Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Mimi bado nasheherekea kushindwa kwa CCM.
Imekuwaje tukasau kuweka picha ya hawa wapiganaji?


chadema_mwera_heche.JPG


Huyu ndiye mbunge mpya wa Tarime Mh. Charles Mwera (kushoto) akiwa na diwani mpya wa jimbo hilo Mh. John Heche




Picha ni kwa hisani ya Michuzi website
Mrithi wa chacha wangwe



.

mkuu lazy dog (mbwa mvivu ha ha ha),

angalia link yako ya picha uiweke tena vizuri maana picha haionekani hapa
 
Ni kweli CCM huwezi kuilinganisha na chama chochote hapa Tanzania kwa sababu ndicho kimepewa nafasi ya uongozi kikashindwa. Wala rushwa wanapeta, wezi wanatanua, wahujumu uchumi ruksa......looo dola imekwenda usingizi na kamanda anatalii. Hao CCM wenye uchungu wako wapi ? Ndugu zangu Ladslaus, Bibi ntilie, Gembe, Masatu, Mtanzania, Fairplayer na wengine wengi tu, mko wapi na haya hamyaoni. FMES ameweza kuyaona mengine lakini kasahau kimoja muhimu - the buck stops with the President.



Neno moja moja hunipiga chenga, ila hapo sentensi nzima nimetoka kapa.
Imebidi kutafuta msaada kwa marafiki.



.
 
ameuliza swali ambalo tungemuuliza yeye, kama walikuwa wanajua jimbo la Tariime lisingebadilisha mwelekeo wa Bunge (siyo kama Bunge lilikuwa linategemea kiti kimoja kuvunja a tie), sasa kwanini hata walishiriiki uchaguzi? Si ingekuwa bora kama wangewaacha wapinzani wachuane wenyewe!?
 
Naomaba niulize hayo matumizi ya helkopta na misururu mikubwa ya magari yalipitishwa bila ya yeye kuwa na taarifa na kukaa chini na kujadili bajeti nzima ya kuendeshe hilo suala likiwa kumanipulate a sensitive organ in the govt like the police force?
Nitakubali kuwa Msekwa he is a man of the people and can not very nuch be compared to other crooks in CCM like Makamba ila yeye kama makamu Mwenyekiti wa CCM alikuwa na uwezo wote wa kuangalia hilo suala na kuaddress.
Ama anaongea hivyo kwa sababu wameshindwa?Wangeshinda si wangesema atleast our Billions did not go to waste?
Msekwa asitufanye watoto!He is in the system and he is there to protect his party and its well being!Chama chote kilihamia Tarime kasoro Mwenyekiti wake na nadhani kama siyo safari ya Mbeya na yeye angeenda kuweka kambi huko!
 
Ndugu Ladslaus,



Hawa baadhi ya wanachama wachache wameweza kuishi na kustawi ndani ya chama ambacho kamanda wake alisema hana ubia na mtu kwa namna gani. Je wanachama hao walio wengi wamewezaje kuvumilia huo uchafu kwa karibu miaka mitatu bila kuufagia. Hivyo nina kila sababu ya kusema UFISADI ndani ya CCM ni way of life.



Kama unasikia uzuzu (samahani sikutukani) ndani ya CCM ndio huu. Mwenyekiti wa CCM ambaye tena ndiye Rais wa Tanzania alipewa mandate na asilimia karibu 80% ya wananchi ailinde na kuitetea katiba ya Tanzania. Aliapa kudumisha utawala wa kisheria halafu siyo tu amezungukwa na washauri wanaompotosha, anakuta hana ubavu wa kupambana nao. Anakula na MAFISADI sahani moja na hapo hapo aitwe msafi. Labda unipe tafsiri yako ya neno msafi.



Hatakuwa wa kwanza kufanya hivyo na kuna wengi tu wamemtangulia. Swali ni kwa nini mtu anayetukana CCM leo kesho apokewe kwa shangwe na vifijo akirejea tena kama chama ni makini. Hii inaonyesha kuwa ndani ya CCM, the end justifies the means. Ni matumbo tu yanayowapeleka watu CCM na siyo maslahi ya taifa.



Huo ndio udhaifu wa JK kama kiongozi na CCM kama chama. Mwanawasa aliamua kufanya kweli, JK amesalimu amri na badala yake amebaki kutalii nchi za nje kuyakwepa majukumu ya nyumbani. What a shame.




Ni kweli CCM huwezi kuilinganisha na chama chochote hapa Tanzania kwa sababu ndicho kimepewa nafasi ya uongozi kikashindwa. Wala rushwa wanapeta, wezi wanatanua, wahujumu uchumi ruksa......looo dola imekwenda usingizi na kamanda anatalii. Hao CCM wenye uchungu wako wapi ? Ndugu zangu Ladslaus, Bibi ntilie, Gembe, Masatu, Mtanzania, Fairplayer na wengine wengi tu, mko wapi na haya hamyaoni. FMES ameweza kuyaona mengine lakini kasahau kimoja muhimu - the buck stops with the President.

Wewe ni wa kupuuzwa tu...
 
sasa yeye atahoji vipi matumizi ya helcopter wakati yeye ni moja wao? au walimficha?
Mimi naona anacho takiwa kulalamika ni kupewa wasaidizi wasio na uelewa kwenye kazi ya kukiimarisha chama na kwenye huo uchaguzi. Once akipata watu kama hao mambo ya helcopter etc yatapotea kimya kimya
 
ameuliza swali ambalo tungemuuliza yeye, kama walikuwa wanajua jimbo la Tariime lisingebadilisha mwelekeo wa Bunge (siyo kama Bunge lilikuwa linategemea kiti kimoja kuvunja a tie), sasa kwanini hata walishiriiki uchaguzi? Si ingekuwa bora kama wangewaacha wapinzani wachuane wenyewe!?


A good example happenned here in UK, when a shadow home secretary David Davis from Conservative resigned as MP to seek re-election against the 42 days detention proposal put forward by Labour governement.

Labour knew that, this could be a stunt by the said MP decided not to oppose him by not fielding a candicate for this by-election, hence Mr. David Davis ended up contesting with Independents and other small parties.

More Information.

Haltemprice and Howden by-election results - Telegraph

BBC NEWS | Politics | In full: Haltemprice candidates


NB: Kwa vyovyote vile CCM walijua watashinda Tarime kwa kutumia msuli wa pesa .......kama sehemu nyingine.
 
Huyu jamaa sindio yule ambae alimuambia warioba anyamaze?sasaleo anasema nini inaoyesha alipotakiwa kuenda tarime huyu mzee alikuwa hajui huko tarime kunanini pengine aliambiwa na wenzake anakwenda kufungua tawi na kuweka jiwe la msingi kwa kama anjua tarime kuna nini basi yeye alikuwa nauwezo wa kuwwaambie wenzake nini cha kufanya hapohapo dar bilya ya kufika hata kimara kwa hiyo mzee wetuumekubali kuburuzwa mpaka wakati wakurudi ndio unaulizia wapi kule tulikokwenda? hiyo ni ishara tosha ya kwamba ccm haina viongozi wanaoona mbali hata kidogo wana tiwa katika pakacha na makamba
mimi ninao muheshiwa kama unayajua yoote hayo nenda upesi kamumbe radhi mzee warioba sio kuwa hautakuwa mwana ccm uccm wako upopale pale na kwa haraka uamue kujiuzulu huo wadhifa kwani hao wenzako wooote hapo juuni ni akina jangala na majuto ni bora tu ujipumzikie huwezi ukjisifu kuwa ulikuwa na nyerere halafu ukakubali kukokotwa na kizza makamba.
 
kwa upande mwingine,

Wananchi wa Tarime wanafurahia mabilioni (bill 2 za ccm) ya pesa yaliyomwaga Tarime na pesa zingine zilizotumika kuweka mafuta kwenye mashangingi ya matajiri wanaoimiliki nchi yetu. Kwa wanafunzi wa uchumi kama mimi, multplier effect ya hizi pesa itakuwa kubwa tu na wananchi wa Tarime angalau kwa mara ya kwanza tangu uhuru (1961) wamekumbukwa na serikali yao (bil 2 kutumika Tarime ndani ya mwezi mmoja?!)
 
Yaliyojitokeza hukoo tarime

Baada ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime kumalizika baadhi ya watu waliokuwa wameletwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameshindwa kuondoka mjini hapa baada ya kukosa 'mbovu za nauli' nauli.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Makongoro Nyerere, alisema kumetokea malalamiko ya wafuasi wa chama hicho, baada ya kushindwa kusafiri.

Makongoro alisema baada ya viongozi wa waandamizi waliokuwepo hapa walijisapia ghafla hata kabla ya kutangazwa matokeo ya ubunge na udiwani juzi.

Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mwera, aliibuka mshindi baada ya kupata kura 34,545 dhidi ya mpinzani wake wa CCM, Christopher Kangoye.

Hatua ya kuondoka viongozi waandamizi wa CCM akiwemo, Katibu Mkuu Yusuf Makamba, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hizza na wengine wengi kimeonekana kuacha kilio kikubwa kwa watu waliotegemea kupewa fedha kwa ajili ya nauli ya kuwasafirisha.

baadhi ya wananchi waliweza kunong'ona chini chini kwamba, wameleta Tarime kwa ahadi nyingi na Makamba wakiwemo na viongozi wengi lakini sasa mambo
yamekuwa si mambo.

Kuna baadhi ya wafuasi wamekuwa katika wakati mgumu kupata mlo wa mchana na jioni, kutokana na kuishiwa mbove, hali ambayo wamesema kama ikiendelea itawaweka katika wakati mgumu.

Na inasemekena kwamba viongozi wametoroka Tarime baada ya kubaini kwamba wametokota kwenye uchaguzi..., ila ukweli ni kwamba wameondoka kama watu wengine wanavyoondoka katika safari zao.

Naye mbunge mteule wa Tarime, Charles Mwera, amesema kazi ya kwanza kuifanya kwa wananchi wa Tarime ni kuhakikisha anaendeleza yale yote yaliyokuwa yakifanywa na mtangulizi wake, marehemu Chacha Wangwe.

Alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati alipokuwa akiagana na timu yote ya Darhotwire, walipojumuka katika uchaguzi huo kwa madhumuni ya kunyaka habari hizo.
 
2008-10-15 10:31:52
Na Mawazo Malembeka, PST Iringa

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeendelea kupata matokeo mabaya baada ya kuangushwa na TLP katika uchaguzi mdogo wa udiwani kwenye Kata ya Lupingu, Wilaya ya Ludewa mkoani Iringa.

Hata hivyo, uongozi wa Mkoa wa CCM, umetoa mpya baada ya kuwatupia lawama walimu kutokana na matokeo hayo.

Katika uchaguzi huo, mgombea kupitia Chama cha TLP, John Kiyowi amepeleka machungu mengine kwa CCM baada ya kumshinda mwenzake wa CCM, Cornely Lusambo.

Uchaguzi huo mdogo ulifanyika sambamba na uchaguzi wa mbunge na diwani jimbo la Tarime mjini uliokuwa umevuta hisia za Watanzania wengi ambao pia ulimalizika huku CCM ikibwagwa na (Chadema).

Habari zilizothibitishwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Kapteni Mwapinga na Katibu wa TLP wa wilaya ya Ludewa, Yusuph Kayombo zimesema Kiyowi wa TLP alishinda kiti hicho cha udiwani baada ya kupata kura 653 dhidi ya mgombea wa CCM aliyepata kura 578.

Akizungumzia matokeo hayo, Katibu wa CCM wa Mkoa, Mwapinga alisema hasira za walimu waliokuwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura dhidi ya serikali ya CCM kutokana na madai ya haki zao, ndio zilizosababisha waangushwe katika uchaguzi huo.

``Unajua walimu wana ugomvi na serikali ya CCM dhidi ya madai yao mbalimbali yakiwemo ya mishahara, tunaamini ugomvi huo umechochea watu kukinyima kura chama chetu kwa sababu hao wana watu wengi nyuma yao,`` alisema.

Kumekucha Wazalendo tulitose hili genge la miungu watu linaloamini lina monopoly katika uongozi nchini. CCM imepoteza dira na inatupeleka kubaya.
 
Na bado................. watapigika kisawa sawa.
Hivi huyu katibu wa mafisadi anadhani walimu si sehemu ya watanzania? Kwa hiyo kama walimu ndiyo wamesababisha hii si ni nzuri? maana hawa ndiyo wasimamizi wa kura siku zote. Ina maana tayari sisiemu imeshatangaza kushindwa chaguzi zote?
 
Wewe ni wa kupuuzwa tu...

Masatu,

Hebu soma hii barua;

Baba, hii nd`o Tarime!

2008-10-14 21:08:36
Na Emmanuel Lengwa, Jijini

Kwako Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Salaam! Ama baada ya maamkizi, sisi wanao tunapenda kukujulisha kuwa tunakukumbuka sana, kwani leo ni mwaka wa tisa sasa tangu Mungu Muumba alipokupenda zaidi kuliko sisi wanadamu na kuonyesha mapenzi yake kivitendo kwa kukutwaa na kukusetiri kwenye nyumba ya milele.

Baba, wanao tumekumisi, tena sana tu. Na mara zote tumekuwa tukikukumbuka kwa mengi mema uliyotuachia.
Baba, pamoja na ukweli kwamba salam zetu hizi zaweza zisikufikie kwa namna tunayoitarajia, lakini bado tunashawishika kufanya hivyo, lengo ikiwa ni kukueleza walau kwa uchache juu ya yale yanayojiri sasa katika Tanzania hii ambayo baadhi wameanza kutenda kinyume cha wosia wako.

Baba, tutakwambia kitu kimoja ambacho kwa vyovyote vile, huenda ungependa kukifahamu, japo kwa uchache sana.
Baba, juzi kulifanyika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime kule mkoani Mara, jirani na kijiji ulichozaliwa cha Butiama.

Baba, katika uchaguzi huo, chama kimojawapo machachari cha upinzani nchini kiitwacho CHADEMA kiliweza kutwaa ubunge na pia udiwani, baada ya kukigalagaza vibaya chama ulichokiasisi cha CCM na vingine kadhaa vya upinzani.

Baba, si unakumbuka yale maneno yako uliyotuachia kama wosia kuhusiana na masuala ya madini?

Baba, si unakumbuka kuwa siku zote ulipenda Watanzania wanufaike zaidi na raslimali walizojaaliwa na Mungu Muumba badala ya kuwaachia wageni waje wanavyotaka na kujichotea midhahabu na maalmasi yetu kwa ujira kidogo huku wakituachia mahandaki yasiyo na ukomo?

Baba, basi kwa kukumbukia wosia wako, leo hii CCM imejikuta ikitoswa kule Tarime baada ya kushindwa vibaya.

Baba, wagombea wa upinzani wametumia gia ya kuwaambia wananchi kuwa CCM ya sasa imesahau wosia wako kwa kutowawezesha wananchi wa Tarime kunufaika na raslimali tele walizo nazo.

Baba, wapinzani wakiongozwa na viongozi wao kitaifa, wakadai mbele ya wananchi wa Tarime kuwa eti, kwa kusahau wosia wako kuhusu ustawi wa Watanzania, CCM imekuwa ikitilia mkazo mdogo katika kukomesha vita vya koo jimboni humo na kwamba wao ndio wanaoweza kupunguza madhila hayo.

Kwa sababu hiyo, na maelezo mengine mengi ambayo wapinzani waliwalisha wananchi wakati wa kampeni, CCM ikajikuta ikiadhibiwa kwa mgombea wake wa ubunge Bw. Chrisopher Ryoba Kangoye kuambulia kura 2,8919 huku yule wa CHADEMA, Bw. Charles Mwera akishinda kwa kuzoa kura 34,545 Baba, pamoja maamuzi hayo ya wananchi kupitia demokrasia ya visanduku vya kura, bado jimboni humo ambako ni jirani tu na nyumbani kwako Butiama, kulishuhudiwa vurugu ambazo enzi zako haziwahi kuwepo.

Baba, askari polisi wanaolipwa mishahara kwa kodi za Watanzania, walijikuta wakitumia mgari mkubwa wenye maji ya upupu, almaarufu kama `washawasha` kwa ajili ya kuwadhibiti wananchi walioadaiwa kufanya vurugu wakati wa uchaguzi huo.

Baba, si hayo tu. Virungu pia vilitumika, mibomu ya machozi nd\'o usiseme.

Kabla ya matokeo ya jana, karibu watu wengi walijikuta wakimwaga machozi hadharani kutokana na athari ya mabomu hayo ambayo yalimwagwa kiusongo na askari kibao waliopelekwa huko kwa ajili tu ya uchaguzi huo.

Baba, cha kusikitisha zaidi, baadhi ya wananchi walitaka kugeukia mambo yaliyotokea Burundi na Rwanda enzi zile, kwa kutembea na mapanga na visu mitaani huku wakiwachapa wenzao kama wanyama, eti kisa sababu za kutofautiana kwao kiitikadi.

Baba, pamoja na yote hayo, ambayo wengine wanadai kuwa ni matokeo ya kusahau wosia wako kuhusu umuhimu wa amani na utulivu nchini, hatimaye wana Tarime wamepata chaguo lao.

Baba, leo hii, kama tulivyokwambia hapo juu, Mwera ndiye Mbunge wa Tarime, akishika nafasi iliyoachwa wazi na marehemu Chacha Wangwe, ambaye alikuwa ni mbunge mwingine wa jimbo hilo asiyekuwa wa CCM.

Baba, yapo mengi ya kukusimulia yakiwemo mazuri kama kujengwa mashule kibao ya sekondari, tena kwa kila kata.
Baba, pia Serikali ina mpango wa kujenga zahanati katika kila kata, kupitia mpango unaofanana na ule wa maendeleo ya elimu ya msingi ambao wenyewe umewezesha shule kibao za msingi kujengwa.

Baba, yapo mambo mengi sana, lakini kwa uchache tuliamua tukudokezee zaidi suala hilo la Tarime.

Baba, ila siku nyingine, tutajitahidi kukueleza kuhusu maskendo kibao yanayotokea nchini hivi sasa, na ambayo enzi zako ilikuwa nadra kuyasikia.

Baba, tukudokezee kidogo? Ni hivi, kuna masuala ya mafisadi wa EPA ambayo Watanzania wana hamu ya kujua wahusika watachukuliwa hatua gani baada ya kukomba bilioni 133 kiujanjaujanja toka BoT.

Pili, kuna suala la Richmond, ambalo wahusika wake waliingiza nchi katika mkenge kwa kusaini mkataba bomu wa kuzalisha umeme uliotugharimu mabilioni ya pesa.

Pia, kuna suala la mgodi wa Kiwira, mikataba inayotiliwa shaka katika madini na mengine mengi, ambayo kama tulivyokuahidi, ipo siku tutakupa `full story` ya mambo hayo.

Baba, kwa leo wacha tuishie hapa.
Tunakutakia mapumziko ya amani huko uliko.
Alamsiki!
 
Hivi hii helikopta waliikodi wapi?

Hivi ni kweli kuwa CCM waanalipia kumbi za mikutano za jengo la Bunge? Kwa wale waliokuwa na ufahamu ktk miaka ya 70 watakumbuka jinsi watanzania walivyochangia ujenzi wa makao makuu, Dodoma. K/hiyo, CCM hawapaswi kuzifanya kumbi hizo kuwa ni za chama.
 
hivi uchaguzi mdogo biharamulo ni lini???...........maana wakati umefika...kwa utendaji wa kisanii wa jk ..mwaka 2010..wapinzani watapata zaidi ya asilimia 40 za viti vya bunge...

inatakiwa baada ya kushinda tarime wapinzani wangepata kausafiri wafanye ziara nchi nzima dubbed kumtambilisha mbunge wao mpya ...waanzie kanda ya ziwa ..up..
 
Safi sana ! Iliandikwa hapa jf kuwa hakuna dola linalodumu milele ila la mwenyezi mungu, kama dola la kirumi ccm imeanza kumeguka kiapnde kipande toka tarime hadi ludewa huu ndo mwanzo wa mwisho wa dola laccm
 
SAHIHISHO MUNGU IN CAPITAL LETTER, HIS OMNIPOTENT, THE NAME Above all the names
 
wapambe wa CCM waachwa bila nauli Tarime

na Kulwa Karedia, Tarime

SIKU moja baada ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime kumalizika baadhi ya watu waliokuwa wameletwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameshindwa kuondoka mjini hapa baada ya kukosa nauli.

Habari za uhakika zilizopatikana mjini hapa jana na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, zinasema kumekuwepo na malalamiko ya wafuasi wa chama hicho kushindwa kusafiri hasa baada ya viongozi wa waandamizi waliokuwepo hapa kuondoka ghafla hata kabla ya kutangazwa matokeo ya ubunge na udiwani juzi.

Katika kinyang’anyiro hicho, mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mwera, aliibuka mshindi baada ya kupata kura 34,545 dhidi ya mpinzani wake wa CCM, Christopher Kangoye.

Hatua ya kuondoka viongozi waandamizi wa CCM akiwemo, Katibu Mkuu Yusuf Makamba, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hizza na wengine wengi kimeonekana kuacha kilio kikubwa kwa watu waliotegemea kupewa fedha kwa ajili ya nauli ya kuwasafirisha.

Mmoja wa wanaCCM ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alisema kitendo walichofanyiwa na viongozi hao ni funzo kubwa kutokana na ukweli kuwa waliahidiwa fedha kwa ajili ya masuala mbalimbali yakiwemo nauli, posho na fedha za kujikimu kwa siku ambazo walikuwa mjini hapa.

Alisema baada ya kukimbiwa na viongozi hao, hivi sasa wamebaki kuwa ombaomba na hawajui nini hatima yao ya kuendelea kubaki hapa huku shughuli zao nyingi zikikwama kutokana na kushindwa kuondoka.

“Tumeletwa Tarime kwa ahadi nyingi na Makamba na viongozi wengi lakini sasa mambo yameharibika wameamua kutukimbia, tena bila hata kutuaga, maana tumekuja kumuona Makamba kwenye luninga akizungumza na waandishi wa habari mjini Mwanza juzi... sasa tabia kama hii inajenga picha gani katika siku zijazo?” alihoji mwanachama huyo.

Alisema mbali yake yeye kuna baadhi ya wafuasi hao hivi sasa wamekuwa katika wakati mgumu kupata mlo wa mchana na jioni kutokana na kuishiwa fedha, hali ambayo wamesema kama ikiendelea itawaweka katika wakati mgumu.

Lakini kwa upande wake, Makongoro alisema amesikia kuwepo kwa suala hilo lakini aliahidi kuwasiliana na viongozi wenzake wa chama haraka, ili kubaini ukweli kama ni kweli au la ili waone namna ya kuchukua hatua haraka ili kunusuru watu hao.

“Nimesikia kuwepo kwa malalamiko hayo na tayari kuna waandishi wa habari wamenipigia simu kuulizia tatizo hili... napenda kutumia nafasi hiyo kuwaomba kwanza niwasiliane na wenzangu ili tuone ni kweli au la,” alisema Makongoro.

Alipoulizwa juu ya viongozi wa CCM kuondoka kimya kimya mjini hapa, Makongoro hakuwa tayari kutoa sababu za kukubali au kukataa zaidi ya kusisitiza kwamba wameondoka kwa taratibu za kawaida kama siku zote.

“Hivi sasa kumekuwepo na uvumi mwingi kwamba viongozi wetu wametoroka hapa Tarime baada ya kubaini kwamba tumeshindwa kwenye uchaguzi... ukweli ni kwamba wameondoka kama watu wengine wanavyoondoka katika safari zao, sasa nashangaa kusikia kwamba wametoroka,” alisema Makongoro.

Katika hatua nyingine, mbunge mteule wa Tarime, Charles Mwera, amesema kazi ya kwanza kuifanya kwa wananchi wa Tarime ni kuhakikisha anaendeleza yale yote yaliyokuwa yakifanywa na mtangulizi wake, marehemu Chacha Wangwe.

Alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati alipokuwa akiagana na timu ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali hapa nchini, waliokuwa hapa kwa ajili ya kuripoti habari za uchaguzi.
 


chama kinapogombea, mwenyekiti wa kile chama ni lazima awepo hakuna excuse hapo!

..kabisa mkuu ..kikwete also shares party of blames....unajuwa strategy ya chadema ilikuwa kali....kuhusu kumshirikisha mwenyekiti wao wa chama...they left people guessing ...and never disclose if he would attend....has ukizingatia na zile shutuma kuwa mbowe alikimbia tarime na anaogopa kwenda.....kila mtu alikuwa anajuwa hangekwenda.....IWAPO MBOWE ANGEWAHI TARIME KAMA WENGINE...ANGESABABISHA CHADEMA KUSHINDWA KWANI ANGEKUWA NA MUDA MREFU ZAIDI WA KUWA CENTRE OF ALLEGATION ,...NA ANGEISHIA KUGEUZWA KITUKO ..ZAIDI PIA ANGEWEZA KUANDALIWA WATU WA MUMZOMEA KWELI...KWA KITENDO CHA KWENDA MWISHONI ..AMEKUWA THE REALLY LAST CARD NA MSAADA KWA CHAMA CHAKE.....

Sasa kitendo cha mbowe kutua ghafla tarime kama mwewe kilimfanya kila mmoja kujuwa atasema nini hasa ukizingatia propaganda zilizokwisha mwagwa mwezi mzima....that helped mbowe to pull crowd......na kwa kuwa alikuwa ameshaandaa maneno ya kuwaambia kutokana na propaganda chafu kuwa hangeenda ..that gave chadema more credits..

The fact kwamba mbowe alienda zimebaki siku 4 ....was good kwa kuwa kina makamba walishaongea yote ...hawakuwa tena na jipya.....kina zitto pia walishasema yao...so mbowe alikuja kumalizia kazi yao nzuri.....na ukizingatia aliingia na nguvu ya helicopter na ndani ya siku nne alipita kila mahali..

Kwa uchambuzi wangu...mtu pekee ambaye angeweza angalau ku cover hiyo gap ya kura 7000 walizowazidi chadema..ni kikwete ...tena hata kina makamba wamejitahidi sana....hawakuwa tena na hoja...laiti na yeye angeingia mwishoni kama mbowe ........angeweza kubadili mawazo ya undecided voters ......kwani waliotoa ushindi tarime ni undecided voters ..kwa hali ile ya low voters turn out..kila chama kilipigiwa kura na wapenzi wake walio sacrifice kujitokeza .......na wachache ambao si wakereketwa walishawishika kujitokeza ndio waliamua
mshindi....

Lakini vile vile kitendo cha rais kutokwenda kinaweza kuwa kimemsaidia....kiusalama ..na pili kisiasa....kwani angeweza kuvuna aibu ya kuzomewa..kurushiwa mchanga,mawe ..potelea mbali hata kama yasingemfikia kutokana na ulinzi wake...but ujumbe ungekuwa umefika...na pia angeweza kushindwa uchaguzi vilevile..matokeo yake ingeporomosha zaidi umaarufu wake kitaifa...

Mbeleni tutarajie upinzani kuendelea kupata nguvu kwani uchaguzi huu umebakisha vyama makini vitatu tanzania..ccm.chadema na cuf...vyama vya nccr,tlp ..et al vimejimaliza uchaguzi huu kwa kuonekana wazi kukubali kutumiwa ...hasa kueneza propaganda chafu...hii itawasaidia watanzania kujua waweke wapi matumaini yao...na kwa hapo tutafikia kwenye utabiri wa nyerere kuwa vyama vibaki vichache makini na kwa tanzania [bara]..chadema ndicho chama makini kwa mtazamo wa mwalimu julius kambarage nyerere,,,,.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom