Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo

Mkuu tafuta pesa ndio ugombee uchaguzi ccm.
Unamaanisha na mimi ninunue uongozi?. No!.
Mimi ni muumini wa ukweli na uwazi, siamini katika wanunua uongozi kwa pesa!.
Pesa tuu zenyewe za fomu, nimefanya kuchangiwa na wana JF!.
CCM wanakwenda vizuri maana hata huko Kenya hakuna maskini ameshinda uchaguzi Wala kugombea..

Maskini watakuwa kama Magufuli wataharibu kila kitu na kujisifu kwa wajinga na cheap politics.
Naendelea kusisitiza, sifa ya uongozi ni uzalendo, uwezo wa uongozi na kukidhi vigezo na isiwe pesa!.
P
 
Tuna Imani na mwenye pesa sio kununua uongozi..

Wewe ukiwa na njaa zako utatuletea disaster
 
Paskali nakusoma ila kilicho dhahiri ni kwamba CCM huijui vizuri na pia "rules of the game" huzijui!

Unachofanya kwenye maandishi yako toka mchakato wa kuchukua fomu ni kama umeingia kutafuta habari lakini si kushindana ili kupata nafasi hiyo!

Ushauri unaotoa ni sawa na Mwanafunzi anayejitungia Mtihani na kuufanya na kumtaka Mwalimu wake ampasishe!

Sikukatishi tamaa ila naona kwa strategy zako na namna unavyo vibrate Mimi naona umeshashindwa hata kabla game haijaanza!

Ninachosubiria kutoka kwako ni kilio kireeeefu katika Makala zako baada ya zoezi hili kukamilika.
HAUKO OBJECTIVE !

Mwisho ni kwamba Paskali wengi humu ni mediocres hawawezi kukushauri na kuku-mentor kwa ajili ya ku- aspire political posts kama hizo, mwishowe utakuwa tu permanent loser!

Kiukweli ni kwamba Paskali Mayalla wewe ni msomi lakini bado kuna ka ushamba fulani ka kisukuma bado kana ku- pull backward!

Kwa summary ni kwamba wewe Paskali Mayalla ni clever but not intelligent!
Nafasi za siasa zinataka watu intelligent na si watu clever!
 
Hahahhahaa imebidi tu nicheke...umeamua umchane tu ukweli....paskali mdomo ndio unaomsumbua...unadhani magufuli alivyokuwa anatafuta public figures walio royal kwake, paskali wasingemchukua? Kama kabudi alichukuliwa, iweje paskali? Aliachwa na ndugu yake kisa mdomo

Sent from my SM-T585 using JamiiForums mobile app
 
Paskali nakusoma ila kilicho dhahiri ni kwamba CCM huijui vizuri na pia "rules of the game" huzijui!.
Mkuu Fumadilu Kalimanzila, kwanza asante, nikushukuru Kwa kunieleza ukweli mchungu ila ndio ukweli wenyewe, mtu ni mwanachama wa CCM, umezaliwa CCM, umekulia CCM, ukajidhania unaijua CCM, akitokea mtu akakuambia huijui CCM, ina maanisha mimi ni mtu niliyejidhania nijajua, kumbe in reality ni sijui kitu!. Akitokea mtu akakuambia hujui, muombe awe Mwalimu wako akufundishe ili sasa ujue, hivyo Mkuu Fumadilu Kalimanzila, nakuomba uwe mwalimu wangu kwenye hili.
Unachofanya kwenye maandishi yako toka mchakato wa kuchukua fomu ni kama umeingia kutafuta habari lakini si kushindana ili kupata nafasi hiyo!
Msemakweli ni mpenzi wa Mungu, nilipojaribu Kawe, I was not serious, but I got some lessons on how dirty games people play to get elected, I decided to try but clean, simjui mtu yoyote, simtafuti godfather yoyote, na sitoi senti tano kwa yeyote, kwasababu I believe in me kuwa CV yangu, experience na exposure itanibeba, lakini kama nitajinjwa kwasababu ndani ya hao 186, mimi naweza kuwa ni sawa na sisimizi, I'll do nothing to push na kujiandaa kupokea matokeo.
Ushauri unaotoa ni sawa na Mwanafunzi anayejitungia Mtihani na kuufanya na kumtaka Mwalimu wake ampasishe!
Duh...!
Sikukatishi tamaa ila naona kwa strategy zako na namna unavyo vibrate Mimi naona umeshashindwa hata kabla game haijaanza!
Asante pia kwa taarifa hii maana huku ni kuniandaa kisaikolojia kuyakubali matokeo, hivyo whatever the outcome will be, the impact won't be devastating kuliko ningeendelea kuwa na the great expectations halafu nikala mweleka nitakuwa na great despair.
Ninachosubiria kutoka kwako ni kilio kireeeefu katika Makala zako baada ya zoezi hili kukamilika.
HAUKO OBJECTIVE !
It's expected nikikatwa I'll make lot's of noises!. I won't!. Uchaguzi ni Bunge la November, hivyo between now and November, I'll shout, and shout and shout ili wakituteulia makorocho, tutasema ni makorocho!.
Mwisho ni kwamba Paskali wengi humu ni mediocres hawawezi kukushauri na kuku-mentor kwa ajili ya ku- aspire political posts kama hizo, mwishowe utakuwa tu permanent loser!.
Duh...!.
Kiukweli ni kwamba Paskali Mayalla wewe ni msomi lakini bado kuna ka ushamba fulani ka kisukuma bado kana ku- pull backward!.
Hii ni kweli, kiukweli sijui ni kwanini sisi Wasukuma tunakuwaga washamba!.
Kwa summary ni kwamba wewe Paskali Mayalla ni clever but not intelligent!
Nafasi za siasa zinataka watu intelligent na si watu clever!
Asante kwa kuniambia udhaifu huu na naomba unifundishe tofauti ya mtu clever na intelligent. Baada ya kusoma Iliboru na kupata LL.B Hons, UDSM, nilijihesabu intelligent kumbe ni clever tuu and not intelligent!. Nifanye nini niwe intelligent nifanikiwe?.
P
 
Duh...!. Kiukweli nasali sana Mungu anifundishe kunyamaza!, kiukweli mdomo umeisha niponza kwa mengi, kitu kizuri kuhusu mdomo wangu ni unasema kweli tupu!, hivyo ukihukumiwa kwa kuusema ukweli mchungu, siku zote mwisho wa siku Mungu huwa anakufidia.
Hivyo wakati nikisubiria jinsi Mungu atakavyo nifundisha kunyamaza, at the moment sinyamazi mpaka nitakapo nyamazishwa, na kwa vile hapa duniani sote tuko safarini, ni watu wa kupita tuu, hivyo nitaendelea kuusema ukweli na kuteseka kwa mateso ya muda tuu ya dunia hii, kisha kuja kupata raha ya milele kule mbinguni maana sisi wakweli wote siku ya siku ni straight mbinguni!.

Pamoja na mimi kuwa mkweli, sometimes mkweli too much, lakini bado ninaendesha mafunzo kwa wengine ili yasije wakuta yaliyo nikuta!. Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa?
P
 
Ndugu yangu Paskali Mayalla kwanza nikupongeze kwa uungwana wako!
Nimeamka muda huu (saa nane usiku) kuingia kazini kwangu nikakuta ume- respond vizuri sana kwa maoni yangu niliyokupa!

Kwa kweli nimefurahi na nimekubali kweli wewe ulikuwa " Mtoto wa Nyoka" ila uliharibiwa tu na Mazingira fulani uliyojiweka au kukutana nayo katika Makuzi yako ( Rejea hotuba ya Makongoro Nyerere mbele ya Rais Hussein Mwinyi kuhusu Mauzauza aliyonayo leo), otherwise nawe ungekuwa " Nyoka" kama Marehemu Baba yako na si " Mjusi " kama ulivyo leo!

Kiukweli wewe ni Mwanafunzi Bora kwani unafundishika na hushupazi shingo kama wapu.mbavu fulani humu!

Nakutakia kila la kheri ktk nyendo (endeavors) zako Ndugu yangu!

Kwakuwa umeniomba mambo mengi na mimi niko tight katika games zangu naomba nianze kwa kukufungua kuhusu tofauti ya mtu clever na mtu intelligent!

Nenda hata kwenye Oxford Dictionary na usome " between lines" utaona kuwa;
"A clever person is somebody "quick " at learning and understanding......, Jitu Clever linaweza kukesha na kuweka miguu kwenye karai la maji baridi "kumeza"/kukariri mambo na likapata ma A+ yote lakini ni debe tupu!

Masomi yetu mengi ni ya hivyo, ni ma - clever people!
Uthibitisho ni kuwa mengi hayana pesa wala madaraka makubwa kisiasa na mengi huwa yanasubiri kuteuliwa na " intelligent people"! ( Soma hata Kitabu cha Robert Kiyosaki, Titled: Why "C" Students employ "A" Students?).

Ndio maana hata wewe Paskali Mayalla as a " Clever person" not an " Intelligent person" unataja sana vitu kama Ilboru ,ufaulu wa LLB Hons na madubwasha mengine kama kujua kuongea kiingereza fasaha n.k!

Intelligent people huwa hawataji hivyo vitu hata kama wanavyo kwani wanajua hizo ni necessary inputs tu, wao akili zao ziko kwenye outputs (matokeo) tu! Ma- intelligent people ni " Makaverians" - End justfy means"!

Sasa Intelligent person ni nani?!
Rudi tena kwenye Oxford Dictionary na usome between lines utaona kuwa,An Intelligent person is somebody "good" nasisitiza not " quick" ! Nasema tena Somebody good at learning, understanding and reasoning at a logical way....!
Paskali Mayalla unaona tofauti hapo?!
Lazima utulie na usiwe na ubishi au akili ya ushabiki wa Simba na Yanga au akili ya Kubet ndo utaelewa hiyo kitu!

Intelligence Bureaus zote Duniani kama vile KGB, MOSSAD, MLS, FBI, Scotland Yard, nadhani hata TISS hapa kwetu huwa hawatafuti " Clever people" bali utafuta " Intellligent people" na ndo maana zinajiita " INTELLIGENCE BUREAUS"!

Hizi huchukua hata watu waliopata matokeo ya Division O kabisa given they are intelligents!

Naweza kwenda mbali na kukupa mifano katika wanasiasa tulionao pia ili uone tofauti hiyo vizuri!
Lowassa ni Clever ( Inasemekana ndo mtu wa kwanza Tanzania kuandika A+ ktk matokeo ya somo la History Form 6, enzi hizo akisoma Milambo Sekondary - Tabora na akina Richard Mabala ( Mzungu, Mzee wa Makengeza, Mabala the Farmer au Auther wa Hawa the Bus Driver).
Jakaya Kikwete ni Intelligent Person, Inasemekana ali- graduate na degree ya " Makarai" pale UDSM ktk masomo yake ya Economics, enzi hizo wakiwa na akina Profesa Haruna Lipumba ( li- Clever Person kingine ) !

Mwigulu L.Nchemba ni Clever Person !
January Makamba ni Intelligent person!
Kwa sasa naomba niishie hapa , kama utakuwa umepata mwanga kidogo basi sawa, details zingine fuatilia mwenyewe!
Karibu sana Mwanduhitinje huku kwetu Meatu!
 
Wewe ni mzalendo?
 
Kwa hiyo ni kama hujui mtindo wa chama chako ama?

CCM kuanzia anayegombea hadi anayepiga kura akili zao sawa.

Mjumbe hapigi kura bila mlungura.
Mgombea huwezi kupita bila kutoa mlungura.

Nimesema MLUNGURA sijasema rushwa. Lakini umeelewa.

Halafu huo uzalendo unaosema utapatikanaje wakati watanzania wote wanajua ukiwa fisadi hufungwi zaidi ya kuendelea kupata neema za uteuzi?
 
Wewe ni mzalendo?
Mkuu MKANDAHARI , hili sasa ndio swali gani?!. Mtu ni Mzalendo wa kweli wa taifa hili na uzalendo wake unafahamika wazi, sio wakutafuta kwa tochi!, unaonekana ,wazi na unajulikana wazi wazi kabisa sio wa kutafuta au wa kumulika kwa tochi, ili uonekane, unamuulizaje kama ni Mzalendo?!. Au umeuliza tuu ili niseme mimi ni Mzalendo na uzalendo wangu ni huu...?.
No please!.
P
 
Paskali una mkosi sana. Kila unapogusa sasa pananuka. Sasa umegeukia huku. Sawa ngoja tuone
 
Sisiemu hakujawahi kuwa na Mzalendo, Mwalimu mwenyewe alisigina hilo, dhambi ya usaliti dhidi ya wazee wapigania uhuru idumu milele

. Cc Mohamed Said
 
Pambana ndugu, kupita hapo inahitaji juhudi haswa
Mkuu Proved , mimi ni muumini, naamini viongozi wazuri huletwa na Mungu na wala sio juhudi binafsi au kupambana!.

Kinachotakiwa ni kitu kimoja tuu, kama una sifa na una kidhi vigezo, ni kutangaza nia kwa kujaza fomu kuomba, kama ni wewe, then ni YEYE mwenyewe ndiye atakupambania.
P
 
Paschal Mayala ni Clever person!
Mkuu Akasankara, naomba usinivimbishe kichwa bure, kiukweli I'm not clever, mimi ni mtu mwenye akili ya average, sijawahi kupata divisheni 1 hata mara moja.

Ila pia kuna baadhi ya mambo, hayawahitaji watu vipanga sana, mfano fani
Sheria, wale vipanga wenye 1st Class, sijawahi kusikia wakishinda kesi yoyote!.

Fani nyingine usiyohitaji vipanga ni uongozi. Viongozi wazuri, hawahitaji kuwa vipanga sana, uongozi unahitaji mtu kuwa strategic
P
 
Karibu
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…