Ubovu wa Katiba kumuondoa madarakani naibu wa Rais Kenya

Ubovu wa Katiba kumuondoa madarakani naibu wa Rais Kenya

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Ni baada ya kuonekana akimuhujumu Rais, akihubiri na kuchochea chuki na migawanyiko ya kisiasa yenye mirengo kikabila na upendeleo wa watu wa kabila na eneo lake la Milima Kenya.

Naibu wa Rais amekiuka sheria na misingi ya kikatiba ya Kenya ya kua nembo ya umoja wa Taifa na kiunganishi cha umoja wa Kenya. Badala yake Naibu Rais huyo wa Kenya, Rigathi Gachagua a.k.a RigGy ameonekana akichochea chuki na migawanyiko serikalini na kumlaumu Rais kwa kuwajumuisha waKenya wa maeneo mengine kwenye serikali anayodai eti hata hawakuchangia vya kutosha kuipata wakati wa uchaguzi 2022.

Kwa katiba mbovu ya Kenya, hiyo inatosha, na ni miongni mwa sababu muhimu zitakazo tumika kumg'oa naibu huyo wa Rais mamlakani.

Na kwasasa, joto la kisiasa liko juu mno, ubabe wa kisiasa na vitisho vya wazi wazi, usaliti wa kambi moja na nyingine, malumbano ya kuhujumiana na kuihujumu serikali kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na kuligawa Taifa kwa misingi ya kikabila na maeneo, utadhani kuna uchaguzi wiki ijayo. Joto la kisiasa ni kali mno. Hakuna kuaminiana tena.

Mbaya zaidi hata ngome yake Naibu wa Rais ya huko Mount Kenya wamegawanyika na tayari wengine wanaunga mkono hatua za kitaka kumbandua. Wengi wadai amejitakia mwenyewe, huku ngome za Rais kote nchini zikiungana na wale wa upinzani waliojumuishwa serikalini ambao naibu wa Rais ndio hasa anawananga, na kuapa kumbandua naibu huyo wa Rais ndani ya kipindi kisichozidi wiki mbili zijazo.

Prof. Abraham Kithure Kindiki waziri wa mambo ya ndani kenya, na Govenor wa County ya Laikipia Anne Waiguru wanatajwa kurithi nafasi hiyo, endapo singombingo hii ya kabokamchizi itafanikiwa.

Je, huu ni usaliti? Au ni miongoni tu mwa athari za ubovu wa katiba ya Kenya au maandalizi ya mapema ya uchaguzi wa 2027?

Je, Naibu wa Rais wa Kenya ndugu Rigathi Gachagua, anaweza kunusurika kwenye jaribu hili la kikatiba linalomzonga, na Kenya itakua na sura gani baada ya hapo?🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Lete hicho kifungu cha katiba kitakachomwondoa Mwamba Gachagua? 😄

150. Removal of Deputy President​

1) The Deputy President may be removed from office--

(a) on the ground of physical or mental incapacity to perform the functions of the office; or
(b) on impeachment--

(i) on the ground of a gross violation of a provision of this Constitution or any other law;
(ii) where there are serious reasons to believe that the Deputy President has committed a crime under national or international law; or
(iii) for gross misconduct.

(2) The provisions of Articles 144 and 145 relating to the removal of the President shall apply, with the necessary modifications,to the removal of the Deputy President.

Tayari sahihi za wabunge zimekusanywa na akidi tayari imetimia kuupa nguvu muswada huo binafsi, ambao unapaswa tu kuungwa mkono na zaidi ya robo tatu ya wabunge, kumbandua na kumpeleka msema kweli huyo na mwamba wa Nyeri nyumbani :pulpTRAVOLTA:
 
Ni baada ya kuonekana akimuhujumu Rais, akihubiri na kuchochea chuki na migawanyiko ya kisiasa yenye mirengo kikabila na upendeleo wa watu wa kabila na eneo lake la Milima Kenya...
Mbona wanasema Kenya wana better katiba na domokrasia pia?
 

150. Removal of Deputy President​

1) The Deputy President may be removed from office--

(a) on the ground of physical or mental incapacity to perform the functions of the office; or
(b) on impeachment--

(i) on the ground of a gross violation of a provision of this Constitution or any other law;
(ii) where there are serious reasons to believe that the Deputy President has committed a crime under national or international law; or
(iii) for gross misconduct.

(2) The provisions of Articles 144 and 145 relating to the removal of the President shall apply, with the necessary modifications,to the removal of the Deputy President.

Tayari sahihi za wabunge zimekusanywa na akidi tayari imetimia kuupa nguvu muswada huo binafsi, ambao unapaswa tu kuungwa mkono na zaidi ya robo tatu ya wabunge, kumbandua na kumpeleka msema kweli huyo na mwamba wa Nyeri nyumbani :pulpTRAVOLTA:
Kama ndivyo vifungu vinavyohusika mbona hao jamaa ni kama wana akili timamu!
Katiba za serikali za kijinga hazina uwazi kama huo!
 
We chawa unafikiri Kenya ni kama huku kwetu? Kurta ama
haya mambo mazito hayahitaji mihemko gentleman, ni ya kibovu mno, ikiwa juna utulivu, kichwa maji au wa kukurupuka huwezi elewa mambo haya muhimu Africa Masharaki :pedroP:
 
Itatuathiri vipi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa?
labda hiyo ungecheki kwenye mjadala wa athari watakazopata chadema lwenye uchaguzi huo baada ya usaliti wa wananchama wao kujitokeza kwenye maandamano haramu yaliyokua yamepigwa marufuku na polisi:pulpTRAVOLTA:
 
Kama ndivyo vifungu vinavyohusika mbona hao jamaa ni kama wana akili timamu!
Katiba za serikali za kijinga hazina uwazi kama huo!
kwahiyo anabanduliwa uongozini na wanao mtetea si timamu, right?

au watu wanao kiuka au kuvunja sheria kwa kujua au kuto kujua sio timamu?:pedroP:
 
Mbona wanasema Kenya wana better katiba na domokrasia pia?
kusema wanaweza kusema sana tu, lakini kiuhalisia ni dhahiri shahiri hilo ni tatizo kubwa mno kenya na inaonekana wazi na kila moja anaona:pulpTRAVOLTA:
 
Wameweka wazi taratibu za kumng'oa madarakani. Vigezo vikitimia wamng'oe tu!
kwahiyo anabanduliwa uongozini na wanao mtetea si timamu, right?

au watu wanao kiuka au kuvunja sheria kwa kujua au kuto kujua sio timamu?:pedroP:
 
Kumtoa Naibu ni sawa na kumtoa Rais, they can't play with fire like that
hata raisi anaweza kutolewa pia, na upo utaratibu wake. Na sio syla la mchrzo au mzaha muswada uko bungeni.

na kwa hali ilivyo ni afadhali muswada ukafanikiwa. Imagine ukafeli, kweli kutakua na kazi za pamoja baina ya Rais na Naibu wake Kenya ama kutakua na serikali mbili hasimu?

katiba, katiba, katiba ni mbovu,
kumbuka,
kiuhalisia muswada huo hauwezi kupelekwa bungeni bila idhini ya Rais,

Na ingalikua si hivyo angekemea naibu wake kubanduliwa. Kukaa kwake kimya ni kwamba hana haja na huyo msaidizi wake muhimu serikalini:pulpTRAVOLTA:
 
Mkuu kwa hii tabia si hata ukiwa mazoezini unammwagia sifa kede kede huyo Daktari wako
kusema ukweli ni sifa nzuri na muhimu sana kwangu.

Na kwakeli siwezi kuacha kusema ukweli hata mara moja gentleman bila kujali mbambamba yoyote 🐒
 
Back
Top Bottom