Ubora wa Lugha ya Kiswahili " Kwishnei"

Ubora wa Lugha ya Kiswahili " Kwishnei"

MZIMU

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2011
Posts
4,058
Reaction score
1,373
Hali ya matumizi ya lugha ya kiswahili ilivyo sasa hasa kwa nchi ya Tanganyika, ambayo ndio inayotegemewa zaidi barani Africa kua ndio nchi inayoongea kiswahili fasaha, ipo hatarini hasa kutokana na vijana wetu wa muziki wa kizazi kipya na waandishi wetu wa habari ambao hupotosha maana na matamshi ya lugha hiyo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya bila wahariri wa vyombo vya habari kukemea au vyombo husika kama BAKITA, na vyenginevyo kuendelea kulizibia masikio jambo hilo.

Kwa mfano ni jambo la kawaida sana, kusikia maneno kama Tupogo, hakunaga, safali, biashala n.k , yakitumika bila kukemewa.

Wachangiaji mnaweza kutoa mifano mingine.

Hali hii isipo dhibitiwa, kiswahili kitakua lugha isio nathamani tena duniani pamoja na Jamii nyingi duniani kupenda kujua na kutumia lugha yetu adhimu.
 
Kwenye utunzi wa mashairi unaruhusiwa kutumia hata lugha ya isiyo rasmi.
 
Zamani kiduchu niliwahi kumsikia marehemu babu yangu akisema....

"Kiswahili ni lugha iliyozaliwa [COLOR=#FF000]Zanzibar[/COLOR]V,ikakulia [COLOR=#FF000]Tanzania[/COLOR],ikafia [COLOR=#FF000]Kenya[/COLOR] na kuzikwa [COLOR=#FF000]Uganda[/COLOR],mizimu yake ikatokomea [COLOR=#FF009]Kongo[/COLOR]"

Nilimshangaa sana mzee wangu na kuhisi umri unamwendesha kombo, loo kumbe uzee dawa.Leo siwezi bisha ule usemi wake....
 
Mzimu! Kwa maoni yangu umegusa "kansa" ambayo imefikia kiwango cha kutotibika. Ninadhani tukubali matokeo kuwa Lugha yetu adhimu, Kiswahili, inapitia kipindi cha mpito kitakachopelekea kupatikana kwa Lugha nyingine kabisa, kama ambavyo Lugha yenyewe ya Kishwahili ilivyoanza.

Juzi hapa hapa JF kuna Mdau amemrekebisha Mchangiaji kuwa lugha sahihi ni "hela" na sio "ela", "halafu" na sio "alafu", "hebu" na sio "embu" n.k. na alichoambulia ni matusi. Wachangiaji ni Wasomi watarajiwa wa Nchi hii. Hiki ni Kizazi ambacho hakiwezi kuandika na kuongea lugha yoyote kwa ufasaha iwe Kiswahili au Kiingereza.

Umetaja Wadau na Makundi kadhaa yenye dhamana ya kukilinda Kiswahili yaani Wanamziki wa Mziki wa Kizazi Kipya (ambao wengi wao hata Elimu ya Kidato cha Nne hawana, kilihitimu Elimu hiyo ni majina tu), Waandishi wa Habari, Wahariri, Vyombo vya Habari na BAKITA (ambao naamini wamediwa nguvu na wako Dar tu, Mikoani hawajulikani). Ninaomba, kwa uchungu sana, kwenye watu na Taasisi wanaoongoza katika kuchefua Kiswahili, tumtaje Mh. Rais, Baraza la Mawaziri (ukiondoa Mh. Waziri Mkuu na baadhi ya Mawaziri wachache sana) na Bunge lote kwa ujumla wake, kwa kasumba zao mbaya za kuchanganya Kiswahili na Kiingereza!

Binafsi, ninapenda sana kuwasikiliza
watu kama Mwl. Nyerere (Marehemu), Dr. Salim A. Salim, Jaji Warioba, Dr. Shein, Mzee Mwinyi, Mzee Chissano, Dr. Magufuli, Dr. Mwakyembe, Dr. Migiro, Prof. Tibaijuka, Dr. Slaa, Prof. Shivj, Mh. (Dr?) Lissu na wengine wachache ambao hawalazimishi wasikilizaji wao kuwatambua kama Wasomi kwa kuchanganya Kiswahili na Kiingereza.

Umewahi kumsikiliza "Mh. Rais" wa TFF? Umewahi kuangalia na kusikiliza EATV (TV ya Vijana)?
 
Ni makusudi kabisa inayofanyika ili kukitoa Kiswahili katika lafdhi za Kiarabu, kuna upotoshaji wa kuwa Kiswahili kikibaki katika lafdhi za Kiarabu inakuwa ni lugha ya Waislaam.
 
Hali ya matumizi ya lugha ya kiswahili ilivyo sasa hasa kwa nchi ya Tanganyika, ambayo ndio inayotegemewa zaidi barani Africa kua ndio nchi inayoongea kiswahili fasaha, ipo hatarini hasa kutokana na vijana wetu wa muziki wa kizani kipya na waandishi wetu wa habari ambao hupotosha maana na matamshi ya lugha hiyo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya bila wahariri wa vyombo vya habari kukemea au vyombo husika kama BAKITA, na vyenginevyo kuendelea kulizibia masikio jambo hilo.

Kwa mfano ni jambo la kawaida sana, kusikia maneno kama Tupogo, hakunaga, safali, biashala n.k , yakitumika bila kukemewa.

Wachangiaji mnaweza kutoa mifano mingine.

Hali hii isipo dhibitiwa, kiswahili kitakua lugha isio nathamani tena duniani pamoja na Jamii nyingi duniani kupenda kujua na kutumia lugha yetu adhimu.
Kwisnei na maneno mengine kama hayo yanaharibu kiswahili
 
Ni makusudi kabisa inayofanyika ili kukitoa Kiswahili katika lafdhi za Kiarabu, kuna upotoshaji wa kuwa Kiswahili kikibaki katika lafdhi za Kiarabu inakuwa ni lugha ya Waislaam.

nani anafanya hayo makusudi? Wakatoliki ndio wanawafundisha watu hayo uyasemayo?................... Kadri siku zinavyoenda weledi wako unazidi kuingia mashaka....hata sijuhi sababu ni nini?.................. nilitegemea mchango wa maana sana kutoka kwako
 
Hali ya matumizi ya lugha ya kiswahili ilivyo sasa hasa kwa nchi ya Tanganyika, ambayo ndio inayotegemewa zaidi barani Africa kua ndio nchi inayoongea kiswahili fasaha, ipo hatarini hasa kutokana na vijana wetu wa muziki wa kizani kipya na waandishi wetu wa habari ambao hupotosha maana na matamshi ya lugha hiyo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya bila wahariri wa vyombo vya habari kukemea au vyombo husika kama BAKITA, na vyenginevyo kuendelea kulizibia masikio jambo hilo.

Kwa mfano ni jambo la kawaida sana, kusikia maneno kama Tupogo, hakunaga, safali, biashala n.k , yakitumika bila kukemewa.

Wachangiaji mnaweza kutoa mifano mingine.

Hali hii isipo dhibitiwa, kiswahili kitakua lugha isio nathamani tena duniani pamoja na Jamii nyingi duniani kupenda kujua na kutumia lugha yetu adhimu.

Mzimu kazi ya kuhakikisha kiswahili kinaendelea kuwa hai ama kufa ni ya BAKITA,kina Ommy Dimpoz na wenzake wanaangalia maslahi zaidi...waimbe mashairi isipokula kwao!
 
Majiji wakimaanisha cities, tangazo hizi limesababishwa na , wakimaanisha limeletwa kwenu na, mjini kati wakitafsiri directly neno town centre, etc
 
Maneno mengine yanayo udhi kuyasikia ni kama haya:- Mdada, Mbaba, Mmama, Mkaka n.k. Mpaka hapo BAKITA, na Wahariri wa Magazeti bado wapo kimya tu.
 
Zamani kiduchu niliwahi kumsikia marehemu babu yangu akisema....

"Kiswahili ni lugha iliyozaliwa [COLOR=#FF000]Zanzibar[/COLOR]V,ikakulia [COLOR=#FF000]Tanzania[/COLOR],ikafia [COLOR=#FF000]Kenya[/COLOR] na kuzikwa [COLOR=#FF000]Uganda[/COLOR],mizimu yake ikatokomea [COLOR=#FF009]Kongo[/COLOR]"

Nilimshangaa sana mzee wangu na kuhisi umri unamwendesha kombo, loo kumbe uzee dawa.Leo siwezi bisha ule usemi wake....

Ni kweli aliyosema babu yako wala hajakosea,lkn sasa tz tumekuwa wa kwanza kukiharibu
 
Ni makusudi kabisa inayofanyika ili kukitoa Kiswahili katika lafdhi za Kiarabu, kuna upotoshaji wa kuwa Kiswahili kikibaki katika lafdhi za Kiarabu inakuwa ni lugha ya Waislaam.
duh ndugu kila kitu wewe unaambatanisha na udini tu,kiswahili kinazungumzwa na wengi wasio waislam na waislam pia na haitatokea hata siku moja kuwa ni lugha ya waislamu...NAKUKUMBUSHA TU:dini utaiacha hapahapa duniani,,Mungu hana dini na hatokaa awe na dini hata siku moja.
 
duh ndugu kila kitu wewe unaambatanisha na udini tu,kiswahili kinazungumzwa na wengi wasio waislam na waislam pia na haitatokea hata siku moja kuwa ni lugha ya waislamu...NAKUKUMBUSHA TU:dini utaiacha hapahapa duniani,,Mungu hana dini na hatokaa awe na dini hata siku moja.

Ungenisoma vizuri, ungeona hiki:

kuna upotoshaji wa kuwa Kiswahili kikibaki katika lafdhi za Kiarabu inakuwa ni lugha ya Waislaam.

Sijui unaelewa Kiswahili?
 
Kwisnei na maneno mengine kama hayo yanaharibu kiswahili

Hili neno "kwishnei" nimeliweka ili kuonyesha ukubwa wa tatizo ulivyo, ila nimeliweka kwenye mabano kuonyesha kua sio neno la kiswahili moja kwa moja.
 
Hili neno "kwishnei" nimeliweka ili kuonyesha ukubwa wa tatizo ulivyo, ila nimeliweka kwenye mabano kuonyesha kua sio neno la kiswahili moja kwa moja.


Hata hizo alama za uandishi ("....." ) *funga,fungua semi*, unazoziita mabano nao ni upotoshaji upotoshaji na uharibifu wa lugha yetu.....!!
 
Back
Top Bottom