Ubovu wa product ya Mo ukwaju

Tuanze na ww umebuni nn kizuri apo ulipo na kikajulikana


unamwalibia mwenzako biashara hujui apo adi TBS wamepitamo, Tanzania tunajua kuponda badala ya kuweka mawazo ili aboreshe nn apunguze nn kwa bidhaa.
Inamaana ukiona kitu kibaya usiseme kisa mwenye product atakasirika? Atajirekebishaje sasa??? Mo vinywaji vyake vingi anaiga azam hlf vibaaaayaa...
 
Kiukweli kasumba hii ya Mo kuiga bidhaa kutoka kwa bakharesa jamaa anayo saana sijui hana washauri??
 
Isije kuwa hasira za wanayanga tu. Muombeni atawasaidia tu.
 
Niliwahi kunywa mo passion ya ml_500, niliumwa wiki nzima

Toka hapo niliapa kutotumia bidhaa na vilaji vya huyo kiumbe
Mkuu mimi nikikunywa hiyo Mo Passion aise kooni nilihisi nimemeza mkojo wa punda ni kali kweli kweli sielewi watu wanaipendea nini.
 
Kaka shoe shiner wa mo. Nimegonga ikulu? Pole sana ila huo ndoo ukwe
Wee n mtazamo wako cema usipende kuaribu biashala za wanaume... Ikiwa kwenu akna history ata ya kiwanda cha ugoro
 
Kwanini MO anapenda kuiga iga kila bidhaa ya Bakhressa ?
 
Mo bidhaa karibu zote lazima akopi kutoka Azam..huwa hana mbinu za kuanzisha kitu
 
Acha waendelee kushindana tu ili fursa ziendelee kupatikana kwa raia.

Miti ya ukwaju kwa sasa ni deal huko Shinyanga na Tabora,miti inalipiwa kabla hata ukwaju haujakauka au kukomaa mitini.

Siku hizi kuna kangomba hadi kwenye mikwaju ilhali ilikuwa miti isiyo na thamani kihivyo ikikatwa mkaa hovyo.

Wataalamu watafiti waje na mbegu za muda mfupi mikwaju iwe zao la biashara kama korosho.
 
Humu watakua wamejaa washabiki wa yanga na Simba, naona mtifuano unaendelea
 
Hiyo MO ni flavoured drink sio ukwaju halisi...
ndo mana hata bei ni kidogo cheap...!!

Ila bakhera kuanzia embe, ukwaju, chungwa na nanasi anakamua mwenyewe just anaongeza CMC tu kwa baadhi ya juice kuifanya juice iwe nzito...
 
Watanzania siku tukiacha huu ujinga na upuuzi, tunaweza kupiga hatua toka kwenye mkwamo huu tulionao, mtu unaamka kutoka usingizini unawaza kuandika ujinga wakati mwanaume mwenzako anajaribu kufanya kila kilicho kwenye uwezo wake ili kujiongezea utajiri kwa ajiri yake na familia yake. Ngozi nyeusi sijui tuna matatizo gani, mtu anaandika story utafikili ana miliki chochote cha maana!! Eti mtu anajisifu chupa ya maji kubebeka?!! Bado tuna safari ndefu.
 
Ukajua kila mmoja atakupenda?

Bila watu kama sisi hawawezi kuona makosa yao, wewe endelea kusifia kila kitu chao kwani ubaya uko wapi tukiwa makundi mawili.

Hauwezi kuwafanya watu utakavyo ila watu watakufanya watakavyo.
 
Mo anasubiri Bakhresa atoe kitu kipya ili na yy aige.
dah!!..kweli mkuu mjomba bakhresa katoa apple punch moo kaja na moo apple mule mule..sema anapopigwa goli ni kwamba bidhaa za azam zipo na quality mnooo,,kwanzia ladha na packaging ni international..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…