Ubovu wa stendi ya mabasi Kigamboni Feri: Watumiaji wamtaka "RC Makeke" Chalamila awakwamue

Ubovu wa stendi ya mabasi Kigamboni Feri: Watumiaji wamtaka "RC Makeke" Chalamila awakwamue

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725
1741962108870.png

1741961846067.png

RC Chalamila

Nimesafiri kutoka kwetu "Sumbawanga Town" nikaja Dar kumsalimia bibi huko Gezaulile Kigamboni.

Kutoka Posta nilipitia Feri nikapanda pantoni, kisha basi kwenye kituo cha manasi cha Kigamboni Feri.

Taarifa nilizokutana nazo ni kwamba watumiaji wa stendi ya mabasi Kigamboni Feri wanamtafuta "RC Makeke" Chalamila awatembelee.

Ukitoka kwenye pantoni kuelekea Kigamboni lazima upande mabasi, boda na bajaji zinazopaki stendi ya mabasi Kigamboni Feri.

Vivyo hivyo, ukitoka Kigamboni kati kwa mabasi, boda na bajaji na unataka kuvuka kuelekea Posta Mpya lazima ushuke stendi ya mabasi Kigamboni Feri.

Sebule za pantoni abiria wanakosubiria usafiri zinavutia.

Lakini stendi ya mabasi Kigamboni Feri imejaa uchafu, makorongo, msongamano na uvundo.

Wananchi waloongea nami wanasema kuwa imani yai ni kwamba "kama yule RC makeke aitwaye Chalamila akitutembelea Kigmboni tunaweza kuamka."

Nimechukua picha moja kuonyesha hali ya stendi ya mabasi Kigamboni Feri ilivyo.

Msongamano wa mabasi ni mkubwa. Ushuru unakusanywa. Lakini maboresho hakuna.

Ni kama dhana ya mipango miji haifahamiki kwa viongozi wa serikali huko Kigamboni, tena mita 300 kutoka Ikulu ya Magogoni.

Huu ni ujumbe kwako "RC Makeke" wa Dar es Salaam.

Mjumbe hauwawi.
 
dah aisee ni kweli kabisa hilo eneo kabla halijawa stand palikua pazuri tu wangetakiwa kabla hawajaweka stand wapatengeneze vyema ndipo waifungue stand sijui viongozi wetu na wasomi wetu wanawazaga nini huko maofisini
 
Back
Top Bottom