Ubingwa wa Rais Magufuli katika kuunda maneno: Je hapa alimaanisha nini?

Ubingwa wa Rais Magufuli katika kuunda maneno: Je hapa alimaanisha nini?

X-bar

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2019
Posts
1,006
Reaction score
1,156
Kitu ambacho nakifuruhia ninaposikiliza maneno/hotuba za wanasiasa hapa nchini ni matumizi yao ya lugha hasa pale wanapounda maneno mapya na tungo/virai ambazo zinasimama kama utambulisho wao kwenye uwanja wa siasa. Yafuatayo ni baadhi ya misamiati na tungo za wanasiasa na majina yao kwenye mabano.
  • Hata nyasi tutakula (Bazil Mramba)
  • Soka la Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu (Rais Mwinyi)
  • Akili za kuambiwa changanya na zako (Rais Kikwete)
  • Ukitakaka kuona nyeti za kuku, subiri upepo upulize (James Lembeli)
  • Kubadili gia angani (Freeman Mbowe)
  • Sawa Sawa! (Maalim Seif)
  • Wacha wazime tutawasha vibatali (Rais Shein)
  • Kujimwambafai (Rais Kikwete)
  • Bao la mkono (Nape)
Lakini kwa Rais Magufuli, yeye ni tofauti kidogo kwamaana anapenda kutunga kauli/maneno ya mkato yenye "vijembe" ndani yake kwa kutohoa maana ya maneno mengine ya kishwahili au hata kingereza kama ifuatavyo.
  • Wanaoshi mabondeni, wacha mafuriko "yawa-bondoe" : Hapa alimaanisha wacha wakumbwe na mafuriko wale wanaokaidi kuhama mabondeni.
Hata hivyo sikumuelewa pale aliposema watalii waje tu na kwamba hawatawekwa karantini ikiwa joto lao la mwili watakapoingia hapa nchini litakuwa la kawaida bali wataruhusiwa waende "waka-coronize" huko mbugani. Je, hapa alimaanisha wakasambaze corona au?
 
Mimi niliipenda Atakayekuwepo dar mpaka 2020 ni mwanaume kweli kweli!
 
Wasambaze tuu virusi kwenye sekta ya utalii.
Shida yetu ni pesa tuu.
Uhai wa binadamu hatuujali sababu tunafyatua watoto vya kutosha
 
Kikwete kaongea maneno yatakayo Baki milele
 
Kikwete kaongea maneno yatakayo Baki milele
 
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Anatufanyizia Kazi
 
"mimba kwa wanafunzi ni viherehere vyao"

JK.

"Sina haja na kura za watumishi"

JK

"Ukitaka kula na wewe lazima uliwe kidogo"

JK.
 
Siyo kila maskini ni mjamaa kamili.

Nia tunayo...

jifunze kusoma wakati ni huu!
jknyererer
 
Uhuru bila nidhamu ni wenda wazimu!

Kazi ni msingi wa Maendeleo!
JKNYRR
Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekeee ya kujenga jamii iliyo sawa na Huru!

Siyo kila aniitaye nyerere ananipenda, adui wa ndani ni hatari kuliko adui wa nje! aluta contin...
 
Back
Top Bottom