inaitwa VPL. Ni vitu viwili si vya kulinganisha!
 
Tokea nianze kufuatilia mpira sijawai kusikia shabiki yeyote wa mpira anajiua kwa kukosa ubingwa ila mara nyingi wanajiua kwa kufungwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…