Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Mods hongereni kwa kuweka heading sawa.Nashukuru sana kwa umakini wenu.Keep up the same spirit!
 
Kwa habari zilizonifikia ni kwamba last week viongozi wakuu wa CHADEMA walimfata kijana mmoja aliyekuwa machachari kwenye siasa za vyuo vikuu nchini ambae hafungamani na upande wowote kisiasa za vyama wakijaribu kumshawishi akagombee Tarime maana wanaona anauzika na the fact kwamba ni mtu wa huko wakadhani anaweza kuwatoa kimasomaso, baada ya kuongea naye sijui walichokubaliana kimsingi japo walisema pia ikiwa yeye hataki awaonyeshe mtu anayedhani anaweza kuuzika wa huko, ila cha ajabu ni kwamba baada ya muda Mzee Kingunge akampigia simu huyio kijana akimwambia "nasikia umefatwa kushawishiwa kijana mbona hatuambiani?" Sasa kitu cha kushangaza ni kwamba nani alimwambia Kingunge hiyo ishu au humohumo ndani ya chadema ndo wamo informers wa ccm? je namna hii kweli chadema watatoboa kama kila wanachofanya ccm wanakijua within minutes? Je ni kweli hawana mtu tarime wa kugombea au wanatishwa na propaganda za ccm? Si wanifate mimi nikagombee, kwi, kwi,kwi.........
 
Kwa habari zilizonifikia ni kwamba last week viongozi wakuu wa CHADEMA walimfata kijana mmoja aliyekuwa machachari kwenye siasa za vyuo vikuu nchini ambae hafungamani na upande wowote kisiasa za vyama wakijaribu kumshawishi akagombee Tarime maana wanaona anauzika na the fact kwamba ni mtu wa huko wakadhani anaweza kuwatoa kimasomaso, baada ya kuongea naye sijui walichokubaliana kimsingi japo walisema pia ikiwa yeye hataki awaonyeshe mtu anayedhani anaweza kuuzika wa huko, ila cha ajabu ni kwamba baada ya muda Mzee Kingunge akampigia simu huyio kijana akimwambia "nasikia umefatwa kushawishiwa kijana mbona hatuambiani?" Sasa kitu cha kushangaza ni kwamba nani alimwambia Kingunge hiyo ishu au humohumo ndani ya chadema ndo wamo informers wa ccm? je namna hii kweli chadema watatoboa kama kila wanachofanya ccm wanakijua within minutes? Je ni kweli hawana mtu tarime wa kugombea au wanatishwa na propaganda za ccm? Si wanifate mimi nikagombee, kwi, kwi,kwi.........

Huu nao ni udaku. Hebu tuambie ni kiongozi gani wa CHADEMA huyo! Kule CHADEMA ni chama tawala, kina watu mashuhuri kama yule Mwenyekiti wa Halmashauri Bwana Mwera halafu kuna yule bwana Sasi ambaye gazeti la Mwananchi lilimuandika kwa kirefu kuwa CCM ilimuandamana zaidi hata ya Chacha. Na yuko kule Tarime, kwa nini asigombee? mi naamini wako wengi tu. Labda bado wako kwenye maombolezo ndio maana hawasemi chochote kuhusu mgombea sasa hivi. Kwani tume imeshatangaza uchaguzi tayari jamani? Marehemu hata siku arobaini hajakaa!

Asha
 
Dada Asha,
Mbona mipango ya kulitwaa jimbo CCM walii ianza hata kabla marehemu hajawekwa kwenye nyumba ya milele?

Wewe unadhani zile taarifa za kukinzana zilizo tolewa na baadhi ya vyombo vya habari kwa makusudi mazima wakati wa msiba zilikuwa za bure? ndo kazi ilisha anza dadangu!

na hapo ndipo najikuta nikijawa na hofu kuuubwa juu ya vifo tata kama hivi, yumkini ...
 
Ni mapema mno kusema CHADEMA hawana mtu, ninachojua kulikuwa na mpango wa kikao kwa CHADEMA kujadiliana nani agombee na walikubaliana kuwa watakifanya baada ya msiba kwisha, lakini Haraka haraka walimfikiria mdogo Wangwe aitwaye Keba hawakuelewana. Ila nimesikia Gachuma nae alikuwa akitaka kugombea nafasi hiyo na tayari alikuwa ameanza mkakati huo. ngoja tufatilie kwa karibu taarifa hizi tutajuzana
 
Huu nao ni udaku. Hebu tuambie ni kiongozi gani wa CHADEMA huyo! Kule CHADEMA ni chama tawala, kina watu mashuhuri kama yule Mwenyekiti wa Halmashauri Bwana Mwera halafu kuna yule bwana Sasi ambaye gazeti la Mwananchi lilimuandika kwa kirefu kuwa CCM ilimuandamana zaidi hata ya Chacha. Na yuko kule Tarime, kwa nini asigombee? mi naamini wako wengi tu. Labda bado wako kwenye maombolezo ndio maana hawasemi chochote kuhusu mgombea sasa hivi. Kwani tume imeshatangaza uchaguzi tayari jamani? Marehemu hata siku arobaini hajakaa!

Asha

Asha mdaku nani sasa? Kama huamini muulize mbowe akanushe? mi sijaona ubaya wowote juu ya wao kutafuta mgombea, na hata mimi japo sina chama kisiasa ningependa sana wapinzani waongezeke bungeni hivyo nisingependa kuona ccm wanashinda tarime, ndo maana najiuliza kwa nin i info za chadema zinaleak kwa ccm? nani anayetoa hizo info? Na kama ulidhani hawajaanza process za uchaguzi pole sana dada.Lakini huo ndo ukweli waulize tu wakulu huko chadema waprove.
 
Inawezekana kabisa CHADEMA wanashindwa kuzichanga vyema karata zao kwa kuwa kuna ishu ya kutegeana katika kuteua wagombea.CCM wananyemelea pengine CHADEMA itangaze mgombea ndipo nao watangaze yule ambaye wanahisi anaweza kuhimili nguvu ya CHADEMA.

Ushauri wangu ni kuwa CHADEMA makao makuu wangetegemea sana wanachadema wa kulekule Tarime na pengine waliopo kulekule ambao wanajulikana na wanarekodi nzuri ya utendaji chamani na jimboni.Wanachadema wa Tarime wapewe fursa ya kuteua mrithi wa Wangwe, bila shaka watampitisha hata kwnye uchaguzi lakini siyo kupelekewa mtu kutoka mjini eti tu kwasababu amezaliwa Tarime.Ishu sasa ni kuwa CCM watacheza katara kwa kutumia kifo cha Wangwe na Chadema wakizubaa tu watapigwa bao.
 
Na hii nimeikuta HabariLeo, inaelekea mambo hayaendi sawa

Chadema yapata pigo John Nditi, Morogoro
Daily News; Monday,August 11, 2008 @08:36

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Morogoro kimepata pigo baada ya viongozi wake wawili wakuu kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Viongozi hao ni Katibu wa Wilaya ya Ulanga wa chama hicho, Said Kaole na Katibu Msaidizi wake Hassan Mohamed.

Viongozi hao walikuwa ni miongoni mwa wanachama 40 kutoka vyama vya upinzani walioamua kuvihama vyama vyao na kujiunga na CCM mwishoni mwa wiki.

Wanachama hao wapya walikabidhiwa kadi za CCM na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba wakati wa ziara yake ya siku saba mkoani Morogoro.

Mbali na idadi hiyo ya wanachama wa upinzani kurejea CCM, watu 396 walijiunga na chama hicho na kupewa kadi za uanachama pamoja na kufunguliwa kwa mashina 17 ya CCM na Katibu Mkuu huyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanachama waliorejea kutoka kambi ya upinzani walidai kuwa wameamua kujiunga na CCM kufuatia utekelezaji mzuri wa Ilani yake juu ya kuwapatia wananchi maendeleo ya kweli, ikiwamo ujenzi wa shule za sekondari, zahanati na maji safi tofauti na ilivyo kwa vyama hivyo wa upinzani.

Makamba aliwataka viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya shina, tawi, wilaya na mikoa kuanza kwenda kwa wanachama kuimarisha uhai kwa ajili ya kukipatia ushindi katika uchaguzi wa Serikali za mitaa wa mwaka ujao na uchaguzi mkuu wa 2010.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo, CCM imeamua kuanza mikakati yake ya ushindi kwa uchaguzi huo ili kuweka mazingira ya kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao.

"Viongozi wa CCM wa ngazi zote sasa hakuna kulala …ni wakati wa kwenda kwa wananchi na wanaCCM kushughulikia matatizo yao na kuyazungumzia yale tuliyotekeleza," alisema Makamba.

HabariLeo
 
Marehemu Chacha Wangwe alikuwa na MVUTO wa AINA yake kwa watu wa Tarime. Kwa kuwa amefariki, JIMBO hili liko wazi kwa chama chochote kile ikiwemo CCM. Kosa walilolifanya CCM 2005 hawawezi kulifanya tena mara hii.
 
Uchaguzi utafanyika kati ya mwezi march na april 2010. Hekaheka za uchaguzi huambatana na matumizi makubwa ya fedha (chakula, malazi, spika, magari, diesel na posho za wapiga debe/wapambe), marehemu alifadhiliwa na G9 baada ya NEC kumpitisha kwa nguvu Kisyeri Chambiri ambaye hakutakiwa. Kumbuka Kisyeri Chambiri alishindwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM.

Kwa sasa G9 hawana sababu tena ya kufadhili chadema kwani shida yao ilikuwa kumwondoa chambiri kwa vyovyote vile.

Chadema haina hulka ya kufadhidi kampeni za wagombea ubunge wake labda ianze sasa! Uchaguzi huu utakuwa na vurugu nyingi na matumizi makubwa ya nguvu na fedha hivyo baada ya matokeo wananchi wakawaida watakuwa wamechoshwa na siasa.

Then, octoba 2010 kutakuwa na uchaguzi tena wa madiwani wabunge na rais, kampeni zitaanza upya tena, nguvu yote ya chadema itahamia kwenye urais na akina slaa/zitto watakuwa majimboni kwao wakihangaika, hapo ndio itakuwa mwisho wa chadema tarime, hawatapata hata udiwani.
 
Jinsi Siasa za Tanzania Zilivyo...Itakuwa Maajabu Lile Jimbo Likichukuliwa Tena Na Chadema.
 
Jinsi Siasa za Tanzania Zilivyo...Itakuwa Maajabu Lile Jimbo Likichukuliwa Tena Na Chadema.

Mimi nadhani hiyo ndio siasa nzuri maana kwa vyovyote vile Zitto alichaguliwa kama yeye sio kama CHADEMA, marehemu Wangwe... the same...

In fact mimi napenda wananchi wachague viongozi wazuri regardless wanatoka chama gani...

Ni kazi ya vyama kusimamisha wanachama wao wazuri...

Mungu Ibariki Tanzania
 
Uchaguzi utafanyika kati ya mwezi march na april 2010. Hekaheka za uchaguzi huambatana na matumizi makubwa ya fedha (chakula, malazi, spika, magari, diesel na posho za wapiga debe/wapambe), marehemu alifadhiliwa na G9 baada ya NEC kumpitisha kwa nguvu Kisyeri Chambiri ambaye hakutakiwa. Kumbuka Kisyeri Chambiri alishindwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM.

Kwa sasa G9 hawana sababu tena ya kufadhili chadema kwani shida yao ilikuwa kumwondoa chambiri kwa vyovyote vile.

Chadema haina hulka ya kufadhidi kampeni za wagombea ubunge wake labda ianze sasa! Uchaguzi huu utakuwa na vurugu nyingi na matumizi makubwa ya nguvu na fedha hivyo baada ya matokeo wananchi wakawaida watakuwa wamechoshwa na siasa.

Then, octoba 2010 kutakuwa na uchaguzi tena wa madiwani wabunge na rais, kampeni zitaanza upya tena, nguvu yote ya chadema itahamia kwenye urais na akina slaa/zitto watakuwa majimboni kwao wakihangaika, hapo ndio itakuwa mwisho wa chadema tarime, hawatapata hata udiwani.

Does that mean jimbo halitakuwa na mwakilishi hadi 2010? Thats very long, why?
 
Kwa habari zilizonifikia ni kwamba last week viongozi wakuu wa CHADEMA walimfata kijana mmoja aliyekuwa machachari kwenye siasa za vyuo vikuu nchini ambae hafungamani na upande wowote kisiasa za vyama wakijaribu kumshawishi akagombee Tarime maana wanaona anauzika na the fact kwamba ni mtu wa huko wakadhani anaweza kuwatoa kimasomaso, baada ya kuongea naye sijui walichokubaliana kimsingi japo walisema pia ikiwa yeye hataki awaonyeshe mtu anayedhani anaweza kuuzika wa huko, ila cha ajabu ni kwamba baada ya muda Mzee Kingunge akampigia simu huyio kijana akimwambia "nasikia umefatwa kushawishiwa kijana mbona hatuambiani?" Sasa kitu cha kushangaza ni kwamba nani alimwambia Kingunge hiyo ishu au humohumo ndani ya chadema ndo wamo informers wa ccm? je namna hii kweli chadema watatoboa kama kila wanachofanya ccm wanakijua within minutes? Je ni kweli hawana mtu tarime wa kugombea au wanatishwa na propaganda za ccm? Si wanifate mimi nikagombee, kwi, kwi,kwi.........

DUh hii kali,,, yaani mtu anafuatwa kuombwa, anakujulisha, baadaye anapigiwa simu na Kingunge anakujulisha na wewe unaweka mambo hadharani JF...

Kwa tafsiri yangu, kama hii habari ni ya kweli, basi wewe ndiye kijana mwenyewe, kama si kijana mwenyewe, huyo kijana hafai hata kuongoza mtaa maana hana 'kifua' na katika siasa kunahitajika 'kifua'.
 
DUh hii kali,,, yaani mtu anafuatwa kuombwa, anakujulisha, baadaye anapigiwa simu na Kingunge anakujulisha na wewe unaweka mambo hadharani JF...

Kwa tafsiri yangu, kama hii habari ni ya kweli, basi wewe ndiye kijana mwenyewe, kama si kijana mwenyewe, huyo kijana hafai hata kuongoza mtaa maana hana 'kifua' na katika siasa kunahitajika 'kifua'.

Halisi unongea kama hujui siasa za bongo? siasa zenyewe za kuuwana hizi? Anyway hakuna mahali niliposema yeye mwenyewe kijana ndo kaniambia, no, hii ishu nimeipata tokea ccm huko. Mimi sie yeye na ningekuwa yeye nisingeliweka hili hapa.
By the way mbona wewe huwa unaweka mambo magumu tu hapa JF au sisi haturuhusiwi mkuu? Nafikiri hadi hii ishu ifike hapa unatakiwa tu uwe umeshaelewa kuwa kijana mwenyewe hana mpango na siasa za bongo. Anahitaji bado kuishi bro.
 
Mbona jimbo la Mwibara haujaitishwa uchaguzi mwingine baada ya mahakama ya kuu kutengua matokeo tangu mwaka jana? au jamaa alikata rufaa?
 
Tujaribu kuhakikisha jimbo hili linabaki kwa upinzani lakini au mtu mwenye mawazo ya maendeleo na si mradi tu kama wale wabunge wa CUF!(sorry about this, coz most of them just dont know why they are there!) Apatikane mtu mwenye nia ya kukuza upinzani wa maendeleo na ambaye ataweza kupambana na sera za kifisadi ambazo zinaiumiza Wilaya ya Tarime ambayo Mungu ameijalia utajiri mkubwa wa madini.
 
Mbona hatuongelei tena umoja wa vyama vya upinzani? Ule umoja umeishia wapi?

Kwa mwendo huu sitashangaa upinzani wakibugizwa magoli tena mwaka 2010. Inaelekea bado hawajajifunza na hawataki kutusikia wananchi tunataka wafanye nini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom