Ubondia wa utotoni umenifanya mimi Deo kisandu kuwa imara kwenye Utu uzima.

Ubondia wa utotoni umenifanya mimi Deo kisandu kuwa imara kwenye Utu uzima.

yani katika watu wana stori kuzidi wote kisandu ni zaidi ya dokta shika
 
Uimara gani unaouzungumzia hapa wakati juzi nilisoma mada humu kwamba ulikoswa koswa kuchezea "kipande cha nyama ngumu".uimara unaujua kweli kweli wewe?
 
'..........Kuna wengine wabeba vyuma, na hawana Marinda..........Zilipendwaaa'
 
Kipindi cha utotoni kimenifanya kukumbuka mambo mengi sana, utotoni nimekulia mtaa wa watoto watukutu sana Wakiislam, Mtaa wa Kilima-Nyihogo hapa wilayani Kahama, mkoa wa Shinyanga. Kulikuwa na Mzee jirani na alipokuwa amepanga mama mzazi, nyumba hiyo ni kwa Mzee Khamis Seif, Mzee Khamis Seif alikuwa na watoto kama sijakosea watatu wa kiume, yule mtukutu sana alikuwa anaitwa MNELA na alikuwa mbabe sana utotoni.

Ilikuwa ni mwaka 1988 nikiwa na miaka 8 hivi, Nakumbuka tulisimama barabarani jirani na nyumbani kwa MAMA HINDU mtaa huo huo, basi watoto wakubwa wa Kiume wa Mama Hindu waakina BAI na KILONGE wakatuona tunarushiana vijembe, wakasogea karibu wakatuambia sasa mpigane tuone nani mbabe, Kilonge akachota mchanga chini akaweka viganjani kwake akasema haya pigeni mchanga, tukapiga mchaga ukamwagika chini kutoka viganjani, aisee MNELA nilimkung'uta makonde mpaka akakimbia kushitaki kwa baba yake, Mzee Khamis alicheka sana siku hiyo, jioni yake nikakutana tena na mtoto mwenzangu mwingine anaitwa MSAFIRI mtaa huo huo jirani na nyumbani kwa baba yangu mzazi, kaka yake EMANUEL akatupambanisha tena, aisee nilipiga isivyo kawaida mpaka kaka yake akatuamua.

Basi mimi nilikuwa najidai mwenzenu mtaa mzima wakaanza kuniogopa hasa vijana wa wakati huo tuko watoto, Mzee alipopata taarifa nilifokewa tabia ya kupigana na watoto wenzangu, basi Mnela akawa hataki tena kuwa na urafiki na mimi Deo Kisandu, nikabaki na marafiki wachache tu akina Sued Khamis na Baltazary(mwarabu). Mzee Kisandu babu yake na baba aliomba nipelekwe kijijini kabisa nikachunge ng'ombe ndipo nilipopelekwa kijiji cha ITUGUNHU ambako nilianza na shule ya msingi.

Nimegundua kuwa kumbe mimi ni BONDIA kabisa sema tu sijapata muda wa kufanya mazoezi ya kutosha, kule kijijini walinishika sana nikawa siwezi kufanya chochote, sasa ivi kwa kweli alhamdurilah ukinifanyia fyoko na kukunja kweli kweli. Kumbe asili huwa haitoki kabisa. Kuna haja ya kujua tabia za watoto wetu na jinsi ya kuzikontro maana anachokifanya utotoni kinaweza kuja kufanyika pia ukubwani.Mtoto wa kuwa karibu na baba mzazi kuna faida kubwa sana. Siku njema

Deogratius Nalimi Kisandu
2 januari 2018.
Sasa uliliwaje Tigo Mkuu? Wakat we ni bondia mzuri tu?
 
Tusi hili Mkuu.



hapana,Deo sasa amekuwa maarufu..japo haeleweki..

Ona..'weka bandiko/thread inayohusu kilimo/ujasiriamali/uchumi/ hata afya,utaona mwitikio wake..' watu hawachangamkii sana

sasa aje Deo.. 'aweke upupu wake...utaona RAIA wanavyojitahidi..kukoment

hapo ndio sasa inabidi 'uwe na akili kama za Deo..'

deo ni Brilliantly
 
Back
Top Bottom