MZIMU
JF-Expert Member
- Apr 29, 2011
- 4,058
- 1,373
Hali ya matumizi ya lugha ya kiswahili ilivyo sasa hasa kwa nchi ya Tanganyika, ambayo ndio inayotegemewa zaidi barani Africa kua ndio nchi inayoongea kiswahili fasaha, ipo hatarini hasa kutokana na vijana wetu wa muziki wa kizazi kipya na waandishi wetu wa habari ambao hupotosha maana na matamshi ya lugha hiyo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya bila wahariri wa vyombo vya habari kukemea au vyombo husika kama BAKITA, na vyenginevyo kuendelea kulizibia masikio jambo hilo.
Kwa mfano ni jambo la kawaida sana, kusikia maneno kama Tupogo, hakunaga, safali, biashala n.k , yakitumika bila kukemewa.
Wachangiaji mnaweza kutoa mifano mingine.
Hali hii isipo dhibitiwa, kiswahili kitakua lugha isio nathamani tena duniani pamoja na Jamii nyingi duniani kupenda kujua na kutumia lugha yetu adhimu.
Kwa mfano ni jambo la kawaida sana, kusikia maneno kama Tupogo, hakunaga, safali, biashala n.k , yakitumika bila kukemewa.
Wachangiaji mnaweza kutoa mifano mingine.
Hali hii isipo dhibitiwa, kiswahili kitakua lugha isio nathamani tena duniani pamoja na Jamii nyingi duniani kupenda kujua na kutumia lugha yetu adhimu.